Uchaguzi 2020 Ni Mwaka wa Uchaguzi Mkuu 2020: Kuthibitisha au Kutengua Maamuzi ya 2015?

Uchaguzi 2020 Ni Mwaka wa Uchaguzi Mkuu 2020: Kuthibitisha au Kutengua Maamuzi ya 2015?

JokaKuu, mojawapo ya mambo mabaya sana ambayo yametokea na yanaendelea kutokea ni hii imani kuwa migogoro ya kisiasa mwisho wake ni ubaya tu. Demokrasia hujengwa kwa migogoro, kupingana na wakati mwingine huokolewa kwa jasho na damu. Hakuna nchi iliyojenga demokrasia ya kweli bila mivutano, misuguano, na hata minyukano. Sasa minyukano si lazima kwa demokrasia, lakini mivutano ni lazima. Tusiogope hii mivutano vinginevyo itakuwa ni kujaribu kuahirisha kisichoepukika. Hofu yangu tunajaribu kuchelewesha kinachotakiwa kufanyika.

Look here, kuna baadhi ya mambo serikali hii inafanya ni mazuri na hata wapinzani wanakiri. But call a spade a spade. Kinachoendelea nchini sasahivi siyo "mivutato" tu. Ni full-blown dictatorship. Marufuku inatangazwa na ukienda kinyume unakamatwa unawekwa ndani. Au unabambikiwa mashtaka yasiyo na dhamana. Ukiwa una bahati mbaya zaidi, utakutwa tu mahali ukiwa umepigwa uko hoi au hutaonekana kabisa. Umeshawahi kujiuliza kwanini hakuna kesi hata moja ya watu kuokotwa wakiwa wameumizwa, kupotea, kupigwa risasi ambayo imekuwa resolved awamu hii? Rais anazungumzia mpaka magomvi ya watu binafsi jukwaani lakini hazungumzii matukio ya kutisha yanayowatokea wananchi wake? Hujifunzi kitu chochote tu hapo, au ni makusudi?
 
Hivi, wakati wa Kikwete upinzani uliruhusiwa sana kufanya siasa bila vizingiti vyovyote? mbona siasa zilifanyika pamoja na songombingo zote za kisiasa?
Wewe tulia huko huko uliko ya huku tuachie wenyewe! Serikali la sasa hivi kama lifamiliya la mlevi!
 
Mwanakijiji unafahamu wazi kwamba ccm haikushinda urais 2015 lakini unaandika as if hulijui hilo ! ikiwa ukitaka wananchi wasibadilishe maamuzi ya 2015 basi chama chako kitaangukia pua
Hizi akili mgando zenu ndio zinafanya ccm iendelee kuwepo madarakani
Mzee Mwanakijiji ametoa threads nyingi sana kuhusu uchaguzi wa 2015,na kueleza kwa nini ccm ilishinda,na akaonya kama msipobadilika,2020 yatakua yale yale
Leo msukule unakuja na yale yale 2015,yatakusaidia nini?endelea kulia kuwa ccm haikushinda,bado miezi sita tu bunge livunjwe,hakuna anaesikiliza kilio chako kamanda,panga safu kuanzia sasa,usisubiri Membe akatwe
 
Mzee Mwanakijiji,
Umepoteza muda kutumia muda wako kuandika vitu vingi. Tanzania kuanzia 2015 iliingia kwenye siasa za Kinyarwanda baada ya makosa ya JK na Lowassa. Huyu aliyepo hawezi kuondoka kwa kipande cha karatasi. Huyu ataondolewa kwa kifo tu. Kama hamuwezi kumuua basi subiri Mwenyezi Mungu atakapochukua roho yake. Huyu ni uzao mmoja na Museveni, Kagame na Nkurunzinza. Hatoki
 
Hakutakua na uchaguzi mwaka huu kwa sababu anayeamua mshindi sio mpiga kura bali tume ya uchaguzi na CCM. Why waste time kwenda kupanga mstari na kupiga kura?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwanakijiji unafahamu wazi kwamba ccm haikushinda urais 2015 lakini unaandika as if hulijui hilo ! ikiwa ukitaka wananchi wasibadilishe maamuzi ya 2015 basi chama chako kitaangukia pua
Taja mikoa na majibu ambayo CDM ilishinda. Hii ya kila uchaguzi kuwa CDM ilishinda ni strategy za kijinga ili wakuu wa Sacco's wasichukuliwe hatua za kichama. Nyumbu wanafuata bila kuuliza maswali magumu. Long way to go
 
Hakuna wakumuondia Magufuli
Hizi ngonjera za Jf Zinaishia hapa hapa
 
Usipoteze muda kumwambia huyo jiwe worshiper uliyoandika sikwamba hayajui nivile kaamua kujitoa ufahamu tu! halafu kwenye paragraph ya mwisho sijaelewa uliposema wapinzani watumie njia mBadala kupata wanachama tofauti na mikutano ya hadhara ungeweka ushauri wako watumie njia ipi ikiwa hata mikutano yao ya ndani wanafuatwa na bunduki

Sent using Jamii Forums mobile app

Sipingani na Kalamu1 kwenye mengi ya mabandiko yake, ila kiukweli sijawahi kupata maelezo yaliyoonyooka jinsi ya kuweza kuwafikia watu. Maelezo anayoyatoa mara zote kuhusu kufikia watu katika mazingira haya, huwa nayaita mazingaombwe. Huenda akakuambia ww, lakini mimi simwelewi kabisa.
 
Hakuna wakumuondia Magufuli
Hizi ngonjera za Jf Zinaishia hapa hapa

Ni kweli usemayo, ila kutokuweza kumuondoa sio kwakuwa anakubalika sana, bali kwakuwa sasa hivi madaraka yake ndio yanayotumika kutangaza mshindi.
 
85%+ inamhusu Rais Magufuli, hakamatiki na sioni wa kupambana naye,time will tell.
Kwa sababu anamiliki power na sio uwezo wa kucompete kwenye field yeyeto iwe siasa,hoja,biashara,uchumi hawezi nje ya kubebwa.
 
Huu mwaka Wa uchaguzi dalili zaonyesha Maisha yatakuwa magumu zaidi hakutokuwa na new investment ndani au foreigners kwa sababu ya investment risk.Wanaomiliki uchumi sio blacks wa ndani watakimbiza pesa zao nje kulinda mitaji yao hofu ya hali itakavokuwa wameona uchaguzi serikali za mitaa ulivo so anything can happen the Hague possible,wa nje hawatoingiza Pesa zao kuivest ni hadi uchaguzi upite sababu upepo haueleweki.Kwa investor smart ni risk sana kuivest Africa,labda kama utafanya trial and error investment.Tujikaze mkanda kwelikweli.
 
..mnadhimu mkuu wa kambi ya upinzani kupigwa risasi 16 ktk eneo ambalo kwa kawaida lina walinzi wa serikali hiyo unaita ni mivutano na minyukano?

..na kwanini jasho na damu iwe kwa upande wa upinzani tu?

..mimi bwana SIUNGI MKONO dhuluma au ukatili wa aina yoyote ile ktk siasa zetu.

..kama ni minyukano basi iwe minyukano ya HOJA au SERA, lakini siyo minyukano ya KIJINAI,au KIGAIDI.

..kama wazee wetu walipata UHURU bila kumwaga DAMU, kwanini sisi watoto wao, au wajukuu wao, tumwage damu kwa ajili ya demokrasia.
Instagram media - Bt2Krycj3b7.jpg
 
Back
Top Bottom