Ni Mshabiki wa Simba SC Mwendawazimu pekee ndiyo atashingilia Ushindi wa Penati ya Kupewa na ya Kuonewa Prisons FC

Ni Mshabiki wa Simba SC Mwendawazimu pekee ndiyo atashingilia Ushindi wa Penati ya Kupewa na ya Kuonewa Prisons FC

Ok, nini kifanyike sasa? Tufanyeni droo basi. Mbona tushazoea?
 
Naipenda sana Simba SC yangu na natamani tushinde ila siyo kwa Kubebwa ( Mbeleko ) kama hii ya Leo.

Wana Simba SC mtakaonichukia kwa hili nichukieni na mkiweza nitukaneni mnavyoweza ila kwa 100% Ushindi wa leo tumebebwa na Mwamuzi.

Tunapokuwa Kila Siku tunawasema Yanga SC na GSM kuwa Wanahonga Waamuzi basi kwa huu Upumbavu na Upuuzi uliotokea leo nasi Simba SC tukubali kuwa METL nao wameamua rasmi sasa Kuingia Kazini.

Nje ya Kushinda kwa Goli la Msanii wa Injili Rose Mhando la Nibebeeee...Nibebeeeee... bado hata leo Simba SC yetu imecheza mpira mbovu na usipeleweka hali inayonifanya niamini kuwa huenda Makocha weru ni tatizo au Wachezaji weru Uwezo wao umefikia Kikomo ili tujipange Kufanya Usajili wa maama Msimu ujao.

TFF, TPLB na Kamati ya Saa 72 nawaombeni hata msichelewe Kukaa Kikao cha Kumfungia huyu Mwamuzi ambaye ana jina la Ubini la Simba hivyo yawezekana alitaka Kulifurahisha hilo Jina kwa Kuibeba wazi wazi Simba SC kwa kuipa Penati leo.

Mwanasimba yoyote ambaye atabisha au atanibishia kuwa leo Simba SC tumebebwa kwa kupewa ile Penati iliyotupa Ushindi ajiite ni Mwendawazimu, Mnafiki na hajui Soka bali ni Shabiki Takataka na siyo Mdau na Mdaawa wa Mchezo wa Soka kama tulivyo Wapenda Haki wengine.

Najiandaa sasa Kusoma Comments za Wanasimba Wendawazimu ambao watakuja Kunishambulia hapa JamiiForums baada ya Kusema huu Ukweli.

Mimi ni Bahari huwa sikai na Uchafu!!!

Bujibuji Simba Nyanaume

IMG-20220204-WA0005.jpg


IMG-20220204-WA0006.jpg
 
Naipenda sana Simba SC yangu na natamani tushinde ila siyo kwa Kubebwa ( Mbeleko ) kama hii ya Leo.

Wana Simba SC mtakaonichukia kwa hili nichukieni na mkiweza nitukaneni mnavyoweza ila kwa 100% Ushindi wa leo tumebebwa na Mwamuzi.

Tunapokuwa Kila Siku tunawasema Yanga SC na GSM kuwa Wanahonga Waamuzi basi kwa huu Upumbavu na Upuuzi uliotokea leo nasi Simba SC tukubali kuwa METL nao wameamua rasmi sasa Kuingia Kazini.

Nje ya Kushinda kwa Goli la Msanii wa Injili Rose Mhando la Nibebeeee...Nibebeeeee... bado hata leo Simba SC yetu imecheza mpira mbovu na usipeleweka hali inayonifanya niamini kuwa huenda Makocha weru ni tatizo au Wachezaji weru Uwezo wao umefikia Kikomo ili tujipange Kufanya Usajili wa maama Msimu ujao.

TFF, TPLB na Kamati ya Saa 72 nawaombeni hata msichelewe Kukaa Kikao cha Kumfungia huyu Mwamuzi ambaye ana jina la Ubini la Simba hivyo yawezekana alitaka Kulifurahisha hilo Jina kwa Kuibeba wazi wazi Simba SC kwa kuipa Penati leo.

Mwanasimba yoyote ambaye atabisha au atanibishia kuwa leo Simba SC tumebebwa kwa kupewa ile Penati iliyotupa Ushindi ajiite ni Mwendawazimu, Mnafiki na hajui Soka bali ni Shabiki Takataka na siyo Mdau na Mdaawa wa Mchezo wa Soka kama tulivyo Wapenda Haki wengine.

Najiandaa sasa Kusoma Comments za Wanasimba Wendawazimu ambao watakuja Kunishambulia hapa JamiiForums baada ya Kusema huu Ukweli.

Mimi ni Bahari huwa sikai na Uchafu!!!

Bujibuji Simba Nyanaume
Mimi ni mwendawazimu

Penati ya haki kabisa
 
Ushirikina ulikuwepo enzi na enzi. Lakini sisi tuliokombolewa na Damu ya Yesu ya thamani(Simba) tunapinga ushirikina kwa nguvu zote.

Ibilisi hawezi kumshinda Mungu kwamwe. Ni suala la muda tu.
Sasa Straika Wapo Wanapoteza Nafasi Za Kufunga Unasema Ushirikina????

Kukombolewa Gani Huko Mkuu Fatilia Vizuri Mfumo Mnaocheza Pia Aina Ya Wachezaji Ulionao Na Si Kuamini Vitu Visivyo Na Msingi.
 
Bora mkuu wewe umeongea uhalisia wa timu.

Hayo ni matatizo ya mwalimu wa timu na si la wachezaji.Wachezaji wanafuata Maelekezo.

Sisi tunawaponda mawinga wakimbiaji wazuri kwa kuwaita wakimbiza upepo,laikini mpira wa sasa unataka spidi.Hata uzuri wa pasi utauona wakati mpira uko kwenye spidi na pace ya mchezo iwe juu
Kabisa mkuu na unakuta kabisa sometimes timu imepaki basi lakini njia mbadala huwa hatuna ....tunalazimisha Tu vipasi vya penetration.

Pia tunapiga pasi nyingi fupifupi as if tunahitaji kupiga pasi 10000 while tunachohitaji ni magoli. Baadhi ya pasi hazina msingi Kwa mm navyoona maana sio kila mpira lazima aguse manula-onyango-enock-mwenda-shabalala'mkude-mara umerud kwa enonga tena ......too boring ....

Sijui saiv tumekuaje maana tunashindwa kufanya transformation ya haraka tunapokua tunashambuliwa then timu pinzani Ikalose possession ya mpira Sisi tukafanya counter attack Kwa haraka. Maana kama timu imepaki basi muda mwingi na mara moja ikapanda then huo ndo muda wa kuiumiza lakini utakuta tupo slow kuondoka Kwa haraka.

strikers binafsi naona hatuna toka msimu ulipoanza ila Kwa mpira tunaocheza sometimes hata huyo striker kupigiwa mipira ni Kwa mbinde ...unakuta anabaki kama mtalii wa ndani ni mwendo t wa pasi weee mara wamekaba.

Kuna muda unapokamiwa ndo muda wa kuonesha uwezo binafsi kwann unacheza timu kubwa ,unalipwa vizuri ,Una kila mahitaji ya kukufanya ucheze mpira. mchezaji hata kuwapita wachezaji wawili watatu ni tatizo duh [emoji119]

Mtazamo wangu wakuu wala nisipigwe mawe.
 
Back
Top Bottom