Dr Restart
JF-Expert Member
- Jul 15, 2021
- 4,949
- 24,046
Wasalaam wapendwa wa MMU.
Kumezuka na msemo maarufu wa vijana haswa wa kike 'unataka kuwajua maEX wangu, unataka kuwanunulia gari?'
Huu msemo una nia ya kupotosha. Zaidi, kuwatia watu katika mahusiano yatakayoandamwa na changamoto nyingi. Nakusihi, ni vema kujua historia ya mahusiano ya mpenzi wako (uliye na nia naye) kabla ya kuamua kujiingiza mazima.
Sababu zifuatazo hapa chini zinadhihirisha umathubuti wa ushauri wangu:
a) Itakusaidia kuepukana na magonjwa.
Lazima ufahamu mtu huyo aliachana na mpenzi wake wa zamani kwa sababu zipi. Watu wengine huachana kwa sababu za kiafya. Mwenzake kaukwaa, akaamua kumkimbilia. Hii itakusaidia katika kuchukua tahadhari zote muhimu kuhakikisha kama yeye pia hajaambukizwa.
b) Wengine wameachana, lakini bado mmoja ana kisasi na mwenzake.
Kuachana kwingi ni kwa shari. Mahusiano mengi huvunjika kwa malumbano. Ni wachache wanaoachana kwa amani. Sasa, itokeapo kuna mtu anapanga kisasi kwa mwenzake, hali hiyo itakuathiri nawe moja kwa moja.
c) Sababu za kitabia zisizovumilika.
Kuna wengine huachana kwa sababu ya kushindwana kitabia. Mwenzi mmoja alikuwa mlevi, malaya, mshirikina au tabia yeyote isiyopendeza. Hii itakusaidia nawe kuona kama utaweza kuendana naye kabla ya kuamua kuwa serious na mhusika.
d) Changamoto za kutoweza kupata mtoto ama uwezo wa kuzalisha.
Mahusiano mengine huvunjika kwa sababu mmoja wao ameshindwa kufanikisha upatikanaji wa mtoto. Naam, kuna wengine mtoto si kipaumbele. Lakini, wengine ni muhimu sana kuwa na mtoto.
Hivyo, ukijua wameachana kwa sababu hizo, utajipima kuona kama je, utaweza kuvumilia katika hali ya namna hiyo? Kama ndiyo, go ahead. Kama siyo, usijiingize kwenye hayo mahusiano.
e) Wengine bado wapo kwenye mahusiano. Mtu ni mke wa mtu, lakini anaamua kukuficha ili afanikishe azma yake. Utakuja kufanyiwa kitu mbaya wakati hukukusidia. Wapo wengi wameumia kwa sababu hawakujua hapo kabla.
Zipo sababu nyingi za kwa nini ni muhimu kufahamu historia ya mahusiano ya unayetaka kujiingiza kwenye mahusiano naye.
Kama ambavyo ni vema kufanya research kabla ya kuamua kujiingiza katika biashara fulani, ndivyo hivyo katika mahusiano.
Hii ni ile uwe na mahusiano imara na thabiti. Japo haitazuia changamoto, lakini angalau utajiweka katika nafasi ya unafuu wa kuzitatua.
Fanya uchunguzi Mkuu.
Kumezuka na msemo maarufu wa vijana haswa wa kike 'unataka kuwajua maEX wangu, unataka kuwanunulia gari?'
Huu msemo una nia ya kupotosha. Zaidi, kuwatia watu katika mahusiano yatakayoandamwa na changamoto nyingi. Nakusihi, ni vema kujua historia ya mahusiano ya mpenzi wako (uliye na nia naye) kabla ya kuamua kujiingiza mazima.
Sababu zifuatazo hapa chini zinadhihirisha umathubuti wa ushauri wangu:
a) Itakusaidia kuepukana na magonjwa.
Lazima ufahamu mtu huyo aliachana na mpenzi wake wa zamani kwa sababu zipi. Watu wengine huachana kwa sababu za kiafya. Mwenzake kaukwaa, akaamua kumkimbilia. Hii itakusaidia katika kuchukua tahadhari zote muhimu kuhakikisha kama yeye pia hajaambukizwa.
b) Wengine wameachana, lakini bado mmoja ana kisasi na mwenzake.
Kuachana kwingi ni kwa shari. Mahusiano mengi huvunjika kwa malumbano. Ni wachache wanaoachana kwa amani. Sasa, itokeapo kuna mtu anapanga kisasi kwa mwenzake, hali hiyo itakuathiri nawe moja kwa moja.
c) Sababu za kitabia zisizovumilika.
Kuna wengine huachana kwa sababu ya kushindwana kitabia. Mwenzi mmoja alikuwa mlevi, malaya, mshirikina au tabia yeyote isiyopendeza. Hii itakusaidia nawe kuona kama utaweza kuendana naye kabla ya kuamua kuwa serious na mhusika.
d) Changamoto za kutoweza kupata mtoto ama uwezo wa kuzalisha.
Mahusiano mengine huvunjika kwa sababu mmoja wao ameshindwa kufanikisha upatikanaji wa mtoto. Naam, kuna wengine mtoto si kipaumbele. Lakini, wengine ni muhimu sana kuwa na mtoto.
Hivyo, ukijua wameachana kwa sababu hizo, utajipima kuona kama je, utaweza kuvumilia katika hali ya namna hiyo? Kama ndiyo, go ahead. Kama siyo, usijiingize kwenye hayo mahusiano.
e) Wengine bado wapo kwenye mahusiano. Mtu ni mke wa mtu, lakini anaamua kukuficha ili afanikishe azma yake. Utakuja kufanyiwa kitu mbaya wakati hukukusidia. Wapo wengi wameumia kwa sababu hawakujua hapo kabla.
Zipo sababu nyingi za kwa nini ni muhimu kufahamu historia ya mahusiano ya unayetaka kujiingiza kwenye mahusiano naye.
Kama ambavyo ni vema kufanya research kabla ya kuamua kujiingiza katika biashara fulani, ndivyo hivyo katika mahusiano.
Hii ni ile uwe na mahusiano imara na thabiti. Japo haitazuia changamoto, lakini angalau utajiweka katika nafasi ya unafuu wa kuzitatua.
Fanya uchunguzi Mkuu.