Ni nchi gani Afrika watanzania wakienda wanapokelewa kiurafiki?

Ni nchi gani Afrika watanzania wakienda wanapokelewa kiurafiki?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
21,470
Reaction score
40,593
Mchango wa Tanzania kwa mambo mbali mbali ya kimaendeleo kijamii ni mkubwa sana Afrika

Na Tanzania ni nchi ambayo inawezekana inaongoza kuwapokea raia wa nchi nyingine za Afrika bila ya kuwafanyia Bugudha.

Kwa wale wenye uzowefu wa kutembelea nchi nyingine za Afrika. Ni nchi gani Afrika ambako watanzania hupokelewa kiurafiki?

Ni wapi katika Afrika mtanzania akifika hujisikia kama yupo nyumbani Tanzania?
 
Mchango wa Tanzania kwa mambo mbali mbali ya kimaendeleo kijamii ni mkubwa sana Afrika

Na Tanzania ni nchi ambayo inawezekana inaongoza kuwapokea raia wa nchi nyingine za Afrika bila ya kuwafanyia Bugudha.

Kwa wale wenye uzowefu wa kutembelea nchi nyingine za Afrika. Ni nchi gani Afrika ambako watanzania hupokelewa kiurafiki?

Ni wapi katika Afrika mtanzania akifika hujisikia kama yupo nyumbani Tanzania?
Mkuu mleta mada ikitoa Tanzania nchi gani una uzoefu nao? yaani ulisha kaa kwa mda
 
Kenya ndio nchi ambayo tunafanana nao kwa mengi. Nadhani kuna Watanzania

wengi zaidi Kenya kuliko nchi nyingine yeyote.
 
Kenya kuna omba omba wengi sana watz. Kenya ni kama ndugu wa tumbo moja. Mikwaruzano mingi lakini bado hamuwezi kutupana.
 
1. Kenya 🇰🇪
2. Uganda 🇺🇬
3. Rwanda 🇷🇼
4. Mozambique 🇲🇿
5. DRC
6. Burundi 🇧🇮
7. South Africa 🇿🇦

Hapo ni baadhi ya nchi mbongo anaishi kama yupo hom mbagala bila shida yoyote. Msumbiji nilikuta wabongo ndo wafanyabiashara wakubwa wa maduka, Rwanda nilikuta masai kibao wanafanya umachinga ila wakanambia wanalazimishwa wafungue maduka wakae sehemu moja walipe kodi ya nchi
 
Masikini hapendwi
Wasipokee matajiri wa kizungu wapokee Watanzania na matatizo yao
 
Kenya .
Pamoja na kwamba kwenye mitandao sometimes tunacharuana🤣 lakini niliikaa 4yrs kama nipo home tu.
 
Back
Top Bottom