Elections 2010 Ni nani aliyeingiza udini kwenye kampeni hizi?

Elections 2010 Ni nani aliyeingiza udini kwenye kampeni hizi?

Status
Not open for further replies.
Mkandara hii issue ya CHADEMA ni tata saana. Si hivyo tu bado wanaonekana wanaimani na serikali ya Kikwete maana wanasema watapeleka matatizo yao. Hivi kama humtambui baba yako, unawezaje kudai matunzo?
Halafu hawa CHADEMA wanapatikana bungeni na huko watakuwa wanahoji utendaji wa serikali. Serikali ipi wakati hawaitambui? Strategy yao bado inapwaya saana.
Kazi kweli kweli..nimekusikia mkuu wangu kwa hiyo mnataka wagome hata kuingia bungeni sio?
Unafikiri CCM watajali wewe mwenyewe umeona CUF wakirukia viti vyao na kucheka sanaaa..
 
Si hivyo tu bado wanaonekana wanaimani na serikali ya Kikwete maana wanasema watapeleka matatizo yao. Hivi kama humtambui baba yako, unawezaje kudai matunzo?
Halafu hawa CHADEMA wanapatikana bungeni na huko watakuwa wanahoji utendaji wa serikali. Serikali ipi wakati hawaitambui? Strategy yao bado inapwaya saana.

Hii strategy kama ingekuwa inapwaya wasingebwaka kama mbwa.
 
Mimi nilichoelewa ni kwa CHADEMA wanamtabua JK kama rais lakini hawautambui mfumo na Muundo mbovu wa NEC uliomuweka Rias na wabunge wote madarakani( CCM CUF, NCRR, etc)

Nilicholewa ni kuwa CHADEMA wamemua kuwasilisha ujumbe wao kwa kufanya migomo kama hii. sabbu hili jambo la tume Huru ya NEC limeombwa kwa njia kiungwana zikashindikana so wanaamua kuweka pressure kidogo.

Nahakika watashiriki shughuli za bunge kikamilifu Na JK ujumbe kaupata hata akiwa mkaidi.


Naunga mkono approach hii kwa mikono na miguu yote
 
Mkuu wangu vipi lakini...Labda mimi sikuelewi unacho maanisha. Kuna watu waliopiga kura za urais kutomchagua Dr.Slaa na leo hawamtambui Dr.Slaa kama rais sasa unataka kusema kwamba hawa watu ambao hawamtambui Dr. Slaa hawakutakiwa kupiga kura toka mwanzo au?

Mkandara,

Logic yako ina mawaa yafuatayo.

Dr. Slaa alikuwa mgombea katika uchaguzi, alikuwa mmoja wa wagombea wengi. Kwa hiyo iliwezekana kabisa kwa watu ambao hawamtambui Dr. Slaa kama rais leo, hawakumtambua huko nyuma pia na wala hawakumuona kama ana uwezo wa kuwa rais, wakampigia Lipumba. Kwa hiyo mfano wako, kwa sababu unahusisha uchaguzi ambao unachagua rais kutoka wawakilishi wa vyama mbalimbali, kwa kupitia watu mbalimbali, hauwezi kufanana na uhakiki wa bunge ambao umeletwa bungeni na mtu mmoja, rais Kikwete.


Narudia
Pendekezo la Pinda lililetwa na mtu mmoja, Kikwete. Alilileta kwa kutumia kofia yake ya urais, kama ilivyosemwa katibani. Kitendo cha wabunge wa CHADEMA kushiriki kupiga kura katika uhakiki huu kilikuwa tayari ni kumtambua Kikwete kama rais.

CHADEMA wangeletewa jina limependekezwa na Matonya, wakaambiwa Matonya hajachaguliwa kuwa rais, lakini kampendekeza Chonya wa Chilonwa kuwa Waziri Mkuu, wangeshiriki kupiga kura kuhakiki pendekezo hili ?

Kama wangeshiriki ni kwa sababu gani ? Kama wasingeshiriki ni kwa sababu gani?
 
Nimefurahi kuona Dr. Slaa anasisitiza kuwa mambo majadiliano yote yaendelee kwa amani. Hii ndivyo inavyotakiwa.
Otherwise swala la kutokumtambua Rais halitekelezeki na ni mbio za sakafuni.
 
Mimi nilichoelewa ni kwa CHADEMA wanamtabua JK kama rais lakini hawautambui mfumo na Muundo mbovu wa NEC uliomuweka Rias na wabunge wote madarakani( CCM CUF, NCRR, etc)

Nilicholewa ni kuwa CHADEMA wamemua kuwasilisha ujumbe wao kwa kufanya migomo kama hii. sabbu hili jambo la tume Huru ya NEC limeombwa kwa njia kiungwana zikashindikana so wanaamua kuweka pressure kidogo.

Nahakika watashiriki shughuli za bunge kikamilifu Na JK ujumbe kaupata hata akiwa mkaidi.


Naunga mkono approach hii kwa mikono na miguu yote

Huwezi kumtambua rais aliyewekwa na NEC na mfumo wetu wa uchaguzi halafu wakati huo huo usiutambue mfumo uliomuweka.

Either huutambui mfumo na rais, ama unatambua mfumo na rais.

Ukisema unamtambua rais lakini huutambui mfumo unasema nini sasa? Kura zimechakachuliwa vibaya vibaya lakini rais halali ? NEC si tume huru lakini rais halali ? CCM imetumia vyombo vya dola kuharibu uchaguzi lakini Kikwete ni rais halali ?

Tusitake kuispin hii, CHADEMA wana half step, wanaharibu maana ya kutomtambua rais.
 
Nimefurahi kuona Dr. Slaa anasisitiza kuwa mambo majadiliano yote yaendelee kwa amani. Hii ndivyo inavyotakiwa.
Otherwise swala la kutokumtambua Rais halitekelezeki na ni mbio za sakafuni.

Tena hasa pale Dr Slaa mwenyewe anaposema kuwa hatumtambui rais huku kwenye maelezo yake yote anatamka rais wa jamhuri, rais wa jamhuri kwa nini asiseme tumeamua kutoka pale Kikwete alipoanza kuhutubia badala ya kusema tumeamua kutoka pale Rais alipoanza kuhutubia. Yaani kuanzia sasa waanze kumtaja muheshiwa aliyebarikiwa na tume ya uchaguzi kuishi IKULU kwa jina lake badala ya cheo ambacho hawakitambui. Yaani ni kama kusema hutambui PhD ya Slaa huku unaendelea kumwita Dr Slaa
 
jamani.. nadhani tunataka kuwa too strict to the point kwamba we become meaning less.. Leo Kikwete nusura amuita Dr. Shein ni makamu wake wa Rais.. as a matter of fact alimalizia kabisa kauli yake. Yawezekana Dr. Slaa hakutakiwa kumtaja kama Rais wa Jamhuri ya Muungano.. lakini maana ya ujumbe wake haiwezi kufutwa na kukosewa kauli au kutamka vibaya. Nadhani kwa kadiri siku zinavyokwenda msimamo wao utakuwa wazi zaidi. The point ni kwamba wao wana tatizo na Kikwete kama Rais aliyetangazwa na tume ya uchaguzi, sidhani kama ni tatizo binafsi na Kikwete mwenyewe.
 
Tena hasa pale Dr Slaa mwenyewe anaposema kuwa hatumtambui rais huku kwenye maelezo yake yote anatamka rais wa jamhuri, rais wa jamhuri kwa nini asiseme tumeamua kutoka pale Kikwete alipoanza kuhutubia badala ya kusema tumeamua kutoka pale Rais alipoanza kuhutubia. Yaani kuanzia sasa waanze kumtaja muheshiwa aliyebarikiwa na tume ya uchaguzi kuishi IKULU kwa jina lake badala ya cheo ambacho hawakitambui. Yaani ni kama kusema hutambui PhD ya Slaa huku unaendelea kumwita Dr Slaa

Nimeiona hii

Ndugu zangu Watanzania, pamoja na ndugu zangu wote waliokuwa wanafuatilia matukio ya bungeni leo. Aaah... ni kweli nimepata watu wengi wakiulizia, aah ni kwanini wabunge wa CHADEMA walitoka ndani ya ukumbi wa bunge, wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano alipoanza kutoa hotuba yake.

Sasa unatuchanganya, unamtambua kama rais au humtambui? Kama humtambui kwa nini unaendelea kumuita rais? Slaa uko serious kweli wewe?

Baada ya kususia hafla ya leo asubuhi , hatua ya pili ilikuwa kususia hotuba ya rais,

Bunge ni mahali ambapo wabunge wana nafasi ya kubeba bendera ya CHADEMA, na mahali pa kwanza pa kuonyesha kwamba hatumtambui rais ni dhahiri basi ni kwamba ni ndani ya bunge. Kitendo cha leo kilianzia asubuhi, kwa wabunge wetu kutohudhuria hafla ya kumuapisha Waziri Mkuu, kwa sababu isingekuwa na maana kwenda kuhudhuria hafla ambayo inasimamiwa na rais ambaye kimsingi hatumtambui, lakini vilevile ni ishara kwa watanzania kwamba bado eenh tunataka maelezo ya kina kutoka serikali kuhusu kauli tulizokwishakuzitoa.

Kwa hiyo jamaa ni rais ila nyie kwa ubishi tu hamumtambui? Au jamaa si rais halali? Kama si rais halali kwa nini unaendelea kumuita rais ?

Huyu Slaa ni PhD kweli ?
 
Mimi nilichoelewa ni kwa CHADEMA wanamtabua JK kama rais lakini hawautambui mfumo na Muundo mbovu wa NEC uliomuweka Rias na wabunge wote madarakani( CCM CUF, NCRR, etc)

Nilicholewa ni kuwa CHADEMA wamemua kuwasilisha ujumbe wao kwa kufanya migomo kama hii. sabbu hili jambo la tume Huru ya NEC limeombwa kwa njia kiungwana zikashindikana so wanaamua kuweka pressure kidogo.

Nahakika watashiriki shughuli za bunge kikamilifu Na JK ujumbe kaupata hata akiwa mkaidi.


Naunga mkono approach hii kwa mikono na miguu yote
Hili ndio tatizo na ndio maana tunasema strategy inapwaya na hawaeleweki wanataka nini! Kifupi hoja kuu ni kutomtambua Rais na ndio maana walivyowaita wanahabari ndicho walicho waeleza.
 
jamani.. nadhani tunataka kuwa too strict to the point kwamba we become meaning less.. Leo Kikwete nusura amuita Dr. Shein ni makamu wake wa Rais.. as a matter of fact alimalizia kabisa kauli yake. Yawezekana Dr. Slaa hakutakiwa kumtaja kama Rais wa Jamhuri ya Muungano.. lakini maana ya ujumbe wake haiwezi kufutwa na kukosewa kauli au kutamka vibaya. Nadhani kwa kadiri siku zinavyokwenda msimamo wao utakuwa wazi zaidi. The point ni kwamba wao wana tatizo na Kikwete kama Rais aliyetangazwa na tume ya uchaguzi, sidhani kama ni tatizo binafsi na Kikwete mwenyewe.

Next time mwambieni Slaa asome a prepared statement, hapo juu kajiadhiri tu, hata Kiswahili hajui.

Kama kitu kingeandikwa na kupata proofreaders watu wangeweza kuona makosa hayo.

Anazidi kuonyesha watu tu kwamba CHADEMA is not ready for prime time.

As much as I don't like CCM, napata tabu kuona mtu asiye makini kama Slaa kuwa rais. Kama mambo yake ndiyo shoddy hivi?

Unaacha wabunge wapigie kura pendekezo la Kikwete kama rais, halafu unataka kuprotest kwenye tafrija, unafikiri tunawezaje kumchukulia seriously hata kama tunataka CCM ifundishwe adabu ?
 
jamani.. nadhani tunataka kuwa too strict to the point kwamba we become meaning less.. Leo Kikwete nusura amuita Dr. Shein ni makamu wake wa Rais.. as a matter of fact alimalizia kabisa kauli yake. Yawezekana Dr. Slaa hakutakiwa kumtaja kama Rais wa Jamhuri ya Muungano.. lakini maana ya ujumbe wake haiwezi kufutwa na kukosewa kauli au kutamka vibaya. Nadhani kwa kadiri siku zinavyokwenda msimamo wao utakuwa wazi zaidi. The point ni kwamba wao wana tatizo na Kikwete kama Rais aliyetangazwa na tume ya uchaguzi, sidhani kama ni tatizo binafsi na Kikwete mwenyewe.
Mwanakijiji unataka tuitazame hii habari kwa juu juu enh! Labda kukufahamisha tu ni kwamba hata ukiassume kwamba Rais ametamkwa kwa bahati mbaya na ukaendelea mbele zaidi kumsikiliza Dr Slaa bado kuna mashaka mengi saana. Kubwa ni kwamba anataka serikali isikilize malalamiko yao. Serikali inayoongozwa na nani? Kiufupi yupo nusunusu, nusu anamtambua kwa ushahidi wa kumuita Rais na kueleza wanaimani serikali itawasikiliza inayoongozwa na Kikwete na nusu nyingine ndiyo wanayotaka wananchi waamini hawamtambui kwa maelezo yake hapo mbele.
 
Next time mwambieni Slaa asome a prepared statement, hapo juu kajiadhiri tu, hata Kiswahili hajui.

Kama kitu kingeandikwa na kupata proofreaders watu wangeweza kuona makosa hayo.

Anazidi kuonyesha watu tu kwamba CHADEMA is not ready for prime time.

As much as I don't like CCM, napata tabu kuona mtu asiye makini kama Slaa kuwa rais. Kama mambo yake ndiyo shoddy hivi?

Unaacha wabunge wapigie kura pendekezo la Kikwete kama rais, halafu unataka kuprotest kwenye tafrija, unafikiri tunawezaje kumchukulia seriously hata kama tunataka CCM ifundishwe adabu ?

Kiranga ile hotuba ya Kikwete iliyopigwa kalenda kujadiliwa bungeni mwaka jana hadi leo hii bado hivi ilikuwaje vile?
 
labda wale wanaounga mkono hatua hii ya kutokumtambua Rais wangetusaidia kujua wao wenzetu wamepata wapi uthibitisho kuwa Rais ameshinda kwa kuiba kura?
Tuliambiwa kuna data zinaandaliwa, ziko wapi?
 
Halafu tuelezane, hao wasiomtambua Rais Kikwete je Rais wao ni nani?
Hili swali nauliza maana naona hii kauli ya Dr. Slaa imeanza kwa wimbo wa taifa!
 
:thinking:

Ujumbe wake Rais mwenye ushindi wa utata, Jakaya Kikwete, kuulani UDINI ndani ya bunge Dodoma hapo jana (Oktoba 18, 2010) uliwaacha watu kibao vinywa wazi kwa dakika kadha huku wakikosa la kusema juu ya wito huu.

Wanaichi wengi ambao wanaamini ya kwamba Ndg Kikwete ndiye mpali miche ya udini nchini kwa sababu ambazo bado hazijabainika vema kwa taifa hili ambalo halikuwahi kufahamu ubaguzi wa aina yoyote hapo nyuma wamedai JK anapoona hutumia mawani ya UDINI, anapoota huota kwa mrengo wa kidini, hupokea ushauri wale anaowaamini kidini tu, na hata anapoteua watu kazi hutumia vipaumbele unaosimama kwenye jiwe la udini.

Mfano raisi zaidi wa madai hayo mazito hapo juu ulidhihirika (Oktober 17, 2010) siku moja tu kabla ya ugeni wake bungeni ambapo kwenye uteuzi wake wa muhimu na kwa awali kabisa wa wabunge maalum nayo pia ikafwaya mkondo huo huo kwa jicho jicho lake kuangaza watu wa dini moja tu kwa mpigo. Walioteuliwa ni pamoja na Ndg Shamsi Vuai Nahodha, Zakia Hamdani Meghji na Prof Makame Mnyaa Mbarawa. Hata hivyo hili halikusumbua wengi sana kwani wamekwishajizoelea kwamba wakuu wa wilaya , mikoa na mashirika mbalimbali ya umma nao lazima wapatikane kwa njia hiyohiyo kama ada.

Kama hiyo haitoshi, mashirika ya madhehebu ya kidini ambayo nazo zilikwemo katika mali binafsi zilizotwaliwa na serikali mwaka wa 1967 baada ya azimio la arusha kuzaliwa. Hivi majuzi baada ya serikali kurejea mfumo wa soko huria, baadhi ya mali binafsi zimepata kurejeshwa mikononi mwao wahusika japo kwa uchache sasa. Madhehebu mbalimbali sana walipokonywa mali zao zikiwemo shule, hospitali, mijengo ya miofisi na hata makazi. Hapa nako gogoro likaelekezwa kivile vile tu!!

Jambo jingine linalotoa wasiwasi mkubwa kwake JK ama ni unafiki na kejeli tu kuhusu swala hili la udini chini mwetu kwa nako pia, pamoja na unyeti wote na ubichi wa kidonda cha kuporwa uchaguzi kwa misingi hiyo hiyo kama ilivyowahi kubashiriwa na mwandishi mmoja mwandamizi Alhaj Y takriban wiki 6 zilizopita, uchaguzi nao ukaporwa kwa misingi hiyo na kuwatisha wananchi kwa kutumia baadha ya kofia za aina hiyo hiyo jeshini na polisi hata wasipige kura.

Kwa upande mwingine wakilainisha chama fulani Machachari sana nacho kikatulia kama barua ndani ya bahasha kwa kuzingatia mwito huo huo wa udini. Leo nako au kesho, nako ndani ya sheria zetu Mahakama ya Kadhi na kujiunga OIC zote zinakuja tupende tusipende nalo kwa mfumo huo huo.

Sasa, tunasema yetu macho .... japokua swali hapa jamvini ni kwamba je JKkweli kaokoka na kilema chake hichi sote tujue tangu alivyozungumza??????????
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom