Ni muhimu sasa kuwa na muongozo wa msafara wa Rais pamoja na gari maalumu lenye hadhi na cheo maalum

Ni muhimu sasa kuwa na muongozo wa msafara wa Rais pamoja na gari maalumu lenye hadhi na cheo maalum

Kweli inasikitisha sana
Hapo ulipoliona la Balozi kubanwa
Ni hivi huwa hatujiandai ki protokali yaani tunaenda tu
Nakumbuka miaka ya 80 kuna balozi wetu wa nchi moja mashariki ya Kati alisafiri kama kawaida toka Dar ila alipofika nchi nyingine kukikuwa hakuna maandalizi yoyote na wao hawakumjua ni nani na kuanza kuishangaa passport yake
Halafu kiarabu hajui na wao English hawajui
Jamaa mmoja akamuuliza kuna nini akasema mimi ni Balozi mpya

Baada ya kuwaambia kiarabu wakamuambia sasa kwa nini ameshukukia hapa aende VIP LOUNGE
Ndio wakampeleka hii ni true story na ilitokea
Wenzetu wanajiandaa kwa kila kitu mpaka mapokezi yao
Kwa maana hiyo, huyo balozi mpya alikaa kwenye siti za nzengo, maana kama angelikaa VIP si wana mlango wao wa kupita tofauti na sisi wabana matumizi?
 
Wabongo bana. Badala uhangaike na tozo unahangaika na viongozi hawa mabilionea wenye hela za kula wao, watoto wao, wajukuu, vilembwe mpaka vizazi hata 10 vijavyo bila kufanya kazi. Leo unahangaika eti nao wakisafiri waende na The Beast na Air Force One zao kama Biden. Mi ningependa hata wakija huku nyumbani wapande mabasi au Rav4 na siyo hii misafara ya mavieite ghali zaidi ya 80....😬😬😬
 
Viongozi wa afrika wanajulikana kwa misafara. Kiongozi mmoja gari zaidi ya 200,wewe unadhani pangetosha hapo. Wazungu ni wajanja walilijua mapema.
 
Nyie watu wa JF mnajua kujitoa ufahamu kweli kweli walahi!
Kati ya marais na mawaziri wakuu walioenda UK ni nchi sita tu ndio marais wao waliruhusiwa kuwa na magari yao wenyewe ambao ni marekani, Israel, Canada, German, Japan na ufaransa, wengine wote ni mabasi!
Kina Australia na nchi kubwa nyingine zilikuwa mwendo huo huo jamani dunia sio tambarare ambapo kila mtu ni sawa [emoji15]
Sio kweli!
Vitu vingine sio vya kulalamika inaonekana kama tahira walahi [emoji3062]
Mfaransa naye alifutikwa ndani ya abood?
 
Wabongo bana. Badala uhangaike na tozo unahangaika na viongozi hawa mabilionea wenye hela za kula wao, watoto wao, wajukuu, vilembwe mpaka vizazi hata 10 vijavyo bila kufanya kazi. Leo unahangaika eti nao wakisafiri waende na The Beast na Air Force One zao kama Biden. Mi ningependa hata wakija huku nyumbani wapande mabasi au Rav4 na siyo hii misafara ya mavieite ghali zaidi ya 80....😬😬😬
Unamaanisha hata kama tuna shida tusijadili sio. Mkuu sio kila muda ni kujihangaisha na maisha....huoni umuhimu hata wa dakika mbili za umbea
 
wazungu bado hawaitambui Africa wanajua bado iko gizani.
Mzungu mmoja aliitukuza sana bongo akaniambia kuna muujiza unatokea BONGO eti wazungu hawaelewi marais wetu wanaachianaje kiti bila bunduki!

Wazungu wanaamini evolution bado inaendelea watu weusi babu zao nyani, ulaya mtumishi wa umma anaogopa raia, magari yanaogopa watembea kwa miguu! Tozo zinajenga nchi raia mnaona je huku kwetu kukoje?

ila coverage ya English channel BBC wanamuonesha sana Bimkubwa hadi raha, wazungu wanampenda sana Maza wetu sehemu nyingi mara nyingi nimemuona Maza, ila Marais wengine wa Afrika ni weusi sana na wengi ni madikteta, yote hayaoneshwi na BBC labda TV za kwao! mi sijaona hata dikteta mmoja!
 
Hakuna sintofahamu yoyote iliyotokea huko UK, ni ushamba tu, kukosa exposure na uelewa mdogo wa wabongo wengi.
UK ina balozi 164 wakati Tanzania ina balozi 33. Serikali ya UK HaiwezI kufuata protokali za kila nchi katika uangalizi wa mabalozi wao.
Itakuwa usumbufu mkubwa sana kwa raia wake.

Balozi wa nchi yako akiwa UK atafuata protokali za huko, atakuwa salama na atafanya kazi yake ya msingi bila bugdha, huko kujimwambafy kwingine hakuna nafasi.
Kufuatia sintofahamu iliyotokea huko UK ambapo Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameonekana kwenye basi lililoandaliwa kuingiza viongozi wa mataifa mbalimbali kwenye eneo la kuaga mwili wa malikia Elizabeth Il.
Inawezekana tukapiga kelele sana ingawa tukashindwa kuwa na sababu thabiti za kwa nini Rais wetu asipande basi?
Binafsi ninapenda kufuatilia protokali za namna viongozi wetu wanapokelewa huko ughaibuni na kulinganisha na sisi tunavyowapokea na kuwatreate viongozi au hata watu maarufu wao .

Hakuna shaka kuwa bado kuna ombwe na utofauti mkubwa .
Nitatoa mfano wa hili kwa kuangazia na kukumbushia tukio la takribani mwezi mmoja uliopita.
Katika mashindano ya michezo ya jumuiya ya madola nilisikitishwa kuona balozi wetu nchini UK akiwa katikati ya msongamano wa wananchi wa kawaida pale aliposhihudia wanariadha watanzania wakituwakilisha vyema katika mashindano hayo.
Balozi Migiro alikuwa amebanwa sana ...hakuwa jukwaa kuu kama nilivyotaraji na ilionekana waandaaji hawakuwa na protokali ya kumualika au kuheshimu uwepo wake kwenye michezo hiyo adhimu...iliniudhi.
kwa Tanzania balozi wa uingereza akiwa kwenye shughuli ya namna hiyo ni lazima tumgempa heshima stahiki pamoja na ulinzi wa kipekee.

Inawezekana haya yanatokea pengine kwa kuwa hatuna miongozo rasmi ya namna msafara wa Rais wetu tunataka iwe popote pale anapoenda na isipokuwa hivyo basi sheria kanuni na taratibu zinakuwa zimekiukwa.

Hivyo ni muhimu sasa kwa guru's wote wa diplomasia na protokali kuja na maboresho muhimu na ya kisheria(legal binding) yanayohusu misafara ,haiba na nembo mbalimbali za utawala.
Aidha hata picha rasmi zinazotolewa lazima zizingatie sheria yaani tutunge sheria rasmi ya privacy ya Rais na viongozi wetu wakuu.atakayerusha picha yoyote ya Rais iwe popote pale lazima awe na kibali maalumu.

ni hayo tu.
 
Hakika
mkuu hao viongozi ufahari wanaouonyesha kwenye nchi zao,matumizi mabaya ya fedha za umma na umasikini uliopo huku kwenye nchi zao ni msiba mkubwa kuliko huo msiba wa huyo mmbibi.
 
Unalinganisha viongozi wengine na head of states?
Kazi ishaisha jana
Wenye usalama wao wamefanikisha
D43C5F1E-ABF9-4953-AB78-4E567F6A5763.jpeg
 
Nyie watu wa JF mnajua kujitoa ufahamu kweli kweli walahi!
Kati ya marais na mawaziri wakuu walioenda UK ni nchi sita tu ndio marais wao waliruhusiwa kuwa na magari yao wenyewe ambao ni marekani, Israel, Canada, German, Japan na ufaransa, wengine wote ni mabasi!
Kina Australia na nchi kubwa nyingine zilikuwa mwendo huo huo jamani dunia sio tambarare ambapo kila mtu ni sawa [emoji15]
Sio kweli!
Vitu vingine sio vya kulalamika inaonekana kama tahira walahi [emoji3062]
Hata wa Canada na Ufaransa walipanda basi.
 
Wanangu tujitahidi kutafuta maarifa unless tutazudi kuaibika. Wewe unafikiri kuruhusu Kila mkuu wa nchi awe na convoy yake hapo London pangetosha?
Mimi nashindwa kuwaelewa hawa wanaolalamika wakati karibu Marais wote siyo tu waliotoka Africa but Asia, Europe, South America walikuwa kwenye buses. Watu wameenda kuzika hawakwenda kwenye ziara binafsi za nchi husika. Viongozi wa nchi zaidi ya 100 kila mtu awe na motorcade yake how comes????!!!!
 
kwani convoy moja ina magari mangapi?na yanachukua urefu na upana upi?argue scientifically
Scientifically? Uwezo wako mdogo, kulalamika tu Kila siku Kama vile una mtindio wa ubongo. Wenzetu wanaamini binadamu wote ni sawa. Na wameonesha Dunia ulinzi uliotukuka Kwa kuhakikisha usalama wa viongozi wote unazingatiwa.
 
Kufuatia sintofahamu iliyotokea huko UK ambapo Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameonekana kwenye basi lililoandaliwa kuingiza viongozi wa mataifa mbalimbali kwenye eneo la kuaga mwili wa malikia Elizabeth Il.
Inawezekana tukapiga kelele sana ingawa tukashindwa kuwa na sababu thabiti za kwa nini Rais wetu asipande basi?
Binafsi ninapenda kufuatilia protokali za namna viongozi wetu wanapokelewa huko ughaibuni na kulinganisha na sisi tunavyowapokea na kuwatreate viongozi au hata watu maarufu wao .

Hakuna shaka kuwa bado kuna ombwe na utofauti mkubwa .
Nitatoa mfano wa hili kwa kuangazia na kukumbushia tukio la takribani mwezi mmoja uliopita.
Katika mashindano ya michezo ya jumuiya ya madola nilisikitishwa kuona balozi wetu nchini UK akiwa katikati ya msongamano wa wananchi wa kawaida pale aliposhihudia wanariadha watanzania wakituwakilisha vyema katika mashindano hayo.
Balozi Migiro alikuwa amebanwa sana ...hakuwa jukwaa kuu kama nilivyotaraji na ilionekana waandaaji hawakuwa na protokali ya kumualika au kuheshimu uwepo wake kwenye michezo hiyo adhimu...iliniudhi.
kwa Tanzania balozi wa uingereza akiwa kwenye shughuli ya namna hiyo ni lazima tumgempa heshima stahiki pamoja na ulinzi wa kipekee.

Inawezekana haya yanatokea pengine kwa kuwa hatuna miongozo rasmi ya namna msafara wa Rais wetu tunataka iwe popote pale anapoenda na isipokuwa hivyo basi sheria kanuni na taratibu zinakuwa zimekiukwa.

Hivyo ni muhimu sasa kwa guru's wote wa diplomasia na protokali kuja na maboresho muhimu na ya kisheria(legal binding) yanayohusu misafara ,haiba na nembo mbalimbali za utawala.
Aidha hata picha rasmi zinazotolewa lazima zizingatie sheria yaani tutunge sheria rasmi ya privacy ya Rais na viongozi wetu wakuu.atakayerusha picha yoyote ya Rais iwe popote pale lazima awe na kibali maalumu.

ni hayo tu.
Ni sisi waafrika ndio tunaocomplicate mambo kufikiri kupanda basi ni udhaifu. Tuache ujinga.
 
Kwa maana hiyo, huyo balozi mpya alikaa kwenye siti za nzengo, maana kama angelikaa VIP si wana mlango wao wa kupita tofauti na sisi wabana matumizi?
Halafu cha kushangaza alipanda economy class kama mtalii tu haha
Kwa Africa huwa tunajijua wenyewe tu

Usishangae hata kwenye Bus lile waliomba maji na korosho
 
Back
Top Bottom