Ni mke wa mtu, ni mzuri, ANANITAKA nifanyeje?

Ni mke wa mtu, ni mzuri, ANANITAKA nifanyeje?

Dogo, watakudokta ulimboka. Mke wa mtu si tu sumu bali ni DDTii. Kwanza huoni kashakuwa screpa! je jamaa akikuachia kimoja si itabidi utunze na kusomesha watoto wa mwanamme mwenzio.
 
Wewe na hamu za wake za watu ziache kwa ushauri story hizi zimo humu kibao endelea kuperuzi utapata majibu mengi sana tushatoa
 
Mtoa mada,kulikoni story nzito kama hii ukaishusha usiku wa manane? Au ulikuwa naye pembeni?
Mshawahi kufanya romance bila ku go all the way?
Ningekuwa wewe kusema ukweli ningempa dozi kisha niingie mitini,utaache mdondo bana?

Kama kawaida yako banana man!
 
Dogo kuna mambo yanayowezekana na wewe unaonekana kumpenda mke wamtu,kuwa makini sana,kama unaweza kuiba iba ila kwa kujiachia kwako futi sita yaja.
 
nina umri wa miaka 30 single... tangu nimeachana na girlfriend wangu miaka mitatu iliyopita imekuwa ikiniwia vigumu kuconnect with a woman, so nimekuwa na marafiki wa kawaida, kati ya marafiki hao, ni huyu dada. Ni age mate, mwaka wa nane yuko kwenye ndoa na ana watoto wawili sasa, urafiki ulianza wa kawaida tu, mara nyingi amekuwa akiniomba ushauri kuhusu mambo mbalimbali na mimi bila hiyana nimekuwa nikimpatia ushauri huo.... miezi sita iliyo pita aliuguliwa na mtoto wake, mimi kama rafiki nilitoa msaada mwangu kulingana mazingira yaliyokuwepo kwa huruma tu rafiki yangu anauguliwa... baada ya mtoto kupona balaa ndipo lilipoanzia, kwanza alianza na shukrani za kilio kwa kudai nilichomfanyia hajawahi kufanyiwa na mtu yeyote... halafu akaanza kunipa historia ya maisha yake ya ndoa, kwanza alilazimishwa kuolewa, na huyo mume wake kila siku ni vipigo, na akadai kuwa huyo mume wake mtoto wake wa pili si wake kwa sababu eti alishaenda kwa daktari akamwambia kuwa hana uwezo wa kuzaa tena... na huyo dada anadai hajawahi kutoka nje ya ndoa.. kwa hiyo umekuwa ni ugomvi mtindo mmoja, si kwa mawifi hadi kwa mama mkwe wake....Nilichokifanya ni kumpa tu ushauri wa kukaa na mumewe wayazungumze wayamalize na ikiwezekana wakafanye DNA ili kuondoa utata...kilichonishangaza akaanza kunambia she is deeply in love with me.. na muda mrefu amesubiri labda nitasema kitu sisemi amejaribu kila njia kunionyesha ila mimi nikawa kipofu... nilipomwambia kuwa siko tayari si tu kwa kuwa yeye ni mke wa mtu pekee bali bado kuna ghost linani haunt siko ready kuwa kwenye mahusiano kwa sasa bado aliendelea kung'ang'ania.... ananijua vizuri kila uongo nilioutumia kumkwepa ilikuwa ni kazi bure...
Najisikia vibaya sio kwamba ni mlokole, ila pia si mfuasi wa shetani, ninge hit nikakimbia lakini kila likinijia wazo la kuwa huyu ni mke wa mtu nashindwa, kibaya zaidi anasema yuko tayari ku sacrifice everything hata ikibidi kuivunja hiyo ndoa kwa ajili yangu... hicho ndio kinaniogopesha zaidi, kwanza najifeel guilty kwa kuiweka mashakani ndoa ya mtu pili hata nikikubali ipo siku yatanikumba kama ya huyo jamaa...TAFADHALI NAOMBA USHAURI WENU.... kama utanitumia email nitashukuru zaidi ...... ngomz25@gmail.com..............THANX


Huo ndio msingi wa kuungangania na la pili ni kukata mahusiano na huyo mwanamke kwani Mola amesema; Hawi watatu kati ya mwanamke na mwanamme, zaidi ya shetani. Ubaya zaidi nikuwa shetani anakuwa kiungo mzuri anaewafahamu udhaifu wenu.
 
Tatatizo analiendeleza yeye mwenyewe, kama vipi amlambe, au aoe na amtambulishe mke wake aone kama atajileta tena...

Huu ndio ushauri mzuri kabisaa!! Atafute mke wake mwenyewe, 30years kama noma na iwe noma OA mkuu.
 
Nakushauri mkuu umaanishe unachokisema, ikibidi hata mawasiliano na huyo mwanamke punguza ibakie salamu inatosha. Inavyoonekana mna wakati mwingi wa kukaa peke yenu faragha mpaka anakueleza matatizo yake na kukuomba ushauri. Kka ikimbie dhambi kwa miguu yako miwili wala sio kwa kutambaa.

Kama huamini wanawake waliokengeuka imani hutumiwa na ibilisi soma vitabu vitakatifu utamkuta Hawa(Alidanganywa na nyoka akala tunda), Delila(Alitumiwa na wafilisti kumuua Samson), Mke wa Ayubu(Aliyemshauri mume amkufuru Mungu), Sara wa Ibrahimu (Aliyemshauri mumewe amtwae kijakazi), Potifa mke wa Mfalme(Aliyemtaka Yusuph kwa nguvu).

Je nawewe unataka uingie kwenye historia hii?
 
Je waweza kuweka moto kifuani na nguo zako zisiungue?kata mawasiliano naye ibaki salamu tu .Mwanamume anayezini na mke wa mtu hana akili kabisa huyo hujiangamiza mwenyewe
 
Piga mzigo huo kwa maufundi ya hali ya juu. Hizi bahati haziji mara mbili.
 
NA wewe usiwe DHAIFU achana nae ni suala la maamuzi tu..ukijishauri hapa inaonekana na wewe ni DHAIFU...chukua hatua mamlaka unaayo yatumie...
 
usiruhusu ukaribu na yeye tena kama kweli hutaki kama unatamani utajiju but you are going to pay for that,so be prepared
 
Hii ni sawa na kumbusu mamba shavuni.....usichukue ushauri huu.
Mzee umenifurahisha sana na hii kitu...."Kumbusu mamba shavuni" ......teh, teh,teh. wewe ungemwaacha angie kichwa kichwa ili aoteshwe kitenisi.
 
Mtoa mada,kulikoni story nzito kama hii ukaishusha usiku wa manane? Au ulikuwa naye pembeni?
Mshawahi kufanya romance bila ku go all the way?
Ningekuwa wewe kusema ukweli ningempa dozi kisha niingie mitini,utaache mdondo bana?

Acha kuganganya. labda kama anatafuta support hapa. lakini anajua ukweli.
 
Kila mla cha mwenzie na chake pia huliwa.

Kabla ya kutembea na mke wa mtu unatakiwa ujiulize hivi kama na wewe mke wako ukagundua anatembea nje ndoa unajisikiaje, kama jibu utaona ni poa hata mke wako akichukuliwa na mtu basi na wewe endelea na hiyo program ya kuchukua mke wa watu. Otherwise mke wa mtu ni sumu ndugu yangu kama alivyochangia Rogie
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom