Ni nchi gani yenye mipango miji mibovu zaidi ya Tanzania?

Ni nchi gani yenye mipango miji mibovu zaidi ya Tanzania?

Hio nchi masikini yenye mipango mizuri ni ipi?
IMG_20210518_120132.jpg
 
hizo nchi umeshawahi hata kupita kwenye anga lake ukaona makorokocho yaliyoko hapo?
 
Dah umenikumbusha juzi nimepita Babati Mjini yani watu wamejenga juu ya mlima wanahatibu kabisa uoto wa mlima ule mzuri unatoa ukingu.
 
Mji wetu pendwa huu nenda kaulize bei za nyumba sasa ndio utajua kachumbali ni mboga sasa hapo ngoja mvua inyesha ni hatari tu.
Screenshot_20210520-094257_Maps.jpg
Screenshot_20210520-094347_Maps.jpg
Screenshot_20210520-094541_Maps.jpg
 
Hta hapo Same
Dah umenikumbusha juzi nimepita Babati Mjini yani watu wamejenga juu ya mlima wanahatibu kabisa uoto wa mlima ule mzuri unatoa ukingu.
Watu wanajenga milimani na serikali inaona haichukui hatua na maeneo tambarare yapo hayapimwi wagawiwe viwanja. Inashangaza sana
 
Naona Katibu Mkuu wa CCM ameanza kulifanyia kazi suala la ardhi. Hii imeriporiwa na gazeti la Mwananchi la Leo

Agizo la CCM kwa Wizara ya Ardhi

THURSDAY MAY 20 2021

Dar es Salaam. Katibu mkuu wa CCM, Daniel Chongolo ameitaka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuongeza kasi ya utatuzi wa migogoro ya ardhi inayosababisha malalamiko kwa wananchi.

Ameyasema hayo leo Alhamisi Mei 20, 2021 katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dodoma huku akirejea ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/25 inayoeleza kasi ya umilikishaji wa ardhi kwa wananchi.

"Hatua hii itawafanya wananchi wawe na usalama zaidi wa maeneo yao na ni muhimu. CCM italifuatilia kwa karibu kuona utekelezaji wake," amesema Chongolo.

Amesema kwa sasa ni wananchi wachache wanaomiliki ardhi kisheria, huku asilimia kubwa wakimiliki kiasili au bila utaratibu wa kisheria, ambapo mtu ananunua ardhi na kujenga nyumba ya thamani kuwa na umiliki halali wa kiwanja hicho.

Aidha, Chongolo amesema chama hicho kinaelekeza kufanyika kwa uthaminishaji na fidia kwa wananchi waliotwaliwa maeneo yao kwa shughuli za umma pamoja na uimarishwaji wa mfuko wa fidia.

"Viongozi wote wa Serikali kuanzia ngazi za vijiji na mitaa mpaka wizara wanapaswa kuhakikisha wanatatua na kuandaa siku mahsusi za kutatua migogoro ya ardhi kwa haraka na wakati.”


"Chama kinaelekeza kumaliza migogoro ya ardhi katika Wilaya za Kondoa, Kitero, Kongwa, Morogoro, Kilombero na pembezoni mwa hifadhi mbalimbali ambayo imekuwepo kwa muda mrefu na kuwasumbua wananchi," amesema.
 
Naona Katibu Mkuu wa CCM ameanza kulifanyia kazi suala la ardhi. Hii imeriporiwa na gazeti la Mwananchi la Leo

Agizo la CCM kwa Wizara ya Ardhi

THURSDAY MAY 20 2021

Dar es Salaam. Katibu mkuu wa CCM, Daniel Chongolo ameitaka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuongeza kasi ya utatuzi wa migogoro ya ardhi inayosababisha malalamiko kwa wananchi.

Ameyasema hayo leo Alhamisi Mei 20, 2021 katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dodoma huku akirejea ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/25 inayoeleza kasi ya umilikishaji wa ardhi kwa wananchi.

"Hatua hii itawafanya wananchi wawe na usalama zaidi wa maeneo yao na ni muhimu. CCM italifuatilia kwa karibu kuona utekelezaji wake," amesema Chongolo.

Amesema kwa sasa ni wananchi wachache wanaomiliki ardhi kisheria, huku asilimia kubwa wakimiliki kiasili au bila utaratibu wa kisheria, ambapo mtu ananunua ardhi na kujenga nyumba ya thamani kuwa na umiliki halali wa kiwanja hicho.

Aidha, Chongolo amesema chama hicho kinaelekeza kufanyika kwa uthaminishaji na fidia kwa wananchi waliotwaliwa maeneo yao kwa shughuli za umma pamoja na uimarishwaji wa mfuko wa fidia.

"Viongozi wote wa Serikali kuanzia ngazi za vijiji na mitaa mpaka wizara wanapaswa kuhakikisha wanatatua na kuandaa siku mahsusi za kutatua migogoro ya ardhi kwa haraka na wakati.”


"Chama kinaelekeza kumaliza migogoro ya ardhi katika Wilaya za Kondoa, Kitero, Kongwa, Morogoro, Kilombero na pembezoni mwa hifadhi mbalimbali ambayo imekuwepo kwa muda mrefu na kuwasumbua wananchi," amesema.
Huyo kazungumzia migogoro hakuna mpango wa kupima wala nini
 
Back
Top Bottom