Ni mbunge Mpina pekee anayetumia ubunge wake ipasavyo, wabunge mliobaki naomba tujikumbushe majukumu ya Bunge la Tanzania

Ni mbunge Mpina pekee anayetumia ubunge wake ipasavyo, wabunge mliobaki naomba tujikumbushe majukumu ya Bunge la Tanzania

Bunge la Tanzania ni baraza la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linalotunga sheria na kuisimamia serikali katika utekelezaji wa majukumu yake.

Majukumu ya Bunge yametamkwa katika Ibara ya 63 (2) ya Katiba ya Nchi, kwa maneno yafuatayo:

“Sehemu ya pili ya Bunge itakuwa ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano, ambacho kitakuwa na madaraka, kwa
niaba ya Wananchi, ya kusimamia na kuishauri Serikali ya Muungano pamoja na vyombo vyake vyote katika utekelezaji
wa majukumu yake “

Hivyo basi Bunge ni Chombo cha Uwakilishi wa Wananchi. Kwa madhumuni ya utekelezaji wa madaraka yake Bunge
linaweza:-

1. Kumuuliza Waziri yeyote swali lolote kuhusu mambo ya Umma.

2. Kujadili utekelezaji wa kila Wizara wakati wa Mkutano wa Bunge wa kila mwaka wa Bajeti.

3. Kujadili na kuridhia Mpango wowote wa muda mrefu au muda mfupi unaokusudiwa kutekelezwa katika Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania na kutunga Sheria ya kusimamia utekelezaji wa Mpango huo.

4. Kutunga Sheria pale ambapo utekelezaji unahitaji kuwapo Sheria.

5. Kujadili na kuridhia Mikataba yote inayohusu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ambayo kwa masharti yake
inahitaji kulidhiwa

Kazi ya bunge sio kusifia wala kuunga mkono mambo. Mbunge ni mwakilishi wawananchi.

Mbunge Msukuma amekuwa akijitahidi sana kusimama katika majukumu ambayo mbunge anatakiwa kuyafanya. Pia kuna yule mbunge wa Kahama wanajitahidi sana.

Kama mbunge hawezi kuwahoji mawaziri anakua anakiuka katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 63 (2). Wabunge tuamke wananchi hawana huwezo wa kuhoji mpaka watembelewe na viongozi.

Mmechaguliwa kuhoji hoji. Kuuliza sio ujinga. Na ukijibiwa kama umeridhika na majibu tulia. Kama hujaridhika hoji tena. Hiyo ndio kazi yako kikatiba.
Umemaliza mkuu Meneja
 
Mpina Luhaga aongee tu, ila Bunge hili si la wananchi ni la CCM au Bunge linalowawakilisha mapolisi.
 
Kujadili na kuridhia Mikataba yote inayohusu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ambayo kwa masharti yake
inahitaji kulidhiwa
Mikataba inawndikwa kwa kiingereza tena cha kisheria, wabunge wanaokijua hawazidi 50 na wanaweza kununuliwa the rest wagonga meza
 
Bunge la Tanzania ni baraza la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linalotunga sheria na kuisimamia serikali katika utekelezaji wa majukumu yake.

Majukumu ya Bunge yametamkwa katika Ibara ya 63 (2) ya Katiba ya Nchi, kwa maneno yafuatayo:

“Sehemu ya pili ya Bunge itakuwa ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano, ambacho kitakuwa na madaraka, kwa
niaba ya Wananchi, ya kusimamia na kuishauri Serikali ya Muungano pamoja na vyombo vyake vyote katika utekelezaji
wa majukumu yake “

Hivyo basi Bunge ni Chombo cha Uwakilishi wa Wananchi. Kwa madhumuni ya utekelezaji wa madaraka yake Bunge
linaweza:-

1. Kumuuliza Waziri yeyote swali lolote kuhusu mambo ya Umma.

2. Kujadili utekelezaji wa kila Wizara wakati wa Mkutano wa Bunge wa kila mwaka wa Bajeti.

3. Kujadili na kuridhia Mpango wowote wa muda mrefu au muda mfupi unaokusudiwa kutekelezwa katika Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania na kutunga Sheria ya kusimamia utekelezaji wa Mpango huo.

4. Kutunga Sheria pale ambapo utekelezaji unahitaji kuwapo Sheria.

5. Kujadili na kuridhia Mikataba yote inayohusu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ambayo kwa masharti yake
inahitaji kulidhiwa

Kazi ya bunge sio kusifia wala kuunga mkono mambo. Mbunge ni mwakilishi wawananchi.

Mbunge Msukuma amekuwa akijitahidi sana kusimama katika majukumu ambayo mbunge anatakiwa kuyafanya. Pia kuna yule mbunge wa Kahama wanajitahidi sana.

Kama mbunge hawezi kuwahoji mawaziri anakua anakiuka katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 63 (2). Wabunge tuamke wananchi hawana huwezo wa kuhoji mpaka watembelewe na viongozi.

Mmechaguliwa kuhoji hoji. Kuuliza sio ujinga. Na ukijibiwa kama umeridhika na majibu tulia. Kama hujaridhika hoji tena. Hiyo ndio kazi yako kikatiba.
Hakuna Wabunge mle kuna Wajumbe wa HALMASHAURI KUU CHAMA kwenye Jengo la BUNGE
 
KWa Tanzania ya sasa watu wanaofanya mambo sahihi ndio tunawaona hawapo sahihi; nakubaliana na wewe kabisa kwamba ndugu Mpina anafanya kazi sahihi ambayo ndio HASA kazi za mbunge but kwa mazoea yetu ya sasa tunamshangaa kwasababu yupo tofauti na wenzie; sikuelewa hata mantiki ya Msukuma kumdhalilisha Luhaga Mpina kwa jambo lile.
Police au hakimu anae kataa rushwa kwasasa jamii inamshangaa, kwamba huyu vipi? Ndio kinacho tokea kwa Luhaga Mpina. Sitashangaa bwana Mpina akipigwa chini kwenye KURA za maoni mwaka 2025, siwezi kushangaa
 
Nepotism ndo inatusumbua Tanzania,kama baba yake alisema sasa hivi wanalamba asali,Samia ataweza kumwondoa kweli?

Nilishangaa sana Baba yake kuongea kihuni vile. Tunalamba asali, Tunalamba asali, tunalamba asali mpaka 2030.

Mtoto absolutely incompetent yeye ni visingizio na kulamba asali.

They are both are out of touch with interests of common people and reality.
 
Fisiemu haijawahi kumpenda mtetea wanyonge mtu anayesimamia haki. Akiendelea hivi yakiomkuta ndugai yatamkuta ana luhaga mpina.
Mark my words
 
KWa Tanzania ya sasa watu wanaofanya mambo sahihi ndio tunawaona hawapo sahihi; nakubaliana na wewe kabisa kwamba ndugu Mpina anafanya kazi sahihi ambayo ndio HASA kazi za mbunge but kwa mazoea yetu ya sasa tunamshangaa kwasababu yupo tofauti na wenzie; sikuelewa hata mantiki ya Msukuma kumdhalilisha Luhaga Mpina kwa jambo lile.
Police au hakimu anae kataa rushwa kwasasa jamii inamshangaa, kwamba huyu vipi? Ndio kinacho tokea kwa Luhaga Mpina. Sitashangaa bwana Mpina akipigwa chini kwenye KURA za maoni mwaka 2025, siwezi kushangaa

Wanaweza kumpiga chini hata kumtafutia zengwe, kumchafua. Lakini katika jamii ya Watanzania tunahitaji watu wachache kujitolea, kutimiza wajibu wao / kazi zao bila woga au kujali sana maslahi binafsi nini kitawatokea.

Tukiwa na wabunge hata nusu, robo wanaotimiza wajibu wao. Watanzania wengi watapata nafuu ya maisha, changamoto nyingi zitatatuliwa haraka na rasilimali za nchi kutumika kwa manufaa ya taifa.
 
Fisiemu haijawahi kumpenda mtetea wanyonge mtu anayesimamia haki. Akiendelea hivi yakiomkuta ndugai yatamkuta ana luhaga mpina.
Mark my words

Hivi hawa wanaosema ukweli, wanaowapigania Wananchi, maslahi ya umma kwanini wasianzishe group lao, chama chao,
ambacho kitakuwa kinapigania haki, maslahi mapana ya Watanzania.

Wapo wakutosha lakini naona bado hawana ujasiri wa kujitokeza, kuungana na kulipigania taifa wazi wazi. Nina uhakika wakijitokeza kwa idadi ya kutosha wataungwa mkono na Watanzania wengi.

Why do they allowed themselves to be ignored, ostracized, marginalised and sidelined?
 
Hivi hawa wanaosema ukweli, wanaowapigania Wananchi, maslahi ya umma kwanini wasianzishe group lao, chama chao,
ambacho kitakuwa kinapigania haki, maslahi mapana ya Watanzania.

Wapo wakutosha lakini naona bado hawana ujasiri wa kujitokeza, kuungana na kulipigania taifa wazi wazi. Nina uhakika wakijitokeza kwa idadi ya kutosha wataungwa mkono na Watanzania wengi.

Why do they allowed themselves to be ignored, ostracized, marginalised and sidelined?
Infwakiti wabongo midomoni tupo vizuri mnoo ila vitendo sifuri matumbo njaaa. Asikwambie mtu kelele za kina mpina ni kwa sababu wamenyinwa ugali waliokuwa wanautafuna enzi za jiwe. Lait wakipewa tonge na mchuzi wanakaa kimya. Mzee wa shule SLOW SLOW alikuwa anapang'ang'a sana sasa kimyaaaaaaaaa. Dont mess up with the FISIEMU. Jamaa wana system ya kunyamazishe vidomo domo.
 
Infwakiti wabongo midomoni tupo vizuri mnoo ila vitendo sifuri matumbo njaaa. Asikwambie mtu kelele za kina mpina ni kwa sababu wamenyinwa ugali waliokuwa wanautafuna enzi za jiwe. Lait wakipewa tonge na mchuzi wanakaa kimya. Mzee wa shule SLOW SLOW alikuwa anapang'ang'a sana sasa kimyaaaaaaaaa. Dont mess up with the FISIEMU. Jamaa wana system ya kunyamazishe vidomo domo.

Wapo waliosimamia maslahi ya Taifa bila uoga kama Augustino Mrema 1995 upigaji, rushwa, ufisadi kila mtu kula kwa urefu kamba zake, mfumuko wa bei, uhuni ulipokithiri

Japo hakutangazwa mshindi, lakini ilisaidia kidogo serikali iliyokuja kupunguza upigaji, rushwa, kwamba kila kitu ni rukhsa.

Awamu iliyofuata japo kwa kiwango fulani na ilijaribu kuunda taasisi imara kusimamia rasilimali za nchi na maslahi ya Watanzania wengi.

His effort was not in vain, kuna mabadiliko ya msingi yalitokea kutokana na jitihada, juhudi na harakati zake. Tunahitaji wakina Mrema wapya wa kizazi hiki.
 
Back
Top Bottom