Uchaguzi 2020 Ni muujiza pekee utakaoifanya CCM wabaki wamoja baada ya uchaguzi utakaofanyika mwishoni mwa mwaka huu

Uchaguzi 2020 Ni muujiza pekee utakaoifanya CCM wabaki wamoja baada ya uchaguzi utakaofanyika mwishoni mwa mwaka huu

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Kuna mlolongo wa matukio yanayotokea nchini hivi sasa, yanayonifanya niweze kutabiri yatakayotokea nchini baada ya uchaguzi mkuu utakaofanyika nchini kwetu mwishoni mwa mwaka huu

Tulimsikia wenyewe Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Magufuli akitamka hadharani bila kificho chochote kuwa kura za maoni za vikao vya CCM vya majimbo mwaka huu si lolote wala chochote mwaka huu, kwani mwenye uwezo wa kuamua ni nani atakuwa mgombea wa ubunge mwaka huu, kwa tiketi ya CCM, atakuwa yeye mwenyewe Mwenyekiti wa CCM Taifa!

Akaendelea kusisitiza kuwa yeye mwenyewe anaweza kumpitisha yule mgombea aliyekuwa wa kumi, katika mchakato wa kura za maoni majimboni kwenu, akiwaacha wale wote walioongoza kwa maana ya wa kwanza hadi wa tisa.na wala hatalazimika kutoa sababu zozote!

Hivi ndivyo ilivyo CCM ya Magufuli, katika kipindi hiki, ambapo yeye hazingatii tena Katiba ya Chama chake inasema nini, bali matakwa yake binafsi, ndiyo yanayozingatiwa

Tumeshuhudia Rais Magufuli akifanya uteuzi mpya wa zaidi ya watumishi 33, katika maandalizi ya uchaguzi mkuu mwishoni mwaka huu, wakiwemo watu "wake" wa karibu wakuu wa mikoa ya Dar na Manyara, Paul Makonda na Alexander Mnyeti "akiwapumzisha" akiwaandaa kuwa waheshimiwa wabunge, baadaye mwaka huu!

Hao ni miongoni ya wale ambao piga ua ni lazima atawateua yeye kuwa wagombea ubunge, kwenye majimbo yao, bila kujali matokeo ya kura za maoni za majimbo husika!

Vile vile jambo lingine litakaloleta chuki kubwa na mtifuano ndani ya CCM, ni kwa wale wanachama wapya wa "kuja" kupewa kipaumbele katika nafasi za kugombea, wakati wale wanachama "asilia" wakiendelea kusugua benchi

Ndipo hapo ninapojiuliza hivi CCM itaendelea kubaki moja baada ya uchaguzi mwishoni wa mwaka huu, licha ya Mwenyekiti kuwa tayari na watu wake katika nafasi za ubunge kwenye majimbo hayo?

Nimekuwa nikijiuliza pia, ni kwanini Mwenyekiti atumie nguvu kubwa kutaka kuwasimika ubunge wa majimbo, wakati yeye anayo nafasi ya Kikatiba ya kuteua wabunge wake yeye mwenyewe, wasiozidi kumi?

Hivi hii hali haitaleta chuki kubwa miongoni ya wagombea wa CCM, watakaokuwa wamekatwa majina yao, licha ya kuwa wameongoza kwenye kura za maoni kwenye majimbo yao?

Tusubiri kuona mtifuano mkali baina ya wale "wateuliwa maalum" wa nafazi za ubunge wa Mwenyekiti na wale ambao watakuwa ndiyo chaguo la wapiga kura majimboni mwao
 
chagu wa malunde
Mbona povu jingi linakutoka?

Jikite kwenye kujibu hoja iliyopo mezani Mkuu
Nakuuliza halimashuri kuu ya Ccm ni JPM peke yake? Maana unaongea uongo mtupu, maana halmashuri kuu inayopitisha majina ina wajumbe wengi . Na alipozungumzia mfano wa Ndumbaro hakumaanisha kuwa anaamua peke yake.
 
Huna mume wa kukuondolea usingizi? Unapost upuuzi tu. Lini rais alisema yeye binafsi anamamlaka ya kumpitisha anaemtaka? Halmashuri kuu ya Ccm ni mwenyekiti peke yake? Au unapenda kugeuza maneno tu.
Una ushahidi gani ametuma hao wateule maalumu au unafanya mambo kwa hisia tu.
Mmejazana hapo Bawacha hata kuolewa hamuolewi mmebakiza kuwaza uongo tu.
Kwanza unajua siri ya haya mafuriko ya watia nia wa CCM?

Ni kutokana na jinsi Mwenyekiti wenu alivyokigeuza chama cha CCM na kukifanya chake binafsi, huku akitumia vyombo vya dola kuendelea kubaki madarakani..

Kwa hiyo kila mtia nia anaamini kwa asilimia 100, kuwa akiteuliwa kwa tiketi ya CCM basi ndiyo kawa mbunge tayari!
 
Acha kupost pumba zako. Mchakato ni mrefu sana na mpaka halmashuri kuu ipitishe jina sio jambo dogo.Mafuriko ni sababu Ccm imenona na ndio maana kila mtu anaikubali.
Kwanza unajua siri ya haya mafuriko ya watia nia wa CCM?

Ni kutokana na jinsi Mwenyekiti wenu alivyokigeuza chama cha CCM na kukifanya chake binafsi.......

Kwa hiyo kila mtia nia anaamini kwa asilimia 100, kuwa akiteuliwa kwa tiketi ya CCM basi ndiyo kawa mbunge tayari!
 
chagu wa malunde
Mkuu jikite kwenye mada, hiyo lugha yako ya matusi iache huko huko Lumumba
Hakuna lugha ya matusi hapo. Ccm ni chama kinchoendeshwa kwa katiba na kanuni. Halmshauri kuu au Cc inafuata misingi ya katiba na kanuni za chama. Kama mtu anapitishwa atapitishwa kwa kufuata katiba na kanuni za chama sio maamuzi ya mtu mmoja. Acha kupotosha umma.
 
Ni kweli mkuu Rais alisema atashughulika na wwgombea ....na inategemeana Siku hiyo ameamkaje!
 
Ni kweli mkuu Rais alisema atashughulika na wwgombea ....na inategemeana Siku hiyo ameamkaje!
Bora umemfafanulia huyo "Praise & worship team for Magufuli" ili imwingie hiyo hoja na aielewe
 
Mtu anayefikiri kwa kutumia makalio ndio ana fikra kama zako.
Mtakuwa mmefilisika kisiasa

Ni kwanini nyinyi watu wa Lumumba, mkiona hoja zimewazidi kimo na hamna ubavu wa kuzijibu, mnakimbilia kutoa matusi?
 
Nyiye watu wa Lumumba, mkiona hoja zimewazidi kimo na hamna uwezo wa kuzijibu, ndiyo mnakimbilia matusi!
Nani mtu wa Lumumba? Mpuuzi huyo anavyosema ninalipwa ana uhakika?
Kwani hajui kuwa NEC ya Ccm ni chombo huru?
 
Safari hii mambo yamebadilika, wagombea watakatwa na jpm kwanza, kisha majina matatu yatarudishwa kupigiwa kura. Naona jpm ananoa kisu ili akate majina now
 
Huo mlolongo wa watia nia kuwa wengi ni kutokana na kuamini kuwa wagombea wa CCM watashinda kwa nguvu kwa hiyo watia nia wanachotaka ni kuwa sehemu ya CCM tu kusudi wakiwfanikiwa wapate kipande cha keki. Wengi wa watakaoshindwa bado wataenedelea kubaki wafuasi wakuu kwa kuangalia nafasi za kuteuliwa.

Mwaka 2010 wakati CCM ikiwa ndani ya muhula wa zomewa zomewa, watia nia hawakuwa wengi vile.
 
Duh! Bora Mie nagombea kwenye chama chetu cha wagema ulimbo, hatutoguswa na maamuzi yake
Nalog off
 
Back
Top Bottom