Ni mbunge Mpina pekee anayetumia ubunge wake ipasavyo, wabunge mliobaki naomba tujikumbushe majukumu ya Bunge la Tanzania

Ni mbunge Mpina pekee anayetumia ubunge wake ipasavyo, wabunge mliobaki naomba tujikumbushe majukumu ya Bunge la Tanzania

Meneja Wa Makampuni

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2020
Posts
7,899
Reaction score
10,415
Bunge la Tanzania ni baraza la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linalotunga sheria na kuisimamia serikali katika utekelezaji wa majukumu yake.

Majukumu ya Bunge yametamkwa katika Ibara ya 63 (2) ya Katiba ya Nchi, kwa maneno yafuatayo:

“Sehemu ya pili ya Bunge itakuwa ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano, ambacho kitakuwa na madaraka, kwa
niaba ya Wananchi, ya kusimamia na kuishauri Serikali ya Muungano pamoja na vyombo vyake vyote katika utekelezaji
wa majukumu yake “

Hivyo basi Bunge ni Chombo cha Uwakilishi wa Wananchi. Kwa madhumuni ya utekelezaji wa madaraka yake Bunge
linaweza:-

1. Kumuuliza Waziri yeyote swali lolote kuhusu mambo ya Umma.

2. Kujadili utekelezaji wa kila Wizara wakati wa Mkutano wa Bunge wa kila mwaka wa Bajeti.

3. Kujadili na kuridhia Mpango wowote wa muda mrefu au muda mfupi unaokusudiwa kutekelezwa katika Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania na kutunga Sheria ya kusimamia utekelezaji wa Mpango huo.

4. Kutunga Sheria pale ambapo utekelezaji unahitaji kuwapo Sheria.

5. Kujadili na kuridhia Mikataba yote inayohusu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ambayo kwa masharti yake
inahitaji kulidhiwa

Kazi ya bunge sio kusifia wala kuunga mkono mambo. Mbunge ni mwakilishi wawananchi.

Mbunge Msukuma amekuwa akijitahidi sana kusimama katika majukumu ambayo mbunge anatakiwa kuyafanya. Pia kuna yule mbunge wa Kahama wanajitahidi sana.

Kama mbunge hawezi kuwahoji mawaziri anakua anakiuka katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 63 (2). Wabunge tuamke wananchi hawana huwezo wa kuhoji mpaka watembelewe na viongozi.

Mmechaguliwa kuhoji hoji. Kuuliza sio ujinga. Na ukijibiwa kama umeridhika na majibu tulia. Kama hujaridhika hoji tena. Hiyo ndio kazi yako kikatiba.
 
Hv huyu makamba ni untouchable au..mbona tuhuma alizopewa nzito...halafu kama hana habari hv.
 
Bunge la Tanzania ni baraza la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linalotunga sheria na kuisimamia serikali katika utekelezaji wa majukumu yake.

Majukumu ya Bunge yametamkwa katika Ibara ya 63 (2) ya Katiba ya Nchi, kwa maneno yafuatayo:

“Sehemu ya pili ya Bunge itakuwa ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano, ambacho kitakuwa na madaraka, kwa
niaba ya Wananchi, ya kusimamia na kuishauri Serikali ya Muungano pamoja na vyombo vyake vyote katika utekelezaji
wa majukumu yake “

Hivyo basi Bunge ni Chombo cha Uwakilishi wa Wananchi. Kwa madhumuni ya utekelezaji wa madaraka yake Bunge
linaweza:-

1 Kumuuliza Waziri yeyote swali lolote kuhusu mambo ya Umma.

2 Kujadili utekelezaji wa kila Wizara wakati wa Mkutano wa Bunge wa kila mwaka wa Bajeti.

3 Kujadili na kuridhia Mpango wowote wa muda mrefu au muda mfupi unaokusudiwa kutekelezwa katika Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania na kutunga Sheria ya kusimamia utekelezaji wa Mpango huo.

4 Kutunga Sheria pale ambapo utekelezaji unahitaji kuwapo Sheria.

5 Kujadili na kuridhia Mikataba yote inayohusu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ambayo kwa masharti yake
inahitaji kulidhiwa

Kazi ya bunge sio kusifia wala kuunga mkono mambo. Mbunge ni mwakilishi wawananchi.

Mbunge Msukuma amekua akijitahidi sana kusimama katika majukumu ambayo mbunge anatakiwa kuyafanya. Pia kuna yule mbunge wa Kahama wanajitahidi sana.
Kumsifia Mpina wakati huu unadhihirisha kuwa wewe ni muumini kindakindaki wa sera za JPM. Unatakiwa uwe na moyo wa kijasiri sana kama wa Simba vile.
 
Kichwa cha habari cha bandiko kinamhusu Luhaga Mpina, maelezo ya habari yanamhusu Mbunge Joseph Kasheku na Jumanne Kishimba.

Mwandishi amekusudia Kutujuza nini katika bandiko hili
😃😃😃😃😃😃😃Wao wameelewa vizuri. Sii wamo humu.
 
Kichwa cha habari cha bandiko kinamhusu Luhaga Mpina, maelezo ya habari yanamhusu Mbunge Joseph Kasheku na Jumanne Kishimba.

Mwandishi amekusudia Kutujuza nini katika bandiko hili
Wasukuma katika harakati zao
 
JPM alishatuambia kwamba Mpina ni kichaa, ana matatizo ya akili
 
Back
Top Bottom