Ni lini Amiri Jeshi Mkuu atavaa sare za Askari Polisi au Magereza?

Ni lini Amiri Jeshi Mkuu atavaa sare za Askari Polisi au Magereza?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
FB_IMG_1574289773224.jpg


iko wazi kwamba yeye ndiye kiongozi wa juu kabisa wa majeshi yote nchini.

Swali langu ni dogo tu , ni lini Mheshimiwa atavaa sare za polisi ili kuonyesha kuunga mkono juhudi zao za kupambana na uhalifu au ni lazima avae za JWTZ tu kama ambavyo ameonekana mara kadhaa?

Naomba kuwasilisha.

====
Maoni ya Wadau

Unauliza ili ujue au ili uzonge?

Mpango mzima wa utawala wa kidemokrasia ni mpango mgeni kwetu Tanzania.

Hili la civilian leadership of the military, katika mazungumzo ukilitaja, unaweza kuambiwa "wewe mbona una mind vitu vidogo hivyo?"

Mkapa kakubali CCM wametumia hela za EPA kwenye uchaguzi. Katika kitabu cha kuelezea maisha yake. Na hamna anayemshitaki wala kuanzisha tume ya uchunguzi. Ndiyo kwanza Zitto Kabwe, mwanasiasa maarufu wa upinzani, anamsifia Twitter huyo Mkapa kwa kuandika kwamba yeye Zitto Kabwe amependa sana jinsi Mkapa alivyokuwa mkweli. Utaambiwa "wewe unalalamika rais anavaa magwanda ya jeshi?"

Tumezoea uchifu chifu. Anachosema mkubwa hakiwezi kuwa kosa.

Ndiyo maana habari za demokrasia, bunge la uwakilishi wa wananchi, mihimili mitatu kukinzana, siasa za vyama, ilani za uchaguzi, siasa za sera, chaguzi zenyewe, elimu rasmi hii ya kupewa vyeti, na nyingi zinazofanana na hizo zinakuwa maigizo tu.

Tukirudi kwenye swali lako la kuhusu "Civilian Leadership of The Military", huko tunakoigiza hii demokrasia, waliona ni jambo la hatari kuchanganya siasa na mambo ya jeshi. Wakajiwekea misingi ya kwamba, jeshi litaongozwa na watu wasio wanajeshi waliochaguliwa kwa kupigiwa kura na wananchi. Wakaweka mipaka kati ya jeshi na uongozi wa kiraia utakaoliongoza jeshi.


Ndiyo maana raisi anakuwa Amiri Mkuu wa Jeshi. Sasa rais kuwa Amiri Mkuu wa Jeshi, ili raia wawe wanaongoza jeshi, na si jeshi linaongoza raia, kimuonekano rais akianza kuvaa migwanda ya jeshi bila sababu maalum, anaondoa muonekano wa raia kuongoza jeshi. Anaturudisha kwenye muonekano wa jeshi kuongoza raia.

Muonekano unatengeneza ukweli wake. Kwenye sheria kuna msemo kwamba, haki si tu itendeke, bali pia ionekane kuwa imetendeka. Kwa sababu muonekano wa haki kutendeka unapanda mbegu ya haki zaidi kutendeka na muonekano wa haki kutotendeka, hata kama imetendeka, unapanda fikra za uonevu.

Vivyo hivyo katika uongozi. Katika nchi ya kidemokrasia, jeshi si tu ni muhimu liongozwe na raia, ni muhimu pia lionekane kwamba linaongozwa na raia. Sio mara tu rais anasema angependa kuwa IGP, mara anasema atawapiga mpaka shangazi za wapinzani, mara kavaa migwanda ya jeshi. Shangazi za wapinzani wengine watakosa raha bure wakijua ndio wanakuja kupigwa sasa.

Sisi Tanzania tulivyokuwa tunaingia kwenye vyama vingi, tuliigiza kulijua hili jambo la "Civilian Control of The Military".

Tukawaambia wanasiasa ambao walikuwa wanajeshi pia kina Kikwete, Ditopile, Makamba, Chiligati, Moses Nnauye na wengine kama hao, wachague moja, siasa ama jeshi. Hao niliowataja wote wakachagua siasa.

Kanuni za "Civilian Leadership of The Military" zikazingatiwa. Kikwete aliyekuwa Kamisaa wa Chama jeshini aliyejua habari hizi, licha ya kwamba alikuwa mwanajeshi, sijawahi kumuona amevaa magwanda ya jeshi kama rais nje ya shughuli za kijeshi. Kwa kweli napata kazi ngumu kukumbuka Kikwete akiwa kavaa magwanda ya kijeshi kama rais wakati wowote.

Sasa Magufuli ambaye jeshi ameishia JKT ya lazima, leo kawa rais, anavaa migwanda kama mtoto aliyenunuliwa nguo ya sikukuu ambaye hawezi kujizuia mpaka sikukuu kuivaa hiyo nguo, ananipa shaka kuhusu uwezo wake wa kuelewa au kujali dhana hii ya "Civilian Leadership of The Military".

Si tu kwa sababu anaipa nchi ambayo inatakiwa kuwa ya kidemokrasia muonekano wa kuongozwa kijeshi, bali pia kwa sababu anatuletea mtiririko mzima wa kurudisha jeshi katika siasa.

Ukweli ni kwamba, rais anaweza kuvaa vyovyote anavyotaka. Anaweza hata kuvaa kibwaya cha wacheza ngoma. Lakini je, muonekano wake utakuwaje?

Magufuli hajaishia kuvaa tu magwanda ya jeshi. Ameteua wanajeshi, na ninapoandika wanajeshi simaanishi wanajeshi wastaafu, namaanisha wanajeshi walio jeshini bado, kushika nafasi za kisiasa serikalini.

Wanaochambua mambo wanajua umuhimu wa ualama (symbolism). Magufuli anaposhobokea magwanda ya jeshi anatupa ujumbe gani?

Ndiyo anataka watu walime kwa meno kwa mwendo wa kijeshi?

Kashaliingiza jeshi kwenye manunuzi ya korosho kusini huko. Kaangusha mapato ya mauzo ya kilimo nje kwa asilimia 55, mwaka uliopita unaoishia Agosti 2019 ukilinganisha na mwaka ulioutangulia. Ripoti ya Benki Kuu ya Oktoba 2019 inaonesha hilo.

Anataka kufuta demokrasia na kuongoza nchi kijeshi?

Anataka kufanya Tanzania iwe nchi ya kijeshi?

Is Tanzania a police state?
The answer lies, at your own gate.
 
Nadhani mada yako ungeiwasilisha kama ombi,

"Naomba amiri jeshi kuu siku moja avae sare za jeshi la polisi/magereza/traffic/zimamoto/ffu/mgambo, nione jinsi zinavyomkaa vema...."

Lmao[emoji23][emoji23]
Hata hivyo imekaa kama ombi mkuu , japo nilikuwa napenda sana wanasheria waseme kama kuna lolote kikatiba linalohusiana na mavazi haya , lengo kuu ni kujifunza .
 
View attachment 1267903

iko wazi kwamba yeye ndiye kiongozi wa Juu kabisa wa Majeshi yote nchini .

Swali langu ni dogo tu , ni lini mheshimiwa atavaa sare za polisi ili kuonyesha kuunga mkono juhudi zao za kupambana na uhalifu au ni lazima avae za JWTZ tu kama ambavyo ameonekana mara kadhaa ?

Naomba kuwasilisha

Avae hayo magwanda ili iweje? Mpate sababu mpya za kumnanga au?

Manake si kwamba akivaa sare za Magereza mtakuja hapa na kuanza kumpongeza....

Sanasana mtakuja na kuendeleza yale yale...’oh oneni huyu, sasa anavaa na sare za Magereza. Kaona zile za jeshi hazitoshi. Sasa anataka kuwa kamishna wa Magereza’

Tokeni hapa na unafiki wenu!
 
Eti hili nalo ni hoja ya kisiasa kwa wafuasi was chadema ambao hawajui hata naana ya vazi la jeshi la ulinzi na usalama (_jw tz),

Mkuu tambua rais anapovaa sare za jw ambayo ina rangi za ugoro =jenzi la magereza ,kaki = jeshi la polisi ,kuna kijani ,ambapo kuna jkt nk.akivaa hivyo basi tambua amevaa sare za majeshi yote ,yaani yeye ni amiri jeshi mkuu wa majeshi yote yaliyo inchini ,so akivaa eidha ugoro tu ambayo ni sare ya magereza itakuwa hajafuata protocalli
 
Tanzania dhana ya "Civilian Leadership of The Military" kueleweka vizuri ni vigumu sana.

Sasa naona Magufuli kazidi!

Hii sijui ni mara ya ngapi tu anayavaa hayo magwanda.

Hiyo hapo kwenye video ni leo [11/20/19].

Sina uhakika na mazingira yenyewe [ilikuwa ni kwenye shughuli ya kijeshi? Ya kiraia?].

Kwa muonekano inaonekana kama shughuli haikuwa ni ya kijeshi.

Naweza kuelewa kama shughuli ni ya kijeshi na yeye kama amiri jeshi mkuu labda anataka kuonyesha kuwa yupo pamoja na makamanda wake kwa hali na mali.

Hiyo naweza kuelewa na naweza kuvumilia ikifanyika in small doses.

Ila hapa, hayo magwanda yanahusikaje? Sielewi kabisa. Naona sasa anazidisha mno.

Shughuli inaonekana ni ya kiraia. Magwanda ya nini?

 
Magufuli ni bonge la mshamba, bonge la limbukeni, bado analimbuka mpaka kesho.

Ni kama mtoto umemnunulia nguo ya kuvaa sikukuu, yeye anataka aivae kila siku watu wamuone ana nguo mpya.

Nyerere nimemuona kavaa nguo za kijeshi kwenye harakati za Vita Vya Kagera tu.

Mwinyi sijamuona, Mkapa sijamuona. Kikwete ambaye alikuwa mwanajeshi na anaelewa "Civilian Leadership of The Military", kwa sababu ilimpa uchaguzi wa kuchagua jeshi ama siasa, sikumbuki kumuona kavaa magwanda ya kijeshi kama rais. Anajua walivyoondoka jeshini yeye, kina Makamba, Chiligati, marehemu Ditopile, na wengine wengi, ili wabaki kwenye siasa.

Magufuli limbukeni hajui au hajali hayo.
 
Komredi, kwahiyo ni bora aendelee kuvaa hayahaya ya JWTZ hata kama anaenda kupokea ndege mpya?

Oh sorry naona kama na mimi nimeshamnanga tayari.

Komredi, long time no see! Uko poa?

Hapana. Asiendelee kuvaa hayo ya JW. Maana sasa kazidi. Kwa mfano, hiyo jana aliyavaa kwa kusudi gani? Manake hapo kwa video inaonekana shughuli ilikuwa ni ya kiraia.

Kwenye shughuli labda zilizo za kijeshi na ambazo labda zinafanyika porini porini huko kwenye makambi ya kijeshi, kama Ngerengere, akivaa magwanda naweza kuelewa. Dressing for the occasion.

Sasa pata picha siku akivaa magwanda ya Magereza au Polisi.

Like...seriously? Si atakuwa amewapa watu fimbo ya kumsulubia?

Ila dizaini za Magufuli wala huwa hazijali. Zikiona kuna kitu baadhi ya watu hawakipendi basi ndo zinazidisha sasa ili watu wazidi kukereka.

Si unaona kwa Makonda..

Hapo si ajabu Magu anamwacha tu jamaa ili kukera watu.

Na hayo magwanda si ajabu kayavaa kwa makusudi tu ili kuwakera wanaokereka.

Kama ushamsoma vizuri, Magu ana makusudi sana. Na usikute yupo humu anatusoma vizuri sana.

Ila walau apunguze kuvaa vaa hayo magwanda.

Haipendezi Rais wa kiraia kuyavaa vaa tu hata pasipohusika.
 
Aisee... sasa ni kwamba wanaoyajua haya na wako karibu na mtu huyu unadhani huwa hawamshauri au hashauriki?
Magufuli hashauriwi na washauri wake, yeye ndiye anawashauri.

Walianza kumshauri wachache, watu wakaona huyu Magufuli ukimshauri tofauti na anavyotaka yeye, anakutoa kazini, anamuweka mwingine.

Kama alivyofanyiwa CAG Assad. Kama alivyofanyiwa Lawrence Mafuru. Kama walivyofanyiwa wataalamu wengi tu.

Sasa washauri ambao wanataka kazi zao wameamua kumuacha tu.
 
Eti hili nalo ni hoja ya kisiasa kwa wafuasi was chadema ambao hawajui hata naana ya vazi la jeshi la ulinzi na usalama (_jw tz),

Mkuu tambua rais anapovaa sare za jw ambayo ina rangi za ugoro =jenzi la magereza ,kaki = jeshi la polisi ,kuna kijani ,ambapo kuna jkt nk.akivaa hivyo basi tambua amevaa sare za majeshi yote ,yaani yeye ni amiri jeshi mkuu wa majeshi yote yaliyo inchini ,so akivaa eidha ugoro tu ambayo ni sare ya magereza itakuwa hajafuata protocalli

Source please
 
Back
Top Bottom