Ni mimi peke yangu natamani maiti yangu ichomwe moto nikifa badala ya kuzikwa ardhini?

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760
Unapozaliwa tayari kuna risiti ya kifo huandaliwa, Kifo ni uhakika hakiwezi kukwepeka.

Utaratibu uliozoeleka hapa kwetu mazishi hufanyika kwa staili ya kuumezesha udongo mwili, kaburi litachimbwa mwili utawekwa ndani yake kisha kufukiwa.

Lakini mimi nimekuwa na approach tofauti kabisa, ningependa nikifa ikiwa mwili wangu utapata bahati ya kupewa heshima ya mwisho basi nichomwe moto mpaka majivu.

kuliko kupitia process za kuoza na kuliwa na mafunza (japo hauwi katika hali ya kuhisii chochote) ila yale mawazo ya kuhisi utaoza na kuliwa na funza inakera
 
Kwanza Maiti sio yako ni yetu
 
As you wish
 
Kuna Taifa ambalo maiti zao hukatwa katwa na kupewa ndege aina ya Tai
Vipi hapo hutaki mwili wako uwe chakula cha ndege?
 
Hata mimi ningependa hivyo ila sijajua kiimani ikoje.
 
Ukifa huna thamani Tena
 
Hauko peke yako, ni mawazo mujarabu kabisa kuliko kupitia process za kuoza na kuliwa na mafunza(japo nadhani hauwi katika hali ya ku-feel chochote) but that feeling ya kuihisi utaoza na kuliwa na funza it's so disturbing.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…