SMU
JF-Expert Member
- Feb 14, 2008
- 9,613
- 7,889
Absolutely!DAWA moja kigongo sana kwa lecturers wasumbufu ni kuhakikisha unafanya yafuatayo:
1. Hakikisha unasoma kozi unayoipenda na KUIMUDU.
2. Hudhuria vipindi vyote darasani.
3. Fanya test na assignment zote.
4. Hakikisha unascore 70%+ kwenye test, assignments na paper zote (Jisomee na kuelewa unachosoma)
5. Tusikuone Facebook (the greatest time waster for useless people)
6. Kila dakika jikumbushe mstari huu: "hapa chuo/shule nimefuata masomo"
ukilenga kufanya hayo HAKUNA lecturer au mtu yeyote atakayekutisha hapa ulimwenguni, achilia mbali duniani.
Matatizo ya kitaaluma mara nyingi mwanafunzi mwenyewe anakuwa amechangia pa kubwa tu na ni machache sana ambayo genuinely yanaletwa/kuanzishwa na wahadhiri. Katika kipindi nilichosoma mimi wanafunzi waliokuwa wana-disco au ku-sup walikuwa obvious kwa kutizama tu mienendo yao katika kujishughulisha na shule (ni wachache sana ambao mtu unaweza hasa kushangaa ukisikia ame-disco au ku-sup).