Ni lini serikali itaingilia kati huu wizi wa mitandao ya simu kuunganisha watu kwenye huduma wasizohitaji?

Ni lini serikali itaingilia kati huu wizi wa mitandao ya simu kuunganisha watu kwenye huduma wasizohitaji?

clinician

JF-Expert Member
Joined
Mar 5, 2014
Posts
2,098
Reaction score
4,926
Ni Jambo linakwaza sana. Unanunua vocha kujiunga na kifurushi unachopenda mara unapata ujumbe kuwa Salio lako halitoshi.

Unafuatilia unaambiwa umejiunga na huduma za kidijitali kama vile "afya call" ,"Tikisa ushinde" n.k.

Huna taarifa na huduma hizo,hujui umejiungaje na wala hujui zinahusu nini,ila pesa zako zinakwenda na kiendacho kwa mganga hakirudi.
Je serikali imebariki huu uhuni wa miaka nenda rudi unaofanywa na Vodacom na mitandao mingine ya simu?

Mbaya zaidi nimejaribu kujiondoa na hizo huduma nimeambiwa "Ombi lako la kujiondoa kwenye Tikisa Ushinde halikufanikiwa Piga *149*83# kujaribu tena."

Huu ni wizi kama wizi mwingine,nadhani ni wakati sasa suala hili likashughulikiwa ipasavyo.
 
Ni Jambo linakwaza sana. Unanunua vocha kujiunga na kifurushi unachopenda mara unapata ujumbe kuwa Salio lako halitoshi.
Unafuatilia unaambiwa umejiunga na huduma za kidijitali kama vile "afya call" ,"Tikisa usinde" n.k.
Huna taarifa na huduma hizo,hujui umejiungaje na wala hujui zinahusu nini,ila pesa zako zinakwenda na kiendacho kwa mganga hakirudi.
Je serikali imebariki huu uhuni wa miaka nenda rudi unaofanywa na Vodacom na mitandao mingine ya simu?
Mbaya zaidi nimejaribu kujiondoa na hizo huduma nimeambiwa "Ombi lako la kujiondoa kwenye Tikisa Ushinde halikufanikiwa Piga *149*83# kujaribu tena."
Huu ni wizi kama wizi mwingine,nadhani ni wakati sasa suala hili likashughulikiwa ipasavyo.
Haya ni mambo yanayohitaji action ya wananchi. Kulalamika tu bila action ni bure. Watu wameanza kulalamika ni miaka zaidi ya 20 sasa lakini kila kukicha mambo ndiyo yanazidi kuwa mabaya. Kukiwasha ni muhimu. Msikubali kuwekewa viongozi wa mchongo wasiojali shida za wananchi.
 
Muda si mrefu nilikua nafikiri kuhusu hili swala jamaa mtandaoni wamejaa wao kama vile hakuna BOT wala TCRA wa kufatilia hizi mambo Wananchi wanaibiwa sana kupitia wizi wa mitandao ndio maana watu wa Afrika Magharibi wanajaa sana hapa wakijua tupo chini sana kwenye swala la ufatiliaji huku wao wakiendelea kuiba tu...
 
mkuu huelewi nini? mimi sio mjinga kufanya jambo nisilolijua. Wakati mwingine huwa wanatumia ujanja sana kukufanya ujiunge na hizo huduma,unakumbuka mchezo wa bahati nasibu wa Vodacom uliokuwa unaitwa BURE? wanakwambia cheza bure,lakini ukicheza unakatwa hela. BURE sio gharama za huduma,BURE ni jina la mchezo. Endelea kucheza bure ujishindie mamilioni.
Ujue ulijiunga , mbona Mimi sijawahi kuunganishwa , mana nikipigiwa simu ya matandao au Fanya ivi kujiunga na huduma flani napotezea ,
 
Ni Jambo linakwaza sana. Unanunua vocha kujiunga na kifurushi unachopenda mara unapata ujumbe kuwa Salio lako halitoshi.
Unafuatilia unaambiwa umejiunga na huduma za kidijitali kama vile "afya call" ,"Tikisa ushinde" n.k.
Huna taarifa na huduma hizo,hujui umejiungaje na wala hujui zinahusu nini,ila pesa zako zinakwenda na kiendacho kwa mganga hakirudi.
Je serikali imebariki huu uhuni wa miaka nenda rudi unaofanywa na Vodacom na mitandao mingine ya simu?
Mbaya zaidi nimejaribu kujiondoa na hizo huduma nimeambiwa "Ombi lako la kujiondoa kwenye Tikisa Ushinde halikufanikiwa Piga *149*83# kujaribu tena."
Huu ni wizi kama wizi mwingine,nadhani ni wakati sasa suala hili likashughulikiwa ipasavyo.


Huo ni wizi wa wazi, na Waziri Nape aliambiwa mara nyingi na hafanyi lolote, mitandao ya simu imekuwa ikiibia wateja wao wazi wazi kwa uhuni huo.. Huo ni uhuni na wizi wa wazi kabisa
 
Huo ni wizi wa wazi, na Waziri Nape aliambiwa mara nyingi na hafanyi lolote, mitandao ya simu imekuwa ikiibia wateja wao wazi wazi kwa uhuni huo.. Huo ni uhuni na wizi wa wazi kabisa
wakati mwingine hawa tunaopeleka malalamiko wapo kwa ajili ya maslahi ya walalamikiwa.
 
Kuna watu wanakopa mtandaoni huko halafu wanaweka namba yako kama mdhamini... Siku anashindwa kulipa deni sasa wana anza usumbufu kisa namba ipo kama mdhamini..

TCRA na BOT iwadhibiti hawa watu... Nipate taarifa kwanza kuna mtu anataka niwe mdhamini... Nikubali mwenyewe ndio wakopeshane huko... Wanakopeshana wenyewe halafu usumbufu wanaleta kwangu... Hii haikubaliki kabisa... Wataoga lugha za maudhi tu.

Samahani mleta mada, nimetoka nje ya maudhui ya uzi wako.
 
Ni Jambo linakwaza sana. Unanunua vocha kujiunga na kifurushi unachopenda mara unapata ujumbe kuwa Salio lako halitoshi.
Unafuatilia unaambiwa umejiunga na huduma za kidijitali kama vile "afya call" ,"Tikisa ushinde" n.k.
Huna taarifa na huduma hizo,hujui umejiungaje na wala hujui zinahusu nini,ila pesa zako zinakwenda na kiendacho kwa mganga hakirudi.
Je serikali imebariki huu uhuni wa miaka nenda rudi unaofanywa na Vodacom na mitandao mingine ya simu?
Mbaya zaidi nimejaribu kujiondoa na hizo huduma nimeambiwa "Ombi lako la kujiondoa kwenye Tikisa Ushinde halikufanikiwa Piga *149*83# kujaribu tena."
Huu ni wizi kama wizi mwingine,nadhani ni wakati sasa suala hili likashughulikiwa ipasavyo.
Kwakweli Vodacom hii tabia imekithili na ukiwapigia hauwezi kuwapata wanakuondoa kwenye huduma ya kuwasiliana nao Moja Kwa Moja na wanakuwekeweke huduma ya ya kuwasiliana kupitia mitandao ya kijamii Kwa kukutumia link zao za Instagram , Facebook, Tweeter(X).
Hivi kweli unachangamoto Yako ya haraka uende Facebook,Tweeter(X), Instagram? kwakweli wanatukwaza sana.
 
Kwakweli Vodacom hii tabia imekithili na ukiwapigia hauwezi kuwapata wanakuondoa kwenye huduma ya kuwasiliana nao Moja Kwa Moja na wanakuwekeweke huduma ya ya kuwasiliana kupitia mitandao ya kijamii Kwa kukutumia link zao za Instagram , Facebook, Tweeter(X).
Hivi kweli unachangamoto Yako ya haraka uende Facebook,Tweeter(X), Instagram? kwakweli wanatukwaza sana.
Voda ndio ilitakiwa wawe wa kwanza kushitakiwa kwa kuondoa huduma kwa wateja, nadhani sheria ya huduma inatakiwa ifanyiwe review haiwezekani watu waamue tu kuondoa hotline yao na kukimbilia kuweka robot. Nilijaribu kuwasiliana nao kupitia whatsapp nikagundua nachat na robot na sio mtu kwa namna alivyokuwa ana respond. Sikupata ufumbuzi kabisa.
 
Ujue ulijiunga , mbona Mimi sijawahi kuunganishwa , mana nikipigiwa simu ya matandao au Fanya ivi kujiunga na huduma flani napotezea ,
Si kweli.
Zaidi ya mara tano nimeungwa bila hiari yangu. Kila nikitaka kujitoa haiwewezekani. Ukiwasiliana nao kupitia 100 au mhudumu ni bla bla tu.
Ninapowaandikia.barua pepe kuwa nitawapeleka TCRA ndipo wananipigia wakiwa wapole na lugha laini wakiomba radhi. Hapo ndipo wananitoa.
Hii na ile ya "Tuma kwenye namba hii" ni kero kubwa.
Kwa nini mamlaka zinaacha tuumizwe hivi?
Jambo hili halitokei bahati mbaya. Ni mpango/mkakati wa watoa huduma.
 
Huu ni ujing mkubwa sana. Junamuda unakuwa unatumia simu yako mara from no where kanakuja kaujumbe ambako kama hauko makini ukinonyesha okay ushajiunga na maujinga yao. Huu upuuzi uko sana vodacom . Sijui waziri na serikali wamekubalije huu utapeli
 
Ujue ulijiunga , mbona Mimi sijawahi kuunganishwa , mana nikipigiwa simu ya matandao au Fanya ivi kujiunga na huduma flani napotezea ,
Eng jamaa katoa angalizo kuwa hao jamaa wapo mimi na wewe kutojiunga haimaanishi wote hawatajiunga tutoe Umimi kwenye jambo hili kama zipo taasisi zinazoweza kufatilia huu wizi wao wafatilie ninachoshangaa mtu anatoa taarifa ya wezi wewe kama haujadhurika una sababu gani ya kupinga ...
 
Wizara husika iko mfukoni mwa haya mashirika. La sivyo mwananchi a singe kuwa anasumbuliwa hivi
 
Ni Jambo linakwaza sana. Unanunua vocha kujiunga na kifurushi unachopenda mara unapata ujumbe kuwa Salio lako halitoshi.
Unafuatilia unaambiwa umejiunga na huduma za kidijitali kama vile "afya call" ,"Tikisa ushinde" n.k.
Huna taarifa na huduma hizo,hujui umejiungaje na wala hujui zinahusu nini,ila pesa zako zinakwenda na kiendacho kwa mganga hakirudi.
Je serikali imebariki huu uhuni wa miaka nenda rudi unaofanywa na Vodacom na mitandao mingine ya simu?
Mbaya zaidi nimejaribu kujiondoa na hizo huduma nimeambiwa "Ombi lako la kujiondoa kwenye Tikisa Ushinde halikufanikiwa Piga *149*83# kujaribu tena."
Huu ni wizi kama wizi mwingine,nadhani ni wakati sasa suala hili likashughulikiwa ipasavyo.
Mara chekecha mkwanja@Vodacom
 
Tanzania haina Wachdog wala Chombo kinachomlinda Mlaji.

Nchi inajiendea tu kwa kudra.
 
Back
Top Bottom