Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
SawaSlowly and kwangwaru are songs. Nimelinganisha
Kama kuwa na uwelewa mkubwa ndio kunawafanya muendeleze ukabila, bora tuendelee na huu uelewa mdogo. Vipi kanisani hujaenda?Acha niachane na nyinyi maana uelewa wenu ni finyu sana. Huku kwetu hatuchezi nyimbo za akina diamond kanisani. Happy sabbath
Kwanini hauendi Leo?Sidhani kama nitaenda
Aaaah! [emoji15][emoji15][emoji15] Haya basi, kuuulaaa ngoma! Kwa raha zako! [emoji1]Labda zile nyimbo za kikikuyu zina beat flan hivi nazipenda!Pia Erick Omondi anajua.
Aaaah! [emoji15][emoji15][emoji15] Haya basi, kuuulaaa ngoma! Kwa raha zako![emoji1]
Mwenzao ndiye amesema kwamba anazipenda. [emoji1] Alafu waulize Saida Karoli alikuwa anatumia lugha gani kuimba. Tuanzie hapo.umezileta ?Subiri matusi. Kama kutaja dini nimeambiwa ni ukabila? Watasema aje kuhusu hii?
Huddah je?Mtu pekee namjua kutoka Kenya ukiacha Uhuru na RAO ni Vera Sidika.
Huyo saida simjui hata. Nimewaambia wakenya wanasapoti gospel sana wakasema nimeleta ukabila humu. Hawa watu huwa siwaelewiMwenzao ndiye amesema kwamba anazipenda. [emoji1] Alafu waulize Saida Karoli alikuwa anatumia lugha gani kuimba. Tuanzie hapo.
Mimi ni SDA church, nilienda janaWewe umeenda?
Ishu sio kuzungumzia dini, ishu ni mbegu ya ubaguzi unayojaribu kuipanda.Mnashangaa nini? Si mnajulikana nyie ndiye kinara wa ushirikina dunia nzima? Ndio maana mnanihukumu kisa nimezungumzia dini
Sikiliza nyanyangu, katika nchi zetu changa kama hizi ambazo watu bado tunajaribu kupambana na ukabila, kitu chochote kile kinachoeleza au kutofautisha watu kutokana na ukabila lake, ni hatari sana kukiendekeza, hata kama lengo ni zuri, lakini madhara yake huwa hayarekebishiki.Na hapo ndipo siwaelewi. Hebu nifafanulie
Mtanzania Saida Karoli alikuwa anaimba nadhani ni kwa kihaya, na nyimbo zake zilisikizwa sana. Nandani kuna nyimbo moja ambayo Diamond ametumia line zake za kihaya. Ile ya chambua kama karanga. Waache unafik.Sasa unataka kusema tupige marufuku nyimbo zinazoimbwa kwa lugha za kikabila? Naelewa Tanzania yote mnazungumza kiswahili na nyimbo zote zinaimbwa kwa hii lugha. Je,hizo kabila za kichagga,kisukuma,na spinach zipo kweli ama ni majina tu?
Aaaah! [emoji15][emoji15][emoji15] Haya basi, kuuulaaa ngoma! Kwa raha zako! [emoji1]
Lie of the day.Nazungumza kuhusu ninachokijua, ni ngumu sana kumkuta Mtanzania anaskliza wimbo wowote nje ya Bongo flava, hili nimeliona sana kwenu na hiyo nchi yenu nimeitembea zaidi ya wengi wenu humu, nimekatiza mkoa kwa mkoa, wilaya kwa wilaya hivyo napafahamu vizuri sana.
Yaan ukute Mtanzania amekaa anaskliza wimbo usio Bongo flava, utatembea sana, ni wachache labda waliobahatika kutoka na kuishi nje ya nchi na kurudi, ila wengine wote mumefungiwa ndani ya zizi moja, athari za ujamaa hizo, inalemaza mtu kiakili kwamba hauwezi kuwaza nje ya ulichoelekezwa.
Leo hii Bongo flava imeanza kubadilika na kuiga mitindo ya Kinijeria na ndio maana unakuta wengine wenu mumeanza kuwakubali hao Wanaijeria.
Huyo jamaa hutafuta tu kasoro kwa kila jambo.Mtanzania Saida Karoli alikuwa anaimba nadhani ni kwa kihaya, na nyimbo zake zilisikizwa sana. Nandani kuna nyimbo moja ambayo Diamond ametumia line zake za kihaya. Ile ya chambua kama karanga. Waache unafik.
Hahaha! [emoji1]Unanikosha sana Mkuu. Nilienda Nairobi kwa mara ya kwanza, nikipofika mahali panaitwa Athi River kwenye njia inayoelekea Mombasa jamaa akaweka hizo nyimbo mpaka tulipofika stand ya magari ya Riverside......!
Tangu siku hiyo nilizipenda hizo nyimbo, jamaa alikuwa anaitwa Mwangi na contacts zake ninazo.
Baadae nikampata GF anatokea Muthaiga....ananipenda sana hadi leo na anajua napenda hizo nyimbo so nikawa nikiweka miadi naye lazima aniandalie hizo nyimbo.
Hahaha! [emoji1]
Safi sana. Nilidhani ni utani jombaa. Mziki ni 'universal' na sio lazima usikie lugha inayotumiwa ili upende mziki wenyewe. Kuna mtindo fulani wa kuvutiwa kwenye nyimbo za kiasili, ndio maana hata Saida Karoli nilimkubali sana enzi zile. Kuna nyimbo flani hivi ya msaani fulani wa Bongo ya zamani kidogo inaitwa lugha gongana pale mwisho mwisho ametumia kilugha kuwaamkua watu wa kwao, freshi sana. Hivyo ni vitu ambavyo huwa tu kwenye nyimbo za lugha za kiasili.