Ni mambo gani uliwahi kuona kanisani kwako ya kakuacha mdomo wazi? Mimi kuzikwa mifupa ya mwanzilishi wa kanisa hilo mimbarini

Religion and witchcraft depends on who is doing it.

Kinacho fanyika makanisani hakina tofauti na wanachofanya waganga na wachawi.

Wakatoliki watakushangaa kusali makaburini kwa mababu zako, Lakini hawajishangai wao kusali kwenye zege lililosimamishwa kama sanamu ya bikira Maria na Yesu.
 
Point yako ni ipi mkuu?
 
...Hilo Kabisa halina Jina ? Kama ilitokea kweli Kwa Nini unaficha jina la Kanisa ?? Ilikuwa Siri ??...
 
Umezunguka sana lakini hapo unamaanisha RC.
Kwanza hakuna kitu kinachoitwa kusimika au kuzindua kanisa.Na masalia yanayowekwa sio ya muanzilishi wa kanisa maana muasisi wa kanisa ni Yesu mwenyewe alipomuambia Petro ya kwamba atalijenga kanisa lake juu yake.

Tukio unalosema ni kutabaruku kanisa.Maana yake ni kuliweka wakfu jengo hilo na kulitenga mbali na shughuli nyingine za kidunia/kijamii ili litumike tu kwa ajili ya sadaka ya ibada takatifu ya misa.

Ubani unawekwa katika chungu na kufukizwa juu ya altare (meza ile ya kutolea dhabihu)ishara ishara ya kupatakatifuza na kumsihi Mungu ya kwamba sadaka zitakazotolewa hapo zipae kwake juu na harufu nzuri ya kumpendeza kama moshi huo wa ubani.Kadhalika husuguliwa kwa mafuta matakatifu ishara ya kupatakasa.

Unayosema mifupa ililetwa sina hakika kama uliiona mifupa kwasababu huwa sio mifupa haswa bali chembe ndogo sana ya masalia ya huyo mtakatifu aliyewekwa kuwa msimamizi wa kanisa mahalia.Kwa imani yetu sisi wakatoliki watakatifu wanao uwezo wa kutuombea kwa Mungu ndio maana tuna litania ya watakatifu.Hivyo kuweka alama yake katika kanisa husika ni ishara ya kukabidhi usimamizi wa kanisa husika kwake.

NB kwa maelezo ya mleta mada ninathubutu kusema sio mkatoliki maana naona hajui kila kitu.
 
Ndio maana nikasema katupiga kamba akitaka aseme yote aliyoyaona na kushuhudia
 

"sina hakika kama uliiona mifupa kwasababu huwa sio mifupa haswa bali chembe ndogo sana ya masalia ya huyo mtakatifu"

Hayo masalia ni nini?
 
hio mifupa inatoka wapi ? Kwa mfano parokia ya Mt yuda tade, hio mifupa inakuwa ya huyo yuda ? Wanaitoa wapi ? Je dunia nzima makanisa yote ya yuda wana mifupa yake ?? Ufafanuzi kdg mkuu ,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…