Ni mapungufu gani ya mkeo/mumeo umeamua kuishi nayo?

Ni mapungufu gani ya mkeo/mumeo umeamua kuishi nayo?

Wangu jamani uwii! Ukikosea analisema jambo kama lilivyo bila hata chembe ya kupepesa macho.

Which is good, but kuna mambo huwa anakosea nashindwa kumface kumchana nampotezea tu nikiamini anajua anachofanya, ila ikija upande wangu nachanwa chanwa bila kuremba kitu. Sasa naona why mimi nambebea madhaifu yake yeye hanibebei? Is it fair?

Ukisafiri ukiwa unarudi lazima alazimishe kuja kukupokea, yaani hii ni lazima sio ombi, tatizo ni kwamba hata umwambie nusu saa kabla hujafika, au lisaa kabisa lazima achelewe, yaani lazima achelewe. Kwahiyo mimi kukaa airport/Au stendi dakika 10/15/20 ni kitu cha kawaida tu. Nilishamshauri hili suala la kunipokea aliache, ntapanda tax, bajaji etc ila hakubali ng'oo ni bora umuue! Nishanuna sana, nishazira sana ila haisaidii. Mwaka wa 9 huu.

Anyways.... Naishi humo!
Sasa kupokelewa kuna ubaya gani jaman?
 
Sheria mkononi 😆🤣 na visu vilivyo zagaa hivi
Hapo!? Nichaji betri kwanza. Eti eh?!
raraa reree kwa ubora wake
Sasa unaemuuliza huenda nae hivo hivo. Mpe akapime nae basi😁😁😁😁🙄🙄🙄
 

Attachments

  • tapatalk_1500946037744.jpeg
    tapatalk_1500946037744.jpeg
    41.2 KB · Views: 9
Ni mbaya sana, nilikuwa hivyo kutokusoma sms na kupokea simu yaani naweza masaa nisiguse simu,


Sasa kuna siku dogo alikuwa anaumwa na homa imemuanzia shule,mama yupo mbali kapewa taarifa ananipigia sipokei na dogo hali si shwari kapelekwa hospital,

Mama alimpigia mtu wa mbali na nyumbani na kumuambia aje aniambie nipokee simu[emoji23], kutizama simu imepigwa hatari


,kumtafuta akaniambia ipo siku utafuatwa na kuulizwa marehemu mama yako utazika hapahapa au utasafirisha[emoji15], aisee toka siku hiyo nipo makini,

na bora anipigie sipatikani lkn sio kutokupokelewa anakerwa.
Hio tabia wanawake wengi wanayo na sio tabia ya kujivunia. Ni aina flani tu ya mapuuza ambayo wengi mnayaendekeza. Simu unapigia ni urgent issue hupokei. Maana yake ni nini sasa.
 
Wakuuu habari za usiku.

Moja kwa Moja twende kwenye maada. Mimi kwa upande wangu mapungu yafuatayo kutoka kwa mama watoto wangu nimekubali KUISHI NAYO.

1. Kuto pokea simu.
Mke wa Mimi hapokei simu hata aione inaita hatashughulika NAYO Hadi amalize shughuli zake. Ukimpigia simu asipo pokea usijisumbue kutuma sms, ukituma Kuna siku utaisoma mwenyewe.

2. Dawa ya mswaki.
Kwenye matumizi ya hii KITU yeye huminya popote pale.

3. Hajichanganya na WATU.
Yeye ni kazini, nyumbani na kanisani. Haendi tofauti na maeneo hayo labda kwenye mambo ya jamii.

4. Ukimkosea hakuulizi na haoneshi kama amechukia ila utaulizwa siku nyingine na atawasilisha kwa njia ya utani.

5. Akikukosea ukiuliza atakuambia nisamehe baba......... hapo hata uongee vipi hatakujibu.

Hapendi kabisaa kijichanganya na WATU hasa ukitaka umuudhi fika nyumbani anza kumwongelea mtu hapendi kabisaa na anachukia kwa dhati.

Haya ndio baadhi ya mambo ambayo nimeamua KUISHI NAYO na nimefamikiwa KUISHI NAYO kwa muda wa miaka 19 ya ndoa yetu.
Kusema kweli sijaona mapungufu mengi kwenye malalamiko yako. Zaidi nimeona mengi ya kumpa hongera.
 
Kosa kubwa hilo. Ushauli (wa keshenzi )lakini unasaidia. We jenga ukalibu na housegirl utaona. Chelewa kulala kaa sebuleni nae mwambie(wife)kwamba sisi ndo kwanza tuaanza kuangalia tamthilia.
Ila muulize kilichomleta hapo ni nini? Na kazaliwa kwa kazi gani?

Mkuu yani wife wangu hama time na mimi yani mara zote yeye sa3 kalala mimi huwa nalala sa8 au9 yani hana hata hofu!!! Kuna siku nimemuangalia dada msaidizi wetu nikaanza kumuona kama ni mzuri hivi[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nikalikataa hili pepo maana nimeshaapa sitakuka nitembee na dada wa kazi
 
Sijui kwa wengine yanakujaga na midawa. Enzi hizo ilikuwa wanatii. Mwanaume na wewe unajistukia unanyenyekea. Sasa hivi,yanaona bora yakupelekeshe sasa. Ndo maana mababu zetu walikuwa wanaamua kuongeza mke. Ukizingua tu,anahamia kwa bi mdogo wewe unabaki na jeuri yako.
Bi mdogo anashukuru kaolewa,hataki kupoteza bahati. Mkubwa nae akiona keshalikologa, anakuwa mpole asiachwe.
Ya leo hii,hamna kitu.
Kuachwa, haina shida.
Mara,we si kitindamimba kwa wanaume.
Mara ohh,mi nimechoka sitaki.


Kama hayupo kwa kukuzalia kwa mkataba,mlete kwa sharti. Kama una nyumba kubwa, kila mtu na chumba chake. Kama chumba mnalala kimoja,kila mmoja na kitanda chake. Mwanaume unajengaje mazoea ya kulala na maanamke?
 
Mpaka sasa ni hasira tu na namna ya kuzidhibiti.

Akikasirika hataki kuongea, ni mpaka hasira zake ziishe sasa mimi hivyo siwezi. Nataka tuongee kwa wakati huohuo nihakikishe yuko sawa ndipo nami nipate amani.

Na akikakisirika zaidi ndio simpati kokote, na hivi yuko mbali nateseka kummiss, naumia sana.

Ila ndio nampenda jamani, akiweza kubadili hili atakuwa ameniokoa sana.
 
Ongea na wife vizuri tu, sometimes mood zinakua down ujue, after sometimes atakua sawa, achana na mchepuko huko unaweza ukaharibu zaidi[emoji848]

Wife sio muongeaje kabisa yani kuna muda namuonaga ana kiburi cha uzima!!! Yani kama leo kaamka asubui subui eti kaalikwa mgeni kwenye graduation, namwambia wewe lala bwana anasema ngoja niende wataona nimewapuuza[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] kwaiyo bora anipuuze mimi!!! Huyu dawa yake nipte demu mkali zaidi yake ndo akili zitakaa sawa
 
Nimekuelewa vizuri tu, unajua sometimes kuna matendo ya upendo mtu unaweza mfanyia mwenzi wako ila kumbe ukawa unaonekana unajipendekeza au mshamba flani. 🤣
No, tatizo lake ni kuwa lazima aniweke stend, ulishawahi kaa stend/airport dakika 20 kumsubiri mtu, unakuwa unazubaa zubaa kama umepotea. halafu sio mara moja ni recurring.

Mfano ndege ya masaa mawili na nusu si unajua kabisa huyu atatua muda fulani kwanini asiwahi nimkute lazima mimi nimsubiri. Na wala hajawahi ona hili kama tatizo. Kwa ujumla tu ana mapuuza kwenye hili.
 
Hio tabia wanawake wengi wanayo na sio tabia ya kujivunia. Ni aina flani tu ya mapuuza ambayo wengi mnayaendekeza. Simu unapigia ni urgent issue hupokei. Maana yake ni nini sasa.
Binafsi nakuwaga sipo bize sana na simu,

Kwasasa nimejifunza, sikai mbali na simu labda iwe haina chaji,


Na mama bora akupigie usipatikane lkn kuliko usipokee.
 
Wife sio muongeaje kabisa yani kuna muda namuonaga ana kiburi cha uzima!!! Yani kama leo kaamka asubui subui eti kaalikwa mgeni kwenye graduation, namwambia wewe lala bwana anasema ngoja niende wataona nimewapuuza[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] kwaiyo bora anipuuze mimi!!! Huyu dawa yake nipte demu mkali zaidi yake ndo akili zitakaa sawa
😂😂😂 Lakini mkuu kwenye hili unamuonea.
 
No, tatizo lake ni kuwa lazima aniweke stend, ulishawahi kaa stend/airport dakika 20 kumsubiri mtu, unakuwa unazubaa zubaa kama umepotea. halafu sio mara moja ni recurring.

Mfano ndege ya masaa mawili na nusu si unajua kabisa huyu atatua muda fulani kwanini asiwahi nimkute lazima mimi nimsubiri. Na wala hajawahi ona hili kama tatizo. Kwa ujumla tu ana mapuuza kwenye hili.
Sasa wewe dawa ni kumdanganya ushafika ilihali ndio uko angani 🤣 ili muende sawa
 
Back
Top Bottom