Ni lini Amiri Jeshi Mkuu atavaa sare za Askari Polisi au Magereza?

Ni lini Amiri Jeshi Mkuu atavaa sare za Askari Polisi au Magereza?

Kama ni suala la kikatiba tufafanulie mkuu , kuuliza ni kutaka kujua tu .
Mkifuatwa mkashughulikiwa ndugu zako watakuja hapa kuanzisha thread.
Mkishiba huku mko huru mnahara utumbo tu kwenye media.
Kuvaa jezi yoyote kwa rais kuna impact gani katika maendeleo.
Au hata siasa,maybe anapenda tu mavazi hayo.mbona mi ninayo kuanzia kapelo mpaka kiatu sijawahi hata kuwaza kumzulu mtu.
Hayo ni mavazi tu
 
Magufuli hashauriwi na washauri wake, yeye ndiye anawashauri.

Walianza kumshauri wachache, watu wakaona huyu Magufuli ukimshauri tofauti na anavyotaka yeye, anakutoa kazini, anamuweka mwingine.

Kama alivyofanyiwa CAG Assad. Kama alivyofanyiwa Lawrence Mafuru. Kama walivyofanyiwa wataalamu wengi tu.

Sasa washauri ambao wanataka kazi zao wameamua kumuacha tu.
Dah... nimekumbuka story ya Bwana Museveni wa Uganda... Huyu bwana inasemekanna alikuwa na washauri 27 lakini yeye ndio alikuwa akiwashauri washauri wake!
 
View attachment 1267903

iko wazi kwamba yeye ndiye kiongozi wa Juu kabisa wa Majeshi yote nchini .

Swali langu ni dogo tu , ni lini mheshimiwa atavaa sare za polisi ili kuonyesha kuunga mkono juhudi zao za kupambana na uhalifu au ni lazima avae za JWTZ tu kama ambavyo ameonekana mara kadhaa ?

Naomba kuwasilisha
Mada hii ni kiashiria cha mwanzo wa mwisho wa hoja constructive..tafuteni kazi nyingine
 
Nyani Ngabu,
Niko komredi...

Nilikuwa kwenye mchakato wa kumwingiza Kasie kwenye 18. Haikuwa kazi rahisi. Nililazimika kuingia msituni na magwanda ya JKT....

Tukirudi kwa Bwana huyu, pamoja na katabia kake ka kupenda kukera watu, pia ana katabia ka ubabeubabe..

Sio ajabu kuvaa magwanda isiwe kwa nia ya kukera watu bali kuwapa taarifa wapinzani wake kuwa yeye ndiye Amiri Jeshi Mkuu... anaweza kuwafanya chochote akiamua.
 
Mh Rais pole kwa majukumu yakitaifa na hongera kwa kazi yakuijenga Tanzania.

Mimi nakuomba jambo moja kama Rais wetu sisi watanzania nakuomba usivae magwanda ya jeshi. Tafasiri yakuvaa hizo nguo inatutisha sote. Hali ya sasa ya siasa nchini na matukio yanaendelea kiukweli joto la hofu linazidi kupanda.

Kweli wewe ndio mkuu wa majeshi yote mpaka wanyama wanajuwa kuna mwanaume amekalia kiti, ila Mh Rais ukipiga kombati watu tunasali tunajuwa kuna kazi inaendelea.

Mkuu hali ya siasa sio nzuri niwakati ambao unapaswa hata kuongea utafakari mara mbili maana neno moja taifa hili linalipuka.

Mwl Nyerere akasema ni hatari kuwaongoza watu wenye njaa hata kusimama simama nihatari sana ktk kipindi hiki.
Hayo ni maoni yangu
 
Dah... nimekumbuka story ya Bwana Museveni wa Uganda... Huyu bwana inasemekanna alikuwa na washauri 27 lakini yeye ndio alikuwa akiwashauri washauri wake!
Museveni alikuwa anakodi teksi inamrudisha mpaka nyumbani kwake Upanga, halafu akifika anamsomesha dereva teksi hamlipi.

Mpaka alivyoondoka Tanzania katika apartment aliyopewa na Ikulu kaacha bill kubwa sana ya maji na umeme.

Yani yeye ni mtu wa kujiweka juu tu, huwezi kumwambia kitu.

Ndiko tulipo sasa hivi kwa Mkulu wetu.
 
Museveni alikuwa anakodi teksi inamrudisha mpaka nyumbaninkwake Upanga, halafu akifika anamsomesha dereva teksi hamlipi.

Mpaka alivyoondoka Tanzania katika apartment aliyopewa na Ikulu kaacha bill kubwa sana ya maji na umeme.

Yani yeye ni mtu wa kujiweka juu tu, huwezi kumwambia kitu.

Ndiko tulipo sasa hivi kwa Mkulu wetu.
Aisee... basi tumeula wa chuya.
 
View attachment 1267903

iko wazi kwamba yeye ndiye kiongozi wa Juu kabisa wa Majeshi yote nchini .

Swali langu ni dogo tu , ni lini mheshimiwa atavaa sare za polisi ili kuonyesha kuunga mkono juhudi zao za kupambana na uhalifu au ni lazima avae za JWTZ tu kama ambavyo ameonekana mara kadhaa ?

Naomba kuwasilisha
Mkuu hii hoja itumieni ipasavyo kama mtaji wa kura kwa wananchi 2020.
 
Nyani Ngabu,
Labda alitoka ktk shughuli ya kijeshi, akaunga hapo hapo.
Pia anapovaa wananchi tunaweza sema anazidisha ila wajeda wanafurahi, wanaona yuko karibu nao.
 
Kumbuka Rais ni Amiri jeshi..kosa likowapi akivaa nguo za jeshi? Au kila anachokifanya Magu ni kibaya? Tuelimike kidogo
Unafahamu "Civilian Control of The Military" ni kitu gani?

Unaelewa kwa nini kina Kikwete, Makamba, Chiligati, Dotopile, Andree Shija, Moses Nnauye waliambiwa wachague moja kati ya jeshi na siasa?

Unaelewa kwa nini Mwalimu Nyerere, rais pekee ambaye ni "Rais wa Vita" Tanzania, hakuvaa magwanda ya jeshi nje ya kuhamasisha vita vya Kagera?

Unaelewa kwa nini Jakaya Mrisho Kikwete, rais oekee ambaye amewahi kuwa mwanajeshi na kamisaa wa siasa jeshini, hakushobokea kuvaa magwanda ya kijeshi akiwa rais?

Unaelewa kwa nini Benjamin William Mkapa, muandiamshi wa habari msomi, mwanadiplomasia wa siku nyingi, na mtu aliyeshika uongozi tangu miaka ya sitini, hajashobokea kuvaa magwanda ya jeshi alivyokuwa rais?

Unaelewa kwa nini Ali Hassan Mwinyi, na hekima zake za Unguja ya zamani, mzee wa Kiswahili, mwanadiplomasia mwenye kujua uwezo wake ulipoishia na kutumia wengine kuongoza, hakushobokea magwanda ya jeshi?

Unaelewa kwamba muonekano wa rais kuvaa vaa magwanda ya kijeshi bika sababu ya kueleweka unaondoa muonekano wa nchi kuendeshwa kidemokrasia na raia?

Umeusoma "Waraka wa Jeshi" na jinsi wanajeshi wanavyokasirika jeshi linavyoingizwa katika siasa?
 
Nyani Ngabu,
Binafsi sioni shida. Ukiangalia anapoyavaa na jinsi anavyo interact na raia kwenye shughuli za kiraia anakuwa kama analisogeza jeshi kwa wananchi na kuwapa wananchi confidence kuwa wanajeshi si wa kuogopwa bali wa kuungwa mkono.
Sema zile kauli zake za "watakiona cha moto, tia ndani, ole wao" huku akiwa ndani ya combat huishia kuharibu dhamira nzuri yote.
 
Nadhani mada yako ungeiwasilisha kama ombi,

"Naomba amiri jeshi kuu siku moja avae sare za jeshi la polisi/magereza/traffic/zimamoto/ffu/mgambo, nione jinsi zinavyomkaa vema...."

Lmao[emoji23][emoji23]

Kuwa huru huyu ni Rais wetu,Watanzania wote, wasilisha hoja kama ombi....itapendeza
 
Kiranga,
Point yako nimeielewa vizuri sana Kiranga ingawa vice versa can be tru kama nilivyomjibu Nyani Ngabu hapo juu.

Hoja zako zimenifanya nifikirie kwa angle nyingine kwamba huenda wananchi wanaandaliwa kisaikolojia kuingizwa kwenye aina hiyo ya utawala kwa muda mrefu ujao, hivyo kuchagua wanajeshi kuwa wakuu wa wilaya na mikoa na vitengo mbalimbali vya serikali wakitumikia nafasi zao hizo huku wakiwa ndani ya Combat ni mpango ambao mahsusi wa kuielekeza nchi huko.

Hivyo kitendo cha Rais naye kuvaa mavazi yake hayo mara kwa mara si mapenzi yake kwa jeshi tu bali ni mkakati maalum na anaelekezwa kufanya hivyo.

Ukiangalia aina ya miradi inayoendelea huvi sasa nchini na hatia zinazo chukuliwa, wenzetu China na nchi nyinginezo (most ni non westeners) waliweza kufanikiwa kwa mtu au kikundi cha itikadi fulani kujiweka madarakani kwa myda mrefu kitu ambacho kwa namna fulani kiliua democrasia nchini mwao.
Kagame is the Living example in this Africa Block.

Cc Malcom Lumumba Chige
 
Back
Top Bottom