Ni muhimu sasa kuwa na muongozo wa msafara wa Rais pamoja na gari maalumu lenye hadhi na cheo maalum

Ni muhimu sasa kuwa na muongozo wa msafara wa Rais pamoja na gari maalumu lenye hadhi na cheo maalum

Jackbauer

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2010
Posts
6,053
Reaction score
2,207
Kufuatia sintofahamu iliyotokea huko UK ambapo Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameonekana kwenye basi lililoandaliwa kuingiza viongozi wa mataifa mbalimbali kwenye eneo la kuaga mwili wa malikia Elizabeth Il.

Inawezekana tukapiga kelele sana ingawa tukashindwa kuwa na sababu thabiti za kwa nini Rais wetu asipande basi?

Binafsi ninapenda kufuatilia protokali za namna viongozi wetu wanapokelewa huko ughaibuni na kulinganisha na sisi tunavyowapokea na kuwatreate viongozi au hata watu maarufu wao.

Hakuna shaka kuwa bado kuna ombwe na utofauti mkubwa.

Nitatoa mfano wa hili kwa kuangazia na kukumbushia tukio la takribani mwezi mmoja uliopita.

Katika mashindano ya michezo ya jumuiya ya madola nilisikitishwa kuona balozi wetu nchini UK akiwa katikati ya msongamano wa wananchi wa kawaida pale aliposhihudia wanariadha watanzania wakituwakilisha vyema katika mashindano hayo.

Balozi Migiro alikuwa amebanwa sana, hakuwa jukwaa kuu kama nilivyotaraji na ilionekana waandaaji hawakuwa na protokali ya kumualika au kuheshimu uwepo wake kwenye michezo hiyo adhimu, iliniudhi.
kwa Tanzania balozi wa uingereza akiwa kwenye shughuli ya namna hiyo ni lazima tumgempa heshima stahiki pamoja na ulinzi wa kipekee.

Inawezekana haya yanatokea pengine kwa kuwa hatuna miongozo rasmi ya namna msafara wa Rais wetu tunataka iwe popote pale anapoenda na isipokuwa hivyo basi sheria kanuni na taratibu zinakuwa zimekiukwa.

Hivyo ni muhimu sasa kwa guru's wote wa diplomasia na protokali kuja na maboresho muhimu na ya kisheria(legal binding) yanayohusu misafara, haiba na nembo mbalimbali za utawala.

Aidha hata picha rasmi zinazotolewa lazima zizingatie sheria yaani tutunge sheria rasmi ya privacy ya Rais na viongozi wetu wakuu.atakayerusha picha yoyote ya Rais iwe popote pale lazima awe na kibali maalumu.

Ni hayo tu.
 
Hao wazungu wanajua viongozi wetu wengi huwa wanaingia madarakani kwa kupora uchaguzi. Hivyo mtu aliye madarakani bila ridhaa ya wananchi ni kumpakiza kwenye Abood fullstop. Hayo maVX waende wakapakie kwenye nchi zao wanakopora uchaguzi.
 
Hao wazungu wanajua viongozi wetu wengi huwa wanaingia madarakani kwa kupora uchaguzi. Hivyo mtu aliye madarakani bila ridhaa ya wananchi ni kumpakiza kwenye Abood fullstop. Hayo maVX waende wakapakie kwenye nchi zao wanakopora uchaguzi.
Kuna kiongozi aliyepora madaraka karuhusiwa kuingia UK?
 
Hao wazungu wanajua viongozi wetu wengi huwa wanaingia madarakani kwa kupora uchaguzi. Hivyo mtu aliye madarakani bila ridhaa ya wananchi ni kumpakiza kwenye Abood fullstop. Hayo maVX waende wakapakie kwenye nchi zao wanakopora uchaguzi.
Abood Ya Uingereza Noma Wangewapa Karanga Watafune
 
Kweli inasikitisha sana. Hapo ulipoliona la Balozi kubanwa

Ni hivi huwa hatujiandai ki protokali yaani tunaenda tu

Nakumbuka miaka ya 80 kuna balozi wetu wa nchi moja mashariki ya Kati alisafiri kama kawaida toka Dar ila alipofika nchi nyingine kukikuwa hakuna maandalizi yoyote na wao hawakumjua ni nani na kuanza kuishangaa passport yake

Halafu kiarabu hajui na wao English hawajui

Jamaa mmoja akamuuliza kuna nini akasema mimi ni Balozi mpya

Baada ya kuwaambia kiarabu wakamuambia sasa kwa nini ameshukukia hapa aende VIP LOUNGE

Ndio wakampeleka hii ni true story na ilitokea

Wenzetu wanajiandaa kwa kila kitu mpaka mapokezi yao
 
Yaani waongeze tozo ili msafara wa rais uende ziara na magari yake kama ulivyo Msafara wa rais wa marekani wanaobeba na magari Yao?
 
Imeisha iyo, unataka kumzika Bibi,panda Adventure,hutaki lala mbele!!
 
Nyie watu wa JF mnajua kujitoa ufahamu kweli kweli walahi!

Kati ya marais na mawaziri wakuu walioenda UK ni nchi sita tu ndio marais wao waliruhusiwa kuwa na magari yao wenyewe ambao ni marekani, Israel, Canada, German, Japan na ufaransa, wengine wote ni mabasi!
Kina Australia na nchi kubwa nyingine zilikuwa mwendo huo huo jamani dunia sio tambarare ambapo kila mtu ni sawa [emoji15]
Sio kweli!
Vitu vingine sio vya kulalamika inaonekana kama tahira walahi [emoji3062]
 
Haya yote yanatusaidia nini wakati watu hata tozo tu ni taabu. Yaani sisi abao tunataka tozo zitolewe na kutafuta pesa tunapoteza muda kujadili mabasi na magari. Unajua kwamba hayo mabasi ni bullet proof. Kuna wakuu wa nchi EU hawana hata magari wala misafara.
 
Back
Top Bottom