Ni nani hasa huitumia ndege ya Rais wetu 5H- ONE Gulfstream G550 maana inaonekana ikizurula tu mikoani na kupaki Zanzibar?

Safari ndefu hivi karibuni ni kwenda na kurudi Ethopia chini ya Makamu wa Rais
 
Kuna wakati imeonekana juzi kati huko Chato ikimpeleka mkuu mmoja wa benki inayojihusisha na maendeleo ya Afrika.

Mkuu huyo alikiri kupewa usafiri na mkuu wa nchi, hii ina maana gani? ....

Kulipa fadhira? Kulipa deni? Hongo.....au ni ukarimu kwenye mali ya umma😳
 
Bi Mikopo haziamini ndege za Tanzania, ndiyo maana haipandi hiko kitu chenu.
 
Mpaka mmeanza kutrack na ndege ya Rais wa JMT? Hii nchi sasa imekuwa ngumu kuliko ugumu wenyewe!
Ila umenikumbusha mambo yale ya zamani. Unakuta " Hili ni eneo maalum. Usipige picha hapa!". Au "Hakuna ruhusa kupiga picha!" Mambo hayo yamepitwa na wakati katika kipindi hiki. Huko juu kuna satellite kibao zinachukua picha za kila kitu ambacho hapa chini mnajidai kwamba hakuna kupiga picha.

Huwezi kuficha chochote ukidhani watu hawatafahamu. Karibu kila kitu kipo wazi kwa walimwengu.
 
Sasa ndiyo mtrack hadi pipa la Rais wetu? Hamjui mnahatarisha usalama wake? Sheria hamzijui? Kesi za ugaidi mnazijua?

NB: Acheni Bi Mikopo achape kazi (ya kuendelea kukopa!) Tutalipa siye wanyonge!
 
Makosa yaliyofanywa na CCM 2015, yatalitafuna hili Taifa kwa miaka mingi sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…