Elections 2010 Ni nani aliyeingiza udini kwenye kampeni hizi?

Status
Not open for further replies.
KIONGOZI ATAYETUFAA SI YULE ATAYETUGAWA KWA MISINGI YA DINI, KABILA AU RANGI. HAKIKA HUYU HAWEZI KULETA MAENDELEO BALI VITA NA UMWAGAJI DAMU....I hope Slaa never said those words!! Kama ni kweli then HUYU HAFAI HATA KIDOGO
 
Hata ukisemaje Dr. Slaa Raisi wetu
 
Leo hii kwa mara ya kwanza nasema hivi...
Kama kweli Dr.Slaa amefikia kusema haya basi tumekwisha... Yaani hata sijui tena nani mbora baina yao!
Wewe Mkandara wote ninyi wapinzani wa Dr. Slaa leo hii unajifanya ulikuwa unampenda!! Kweli watanzania kinachotumaliza ni unafiki
 
Nilikuwa mmoja wa waumini wake pale Mnazi Mmoja kanisa la mito ya baraka sasa liko Jangwani. Anashangaza sana kukemea wakristo kukemea sera ya udinu ilhali yeye mwenyewe alikuwa wa kwanza kudai kuwa kikwete ni chaguo la mungu. Iweje Mungu achague mwana siasa wakati kuna maaskofu na wachungaji kwa ajili ya shughuli zake?
Ukisema wewe ni vema, wakisema wengine ni kosa? Kwani ni kosa gani kuitosa CCM?
 

Baraza la Mawaziri la Kikwete lina watu wangapi? Kwa nini usingeweka majina ya mawaziri wote na manaibu wao na ukaishia kuchagua majina unayodhani ni ya kiislamu tu? Kama kweli Dr. Slaa ameongea haya yaliyoandikwa basi I'm really disappointed
 

Wakati gani tutaongelea haya mambo, baada ya Slaa kuingia Ikulu?? Kwa nini dini imekuwa kigezo sasa ?? If there are more christian or more muslims, who gives a damn!! Unless you are segregating people based on their religion?? I say it again, if Slaa truly said those words, he has lost many supporters and yes huu ni wakati muafaka kujadili haya mambo
 
Lakuvunda halina ubani, hili limekorogwa bila hata ya chumvi. Nilishaongea tangu mwanzo kwamba timu mzima ya uhakiki wa kampeni za Chadema inabidi ibomolewe maana inafanya kazi kitoto. Hotuba za Dr Slaa zinakosa uhakiki, zinakosa uchambuzi. Bila utafiti Chadema walisema Karume hakuwa na elimu, bila utafiti wakaja na story kwamba kontena la kura za JK lipo Tunduma, Dr Slaa akaja kuushangaza umma kwamba hakujuwa kwamba mchumba wake alikuwa kaolewa, leo hii CCM wamemtega aongelee udini na yeye kaingia kichwa kichwa. Swali langu: hivi waandishi wa hotuba za Dr Slaa ni akina nani na wana ujuzi gani katika ku-digest kile anachokiongea Slaa na impact yake katika kampeni?
 

Hili Swala linaweza ku"torpedo" ndoto zote za Slaa na Chadema kupewa uongozi wa nchi hii.
na ikitokea Wa kulaumiwa watakuwa ni wao wenyewe, kwa kushindwa kuheshimu hisia za mamilioni ya wananchi wa nchi hii.

MOD USIITOE MADA HII IACHE HAPA, IJADILIWE MPAKA TUWEKANE SAWA MAANA MFICHA MARADHI KIFO HUMUUMBUA
UKIITOA UTAKUWA HUWATENDEI HAKI RAIA WA TANZANIA WANAOTAKA KUJUA WAGOMBEA URAISI WETU WANALIHANDLE VIPI SUALA SENSITIVE LA UDINI, ILI WAKIAMUA KUPIGA KURA WAJUE KABISA WANAMCHAGUA NANI.
 
"Askofu Kulola, ameyasema hayo jana, katika mahojiano maalum na mwandishi wa habari hii yalifanyika kwa njia ya mtandao wa video mwandishi akiwa Dar es Salaam na Askofu akiwa mjini Mwanza ambako kanisa lake, linafanya maombi maalum ya kuombea amani kwenye uchaguzi mkuu yaliyofanyikia viwanja vya Misungwi mjini Mwanza"

Sina hakika, nahisi kukuona jana Mwanza Airport majira ya saa Tano uki-check in ndege ya saa 5 Mwanza- Dar. Si mkono mmoja unavaa bendeji ya kushikilia mkono?
 
Chagua Dr. Slaa. Rais wa watanzania wote (waislamu, wakristo na wapagani). Rais atakaefyeka mafisadi wote papa na nyangumi na kusomesha watoto wetu bure!!!
Brazaa treni haijazi mafuta shell , atuwezi kuchagua mkenge ,yaani hata kama hatuna budi ,kwa Slaa inabidi tuangalie kwa makini sana ,majuto ni mjukuu ,Slaa hatoweza kabisa kuiweka sawa nchi hii ,na itavurugika katika mida mchache sana .
 

Mchangiaji mwongo mkubwa.

Slaa hajasema Kikwete mdini na kateua waislam wengi.

Katamka hivi:

"Viongozi wa (CCM) wengi ni Waislamu; yeye mwenyewe Kikwete ni Mwislamu; mgombea mwenza wake ni Mwislamu na mwenyekiti wake wa kampeni ni Mwislamu, lakini mimi sijawahi kusema kuwa CCM ina udini. Hata hivyo, katiba ya nchi inasema serikali haina dini... sasa kama mtu anasema mimi nahubiri udini kwa maana hiyo, aseme".

Weka nukuu inayosema Slaa kadai Kikwete ni mdini na kateua Waislam wengi na katoa takwimu.

Mwongo, fidhuli mkubwa.
 
Dr. Slaa ndiye anayetumia UDINI. Anasema kwamba Kikwete kawaweka watu wa din yake, ni tosha huyu jamaa Dr. SLAA HAFAI KUWA RAIS. Kasahau kwamba Nyerere aliwapa kazi watu wa dini yake tu. Mbona asemi Nyerere alikuwa Mdini. SLAA HAFAI KUWA RAIS.
 
,baada ya hapo ofisi za serikali zikawekwa misikiti,wakati serikali haina dini
Kwa hiyo nanyi ndo mnataka Dr. Bunduki akaweke makanisa katika hizo ofisi za serikali, "dhambi ya ubaguzi ni kama kula nyama ya mtu"-hata mwenyewe kajishtukia.
 
Siasa za kidini zinzletwa na losers wa political games. Mimi sioni udini katika mahusiano yangu ya kikazi wala ya kirafiki. Siamini kabisa udini utaniletea lolote ninalotaka klulipata zaidi ya majuto ambaye ni mjukuu. Tuachane wanafiki wanaoeneza siasa za kidini.
 
Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF) Zachary Kakobe, amesema madai ya udini kwenye Uchaguzi Mkuu ujao ni dhana ya kufikirika isiyo na mantiki na inapaswa kupuuzwa na Watanzania wote.

Askofu Kakobe alisema kuzua jambo hilo wakati halipo, ni kosa kubwa linaloweza kutoa mwanya wa kuliumba na kuliingiza vichwani mwa watu bila sababu za msingi.

Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, Askofu Kakobe alieleza kusikitishwa kwake na tetesi za madai kuhusu kuwepo mkakati wa wananchi kupiga kura kwa misingi ya udini Oktoba 31 mwaka huu na kufafanua kuwa jambo hilo ni uzushi na 'linapikwa' kwa makusudi.

"Hili wimbi la maneno ya udini ni dhana ya kufikirika tu, haipo. Inasikitisha tunapoona jambo hili linavaliwa njuga na kusemwa sana wakati huu. Udini usiokuwepo unapotajwatajwa sana, huko ndiko kuupalilia, tunatengeneza kitu kisichokuwepo na kukiingiza vichwani mwa Watanzania, hii ni hatari!" alionya Askofu Kakobe.

Alipuuza propaganda hizo na kueleza kuwa kama kuna udini, mbona mwaka 2000, alipanda jukwaani kumpinga mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Benjamini Mkapa (ambaye ni Mkristo mwenzake)?

Alisema kadhalika mwaka 2005, baadhi ya maaskofu walipoibuka na kudai mmoja wa wagombea ni chaguo la Mungu hakuna aliyedai kuwepo tishio la udini kwenye uchaguzi huo.

"Mwaka 2005 napo wakaibuka baadhi ya maaskofu wakasema mmoja wa wagombea ni chaguo la Mungu, udini haukusemwa, leo hii haya yanatoka wapi? Au wameona kuna mtu fulani hatajwi ndio maana", alisema Askofu Kakobe.

Alitoa mfano wa Kanisa lake kubadili ratiba ya ibada siku ya uchaguzi mwaka huu ambapo badala ya kufanyika Jumapili, itafanyika Jumamosi ili kutoa nafasi kwa waumini kupiga kura. alisema jambo ambalo hilo si udini bali ni kuwapa nafasi waumini hao kutekeleza haki yao ya msingi kwa taifa.

Alisisitiza kwamba jambo hilo si udini hata kidogo na mamlaka husika zilipaswa kumpongeza kwa hatua hiyo ya kuchangia kufanikisha shughuli ya upigaji kura ambayo ni haki ya msingi kikatiba kwa kila raia mwenye sifa.

"Kwa mfano hapa kwangu mimi nimesema ibada zitakuwa Jumamosi badala ya Jumapili ili kuwapa waumini nafasi kushiriki vyema kupiga kura. Mimi nilidhani wangefurahi na kutupongeza kwa kusaidia kufanikisha zoezi hilo. Hapa kwangu wote ni mashahidi, sijamwambia yeyote amchague nani. Kila mtu ana utashi wake. Kumbe basi kila chama kina kura hapa. Wanaopinga mkakati huu wanajua waumini hawa watampigia kura nani? Bila shaka wako watakaowapigia kura Chama tawala, na wako watakaowapigia kura vyama vya Upinzani.", alisema Askofu Kakobe.

Askofu Kakobe alilinganisha sera zinazoendelea kunadiwa majukwaani na bidhaa zinazouzwa madukani na kufafanua kwamba wateja daima huvutwa na kununua bidhaa bora.

"Sera ndizo zinazomuuza mgombea, sera ni sawa na bidhaa sokoni au madukani kama vile shati na gauni. Mtu yeyote wa dini yeyote atavutwa na nguo kutokana na kuridhishwa na ubora wake. Shati bora litanunuliwa na yeyote awe muislamu, mkristo hata mpagani, kudai mtu ananunua kwa misingi ya dini ni dhana potofu ya kufikirika.

"Bidhaa ikiwa nzuri mtu yeyote ataihitaji, hata awe mpagani atainunua tu", alisema Askofu Kakobe na kuzidi kufafanua:

"Kama sera ni nzuri zitanunuliwa na mtu yeyote mwenye dini na asiye na dini. Sera nzuri ni bidhaa inayouzika kwa kila mtu. Ni jukumu la wanasiasa kufafanua sera zao zieleweke kwa wananchi. Hapa hakuna suala la udini.

"Wagombea wajue sera ndizo zinazowauza, unaweza kuuza sera zikakataliwa usitafute visingizio, zitengeneze zikubalike. Kelele zinazopigwa sasa kuhusu udini ni vitu vya kufikirika. Ukizungumza sana kitu hata kama cha uwongo baadaye vitakuwepo, ukitaja sana ukabila, udini ndio unaviumba", alionya.

CHANZO: Majira 25.10.2010
 
CCM hawazoea kushindwa, mwaka huu wanaonja shubiri, wanatapatapa kama mfa maji, kifo cha nyani miti yote inateleza. Hongera Kakobe kwa kuwapiga shule hao CCM ambao tunawasahau rasmi baada ya uchaguzi.
 
You said it all, salute.
 
sitaki kuamini kwamba gazeti hili lilisajiliwa kwa ajili ya kueneza chuki na udini wa hali ya juu kiasi hiki!
Mimi sio mdini,ila kwa kiwango ambacho gazeti hili limefikia linaanza kunifanya niangalie mambo kwa jicho la udini sasa!


  • Mbona linafanya uchochezi na halikemewi?
  • Mbona magazeti mengine ya wakristo hayaenezi upuuzi kiasi hiki?
  • Mbona magazeti kama mwananchi na mwanahalisi wanatishiwa kufungiwa kwa sababu zisizo eleweka na wachochezi kama hawa wanaachiwa wazi wazi?
  • kikwete anaongelea uchochezi gani wa kidini kila siku au halioni gazeti hili?
  • Au kwa serikali ya kikwete uchochezi wa kidini ni pale tu wakristo watakapo ongea chochote hata kama ni cha maana ila waislamu wakitoa tuhuma nzito za mauaji kama hizi hawakemewi?
  • Chuki hizi zimebalikiwa na nani?
  • sina udini,kama gazeti hili lime fanikiwa kinifanya nianze kufikiria masuala ya udini ni watanzania wangapi wamepata sumu hii?
  • Ili tufanye nini baada ya kutupatia sumu hii ya chuki?
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…