Elections 2010 Ni nani aliyeingiza udini kwenye kampeni hizi?

Elections 2010 Ni nani aliyeingiza udini kwenye kampeni hizi?

Status
Not open for further replies.
Maaskofu na mashekhe wachapwe viboko hadharanii na kuwapa laana maana hatutaki damu imwagike kwa udini ili kulidhisha kundi fulani la kisiasa. tukumbuke, watu wanaotumia dini au kabila au mkoa kupata maslahi yao kisiasa ni watu waliofilisika kimawazo, na kifikra
 
Matthew:
5:43 "Mmesikia kwamba ilisemwa: `Mpende jirani yako na kumchukia adui yako.`

5:44 Lakini mimi nawaambieni, wapendeni adui zenu na kuwaombea wale wanaowadhulumu ninyi

5:45 ili mpate kuwa watoto wa Baba yenu aliye mbinguni. Kwa maana yeye huwaangazia jua lake watu wabaya na wema, na kuwanyeshea mvua watu wanyofu na waovu.

5:46 Je, mtapata tuzo gani kwa kuwapenda tu wale wanaowapenda ninyi? Hakuna! Kwa maana hata watoza ushuru hufanya hivyo!

5:47 Kama mkiwasalimu ndugu zenu tu, je, mmefanya kitu kisicho cha kawaida? Hata watu wasiomjua Mungu nao hufanya vivyo hivyo.

5:48 Basi, muwe wakamilifu kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.

 
Nilishangazwa sana na hotuba ya rais pale bungeni alipotaja udini kisha hakufafanua zaidi. Hali iliamsha maswali mengi miongoni mwa jamii na sasa tunashuhudia hali ya misimamo ya kidini ikirindima na kushika hatamu kwa kasi ya ajabu.

Sijaona Serikali ikikemea ama kutoa taarifa nyingine zaidi ya ile iliyotolewa siku ile kwenye uzinduzi wa Bunge pale Dodoma.

Hakika ninashawishika kuamini kabisa masuala ya udini yalizinduliwa rasmi pale Bunge na haya tunayoshuhudia sasa ni matokeo ya uzinduzi huo. Taifa linaelekea kubaya na sidhani ikiwa mwaka huu utaisha bila taifa kuingia katika janga kubwa ambalo ni matokeo ya moto huu uliowashwa pale bungeni.

Namtaka JK baada ya kunusa harufu ya udini basi achukue hatua za dhati za kuuzima huo udini kwa kutumia taarifa za kiintelijensia za wachochezi wa kidini na hata hata ikibidi uwajibikaji wa pamoja wa baraza la mawaziri wote wa Kikristo na Kiislam.

Nakuomba rais wangu uchukue hatua.
 
Hilo swala la udini jk ndio aliliazisha dodoma,na hana mtu wa kumlaumu kuhusu hilo,kwasababu yeye andiye mwazilishi basi alimalize yeye mwenyewe.
 
Unaikalia tu politiki, kazi hautafuti, utakula nini?

Na ndio hii iliyotufikisha hapa, maana isngekuwa politics tusingeongea leo masuala ya udini. Politics na njaa ni hatari, lakini Politics na udini ni hatari zaidi na zaidi:hail::fencing::laser::amen:
 
Alipokosa asilimia 80 ya mwaka 2005 akadhani Wakristu wamemtosa na kumpigia Dr Slaa.
Akadhani pia kwamba kumtosa EL kumechangia Wakristo kumtosa.
Akasahau mikashfa yote iliyouandama utawala wake.
Akasahau udini aliouonyesha kwenye teuzi zake.
Akawa haoni afya inavyomnyanyasa hadharani.
Akawa haoni alivyopwaya kwenye nafasi ile.
Akafumbia macho matatizo lukuki ya kiuchumi.
Akaitangaza zaidi familia yake kuliko sera za CCM.
 
Alipokosa asilimia 80 ya mwaka 2005 akadhani Wakristu wamemtosa na kumpigia Dr Slaa.
Akadhani pia kwamba kumtosa EL kumechangia Wakristo kumtosa.
Akasahau mikashfa yote iliyouandama utawala wake.
Akasahau udini aliouonyesha kwenye teuzi zake.
Akawa haoni afya inavyomnyanyasa hadharani.
Akawa haoni alivyopwaya kwenye nafasi ile.
Akafumbia macho matatizo lukuki ya kiuchumi.
Akaitangaza zaidi familia yake kuliko sera za CCM.

Ikiwa mwaka 2005 Watanzania wakiwamo wakristu walimchagua kwa zaidi ya 80% hawakuuona uislam wake? Anatakiwa kujua waTZ wamepima uwezo wake wakaona hawezi kukidhi matarajio yao, wakapunguza kura na kumpa Slaa. Je kwa kufanya hivyo tayari ni udini huo. Mbona yeye alivuta kutoka 75% ya Mkapa kwenda hadi zaidi ya 80% mbona hatukusema udini?

Rais wangu chapa kazi achana na mambo yasiyojenga..Tanzania ya leo, kesho na miaka yote mbeleni inategemea msingi unaoujenga leo.
 
Kuwagawa watu katika makundi ni silaha ya pili kutoka mwisho, lakini hiyo ikishindikana basi matumizi ya nguvu ya dola na kuminya uhuru wa vyombo vya habari na propaganda chafu hufuata.

Lakini mwisho wa yote ni anguko baya la mweleka wa MENDE.

Watanzania, hizi dini zimeletwa tu na watu wa Ulaya na Asia. Tusikubali zikatutenga na kutufanya tusambaratike
 
Nilishangazwa sana na hotuba ya rais pale bungeni alipotaja udini kisha hakufafanua zaidi. Hali iliamsha maswali mengi miongoni mwa jamii na sasa tunashuhudia hali ya misimamo ya kidini ikirindima na kushika hatamu kwa kasi ya ajabu.

Sijaona Serikali ikikemea ama kutoa taarifa nyingine zaidi ya ile iliyotolewa siku ile kwenye uzinduzi wa Bunge pale Dodoma.

Hakika ninashawishika kuamini kabisa masuala ya udini yalizinduliwa rasmi pale Bunge na haya tunayoshuhudia sasa ni matokeo ya uzinduzi huo. Taifa linaelekea kubaya na sidhani ikiwa mwaka huu utaisha bila taifa kuingia katika janga kubwa ambalo ni matokeo ya moto huu uliowashwa pale bungeni.

Namtaka JK baada ya kunusa harufu ya udini basi achukue hatua za dhati za kuuzima huo udini kwa kutumia taarifa za kiintelijensia za wachochezi wa kidini na hata hata ikibidi uwajibikaji wa pamoja wa baraza la mawaziri wote wa Kikristo na Kiislam.

Nakuomba rais wangu uchukue hatua.


Hapo kwenye red umefuta uhalali wa kusaidiwa. Kama rais wako kafanya hivyo basi analo lengo, wewe unatakiwa usubiri amalize then aende tena bungeni kwenu ahitimishe.


 
kikwete alihalalisha udini tangu kipindi chake cha kwanza ndiyomaana alidhamiria kuibeba dini yake ya kiislamu kwa namna yoyote ile ndiyomaana aliweka kwenye ilani ya ccm mamboya kidini ya kiislamu ya mahakama ya kadhi...........rais dhaifu km kikwete ni rahisi kukimbilia defensive mechanism ya udini wakati yeye na waislamu ndiyo waasisi wa haya mambo....na nasikia kikwete amekula yamini na amekula kiapo mbele ya waislamu kuwa lazima atekeleze mahakama ya kadhi na oic la sivyo atasomewa albadri
uislamu ni dini hatari sana kwani palipo na uislamu pana chuki, mafarakano, vurugu, kujitolea mhanga na wivu na uvivu wa kufikiri
 
kikwete alihalalisha udini tangu kipindi chake cha kwanza ndiyomaana alidhamiria kuibeba dini yake ya kiislamu kwa namna yoyote ile ndiyomaana aliweka kwenye ilani ya ccm mamboya kidini ya kiislamu ya mahakama ya kadhi...........rais dhaifu km kikwete ni rahisi kukimbilia defensive mechanism ya udini wakati yeye na waislamu ndiyo waasisi wa haya mambo....na nasikia kikwete amekula yamini na amekula kiapo mbele ya waislamu kuwa lazima atekeleze mahakama ya kadhi na oic la sivyo atasomewa albadri
uislamu ni dini hatari sana kwani palipo na uislamu pana chuki, mafarakano, vurugu, kujitolea mhanga na wivu na uvivu wa kufikiri

Mkuu haujatafuna maneno, lakini kwa wale wasiokuwa na Hekima na Busara hayo uliyosema ni Hakika na kweli, lakini kuna wachache wanaoweza kusimama kama waislam kweli na kazi yao kubwa ni kumtumia Alah. Majority ndio hao uliowataja hapo.
 
kikwete alihalalisha udini tangu kipindi chake cha kwanza ndiyomaana alidhamiria kuibeba dini yake ya kiislamu kwa namna yoyote ile ndiyomaana aliweka kwenye ilani ya ccm mamboya kidini ya kiislamu ya mahakama ya kadhi...........rais dhaifu km kikwete ni rahisi kukimbilia defensive mechanism ya udini wakati yeye na waislamu ndiyo waasisi wa haya mambo....na nasikia kikwete amekula yamini na amekula kiapo mbele ya waislamu kuwa lazima atekeleze mahakama ya kadhi na oic la sivyo atasomewa albadri
uislamu ni dini hatari sana kwani palipo na uislamu pana chuki, mafarakano, vurugu, kujitolea mhanga na wivu na uvivu wa kufikiri

Mimi sio mwislamu na Kikwete ni rais dhaifu sana, lakini kwenye ukweli sintosita kuusema ukweli.
1. Kikwete hakuweka kwenye ilani ya uchaguzi ya ccm swala la mahakama ya kadhi, bali ni Mkapa na watunga sera wenzake ndani ya ccm kwa kipindi kile, kumbuka ilani ya ccm huwa inaandaliwa kabla ya mchakato wa kumpata mgombea urais, mgombea akishapatikana ndio chama kinamkabidhi ilani kwenda kuinadi. sitaki Tanzania ligeuke Taifa la watu wazushi wasofanya utafiti. na swala hili la mahakama ya kadhi alianza kuliahidi Augustino Mrema kwamba akishinda urais atarudisha mahakama ya kadhi, ndio ccm wakaona kumbe ukitaka kura za waislamu kanzu unawaahidi vitu vya kusadikika wanakupigia kura, ndivyo ccm ilivyojiingiza yenyewe mkenge na kuwapiga changa la macho waislamu.
2. kuhusu udini mimi nadhani JK wala hata huo uislamu wala hana habari nao na hana imani ya dini ya kiislamu ila kwa sababu ni rais wa nchi uwa anzuga kwenda msikitini siku za sikukuu ya eid elfitri, kama unaufahamu uislamu una nguzo tano ambazo nguzo moja muhimu ni kwenda kuhiji maka, je JK amewahi kwenda kuhiji maka? ndio maana haitwi alhaji, lakini amekwenda saudi arabia mara nyingi kwa nini haendi maka? fikiria chukuwa hatuwa. udini ni mradi wa watu wa kati, JK hamna analolijuwa
 
Wana JF wenzangu, kama kuna mambo ambayo mkwere hataki kuwaambia ukweli wenzake ni kuhusu hayo wanayoyataka. Kwa mujibu wa dodosa zangu qualifications za full membership wa OIC main ziko 2; moja lazima 70% ya raia wawe wenzao sasa bongo ni 35% hilo limeshindikana; pili viongozi wote wa juu wawe wenzao amejitahidi kuwaweka lakini naona inashindikana sababu ashashtukiwa..... kwa hali hiyo hilo haliwezekani tena awaambie tu ukweli wenzake..... pili kuhusu mahakama yao tatizo si sheria, tatizo si sheria kwani sheria iko wazi kwa taasisi za kidini kuruhusiwa kufanya kazi na hata hiyo mahakama haikufutwa ilikufa yenyewe baada ya kuacha kupewa mgao wa fedha za umma, sasa si waifund wenyewe na iwahukumu wenyewe..... TATIZO HAWAAMBIWI UKWELI!!!
 
Udini ameuanzisha mwenyewe. Na sasa tunaanza kuona athari zake. Hili zigo la Udini atalibeba mwenyewe. :shocked:
 
Heshima kwenu wanajamvi,

Wakuu leo asubuhi nimeamka na tafakari juu ya siasa na muelekeo wake hasa kipindi hiki kilichogubikwa na sakata la Dowans na suala la katiba mpya.

Ukifuatilia mjadala mzima wa masuala haya unabaini serekali na chama tawala haipo kwaajili ya kuwatetea,kuwakilisha,kuboresha maisha ya wananchi wa kawaida.Serekali ya sasa ni kikundi kidogo cha wateule ambao wapo kwaajili ya maslahi yao binafsi na familia zao.

Serekali na chama tawala wanapokosa hoja za kutetea ubadhirifu,ufisadi au maamuzi mabovu wanakimbilia hoja za kugawa wananchi kupitia mdudu udini.Ni ajabu sana mkuu wa nchi anatoa hotuba ndani ya bunge kwamba sasa Tanzania kuna udini pasipo kuchukua hatua madhubuti za kuondoa udini badala yake tunashuhudia chama chake kikiwatumia mashehe kuunga mkono mauaji ya polisi [Maandamano ya Arusha].

Udini Tanzania umeletwa,unakuzwa,unapaliliwa,unatiwa mbolea na kumwagiliwa maji na CCM kwa nia ya kuendelea kubaki madarakani pasipo mwisho.Bahati mbaya wapanga mkakati wengi ndani ya CCM ni watu wenye uwezo mdogo wa kuona mbali wamewekeza kweye siasa za muda mfupi sana.Wapo wanaCCM wenye uwezo mkubwa sana wa kufikiri na kupanga mikakati mizuri kwaajili ya wananchi lakini bahati mbaya CCM ya sasa hawana nafasi na wanachama wa aina hiyo wenye nafasi nzuri ni wanachama wa aina ya Tambwe Hiza na Yusuph Makamba.

Kuthibitisha hoja yangu kwamba CCM wamekuwa wakitumia karata ya udini muda mrefu sana nitaanzia uchaguzi wa mwaka 1995.CCM waliwaamisha watanzania wengi kwamba CUF ni chama cha kiIslam lakini kauli hizo walikuwa wanakwepa kuzitoa kwenye mikoa yenye waIslam wengi kama Lindi,Tanga na pwani.Wakati huo huo walitumia wanazuoni waIslamu kupaka matope mgombea wa NCCR mageuzi A L Mrema kwamba ni adui mkubwa wa waIslam kanda za kaseti zitisambazwa kwenye misikiti na vijiwe vya kahawa bila kizuizi chochote.CCM walikuwa wakichekelea sana dhambi hiyo kwakuwa ilikuwa inawanufaisha na kuwahakikishia ushindi.Sheckh wa mkoa wa Arusha Bwana Kisiwa alijengewa nyumba maeneo ya Njiro na mheshimiwa B Mkapa kwa kufanisha zoezi la kutawanya kanda kwenye misikiti yote ikiwa ni pamoja na kutoa mihadhara ya kumbomoa A L Mrema.

Mwaka 2005 CCM waliweka ndani ya ilani yake kipengele cha kuanzisha mahakama ya Kadhi kama wananchi wangewapa ridhaa ya kuongoza tena.CCM si wajinga walijua wangeanzisha mahakama ya kadhi wangekuwa wanavunja katiba ya JMT walichokuwa wanahitaji ni kurejea magogoni kwa gharama yoyote.

Mwaka 2010 mgombea wa CHADEMA Dr W Slaa alikuwa tishio kwa mgombea dhaifu wa CCM mheshimiwa Jakaya Kikwete amaye alikuwa ameshindwa kusimamia vyema rasilimali za watanzania na vita ya ufisadi.Karata ya udini ikaanzishwa tena kwamba Dr W Slaa ni mkatoliki wakasahau Nyerere pia alikuwa mkatoliki.Wakajitahidi sana kuwasahaulisha watanzania sifa za Dr W Slaa dhidi ya ufisadi wapo watanzania wajinga walioingia kwenye kundi hili siwezi kuwalaumu kwasababu sifa kubwa ya mtanzania ni kusahau haraka.Bahati nzuri wapo watanzania zaidi ya milioni mbili waliokataa usungura wa CCM.

Mwaka huu wa 2011 maandamano ya Arusha CCM walijitahidi sana kuyageuza na kuyapa sura ya udini bahati mbaya kama nilivyotangulia kusema awali CCM hawana wana mkakati wenye akili sawa sawa.Mpaka mwaka huu umalizike tutashudia wenyewe mikakati ya kutupachikia udini zikiendelezwa kwa juhudi kubwa kwakuwa watawala wetu hawana tena majibu ya matatizo yetu.Usishangae maandamano ya wanafunzi wa vyuo vikuu yakahusushwa na udini !.

Matatizo ya watanzania si udini viongozi wanaokimbilia hoja za udini hawana sifa za kuongoza.Shida za wananchi ni maradhi,ujinga na umaskini viongozi waonyeshe njia sahihi za kukabiliana nayo.Athari za kuporomoka kwa shilingi y kitanzania kunawaumiza waIlsam na waKristo,upanda holela wa bei ya umeme hakuchagui kama wewe ni mkristo au muIslam wote tutaumia sana tusikubali kutumiwa.
 
thanx bro. But revisit the true history of tz u will realise the truth of the origin of the udin.
 
Heshima kwenu wanajamvi,

Wakuu leo asubuhi nimeamka na tafakari juu ya siasa na muelekeo wake hasa kipindi hiki kilichogubikwa na sakata la Dowans na suala la katiba mpya.

Ukifuatilia mjadala mzima wa masuala haya unabaini serekali na chama tawala haipo kwaajili ya kuwatetea,kuwakilisha,kuboresha maisha ya wananchi wa kawaida.Serekali ya sasa ni kikundi kidogo cha wateule ambao wapo kwaajili ya maslahi yao binafsi na familia zao.

Serekali na chama tawala wanapokosa hoja za kutetea ubadhirifu,ufisadi au maamuzi mabovu wanakimbilia hoja za kugawa wananchi kupitia mdudu udini.Ni ajabu sana mkuu wa nchi anatoa hotuba ndani ya bunge kwamba sasa Tanzania kuna udini pasipo kuchukua hatua madhubuti za kuondoa udini badala yake tunashuhudia chama chake kikiwatumia mashehe kuunga mkono mauaji ya polisi [Maandamano ya Arusha].

Udini Tanzania umeletwa,unakuzwa,unapaliliwa,unatiwa mbolea na kumwagiliwa maji na CCM kwa nia ya kuendelea kubaki madarakani pasipo mwisho.Bahati mbaya wapanga mkakati wengi ndani ya CCM ni watu wenye uwezo mdogo wa kuona mbali wamewekeza kweye siasa za muda mfupi sana.Wapo wanaCCM wenye uwezo mkubwa sana wa kufikiri na kupanga mikakati mizuri kwaajili ya wananchi lakini bahati mbaya CCM ya sasa hawana nafasi na wanachama wa aina hiyo wenye nafasi nzuri ni wanachama wa aina ya Tambwe Hiza na Yusuph Makamba.

Kuthibitisha hoja yangu kwamba CCM wamekuwa wakitumia karata ya udini muda mrefu sana nitaanzia uchaguzi wa mwaka 1995.CCM waliwaamisha watanzania wengi kwamba CUF ni chama cha kiIslam lakini kauli hizo walikuwa wanakwepa kuzitoa kwenye mikoa yenye waIslam wengi kama Lindi,Tanga na pwani.Wakati huo huo walitumia wanazuoni waIslamu kupaka matope mgombea wa NCCR mageuzi A L Mrema kwamba ni adui mkubwa wa waIslam kanda za kaseti zitisambazwa kwenye misikiti na vijiwe vya kahawa bila kizuizi chochote.CCM walikuwa wakichekelea sana dhambi hiyo kwakuwa ilikuwa inawanufaisha na kuwahakikishia ushindi.Sheckh wa mkoa wa Arusha Bwana Kisiwa alijengewa nyumba maeneo ya Njiro na mheshimiwa B Mkapa kwa kufanisha zoezi la kutawanya kanda kwenye misikiti yote ikiwa ni pamoja na kutoa mihadhara ya kumbomoa A L Mrema.

Mwaka 2005 CCM waliweka ndani ya ilani yake kipengele cha kuanzisha mahakama ya Kadhi kama wananchi wangewapa ridhaa ya kuongoza tena.CCM si wajinga walijua wangeanzisha mahakama ya kadhi wangekuwa wanavunja katiba ya JMT walichokuwa wanahitaji ni kurejea magogoni kwa gharama yoyote.

Mwaka 2010 mgombea wa CHADEMA Dr W Slaa alikuwa tishio kwa mgombea dhaifu wa CCM mheshimiwa Jakaya Kikwete amaye alikuwa ameshindwa kusimamia vyema rasilimali za watanzania na vita ya ufisadi.Karata ya udini ikaanzishwa tena kwamba Dr W Slaa ni mkatoliki wakasahau Nyerere pia alikuwa mkatoliki.Wakajitahidi sana kuwasahaulisha watanzania sifa za Dr W Slaa dhidi ya ufisadi wapo watanzania wajinga walioingia kwenye kundi hili siwezi kuwalaumu kwasababu sifa kubwa ya mtanzania ni kusahau haraka.Bahati nzuri wapo watanzania zaidi ya milioni mbili waliokataa usungura wa CCM.

Mwaka huu wa 2011 maandamano ya Arusha CCM walijitahidi sana kuyageuza na kuyapa sura ya udini bahati mbaya kama nilivyotangulia kusema awali CCM hawana wana mkakati wenye akili sawa sawa.Mpaka mwaka huu umalizike tutashudia wenyewe mikakati ya kutupachikia udini zikiendelezwa kwa juhudi kubwa kwakuwa watawala wetu hawana tena majibu ya matatizo yetu.Usishangae maandamano ya wanafunzi wa vyuo vikuu yakahusushwa na udini !.

Matatizo ya watanzania si udini viongozi wanaokimbilia hoja za udini hawana sifa za kuongoza.Shida za wananchi ni maradhi,ujinga na umaskini viongozi waonyeshe njia sahihi za kukabiliana nayo.Athari za kuporomoka kwa shilingi y kitanzania kunawaumiza waIlsam na waKristo,upanda holela wa bei ya umeme hakuchagui kama wewe ni mkristo au muIslam wote tutaumia sana tusikubali kutumiwa.

Waasisi wa udini ni wanasiasa lakini wakristo na waislam hawana matatizo ndo maana wanakaribishana katika uislam na ukristo kama unavyoweza kumsikiliza mchungaji Adam Haji Mohamed: YouTube - Waislamu twendeni kwa Yesu -Testimony 13
 
Ni yale yale yanarudiwa! tafuta topic mpya, hii imeshapitwa na wakati!!!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom