Ni rahisi kwa Mzazi wa Kiafrika kukutukana kuliko kukwambia 'Nakupenda Mwanangu'

Ni rahisi kwa Mzazi wa Kiafrika kukutukana kuliko kukwambia 'Nakupenda Mwanangu'

Matendo mengi sana ya Mzazi wa ki Africa yanawakilisha Upendo, hata kama hasemi.

UZUNGU mnaouona kwenye tamthiliya, mnadanganyana nao tu, hakuna watu wa hovyo kama hao.

Wazazi walipe ada, wakupe chakula, wakupe mavazi na maitaji, Huo ndo Upendo, hata kama hawasemi.

Majukumu na wajibu wa mzazi ndio unaita Upendo?
 
Hakuna anayepuuza utamaduni, ila kuna mengine lazima yaachwe, hiki tuu kifaa tunachotumia wewe na mie wametengeza hao hao tunawagawia malighafi kisha wanatuletea simu, sie kukenua tu.

Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
Mbona wachina hawadekezwi kama wazungu lakini wapo vizuri kitechnolojia na kimaendeleo. Malezi ya mzazi wa kichina hayana tofauti na mzazi wa kiafrika. Kiufupi Asia na Africa tamaduni zinafanana. Kudekezwa sio kuwa na akili
 
Okay. Wazazi wa Ki Africa hawapendi watoto wao, Wazungu ndo wanapenda watoto wao.

Hayo ni maneno yako.
Mimi nilikuwa nakuweka Sawa tuu kuwa kuwalea watoto wako ni wajibu na Majukumu yako. Hazihusiani na Upendo.
Upendo ni zaidi ya hayo uliyoyataja
 
Mie nimewaambia mpaka nimechoka sasa...naona wanavimba vichwa tu🙄
 
Hayo ni maneno yako.
Mimi nilikuwa nakuweka Sawa tuu kuwa kuwalea watoto wako ni wajibu na Majukumu yako. Hazihusiani na Upendo.
Upendo ni zaidi ya hayo uliyoyataja

Okay Kaka! Kusema ukweli sina kumbukumbu nimewahi waambia na kutamkia wanangu kuwa na wapenda.

Ila hata ndugu, huwa wanawaambia mna Baba mzuri sana anawapenda, na wao wanakiri hayo kwa kusema, I dont know how and why, bu haiji tu.
 
Mzazi wa africa kimaneno yupo tofauti na moyoni , apo unakuta moyoni anakupenda sna .
 
Okay Kaka! Kusema ukweli sina kumbukumbu nimewahi waambia na kutamkia wanangu kuwa na wapenda.

Ila hata ndugu, huwa wanawaambia mna Baba mzuri sana anawapenda, na wao wanakiri hayo kwa kusema, I dont know how and why, bu haiji tu.

Upo sahihi Kabisa.
Kuna upendo wa Matendo na upendo wa maneno.
Mtoto anaweza akajua unampenda Kwa kuona mambo hayo mawili. Matendo na maneno yako.

Epuka kuonyesha Huduma unazowapa Watoto au MKE kama sehemu ya Upendo, hiyo ni big mistake.
Na epuka kusema kwa mdomo Kuwa unawapenda Watoto kuliko wao wanavyoona.

Hata hivyo Haivutii wala kupendeza Kwa Baba kumwambia "NAKUPENDA"mtoto wake wakiume (kijana). Upendo wa Baba Kwa mtoto utahusu kauli za kumtia moyo Kwa mfano, Kijana wangu wewe unaakili Sana, au ingawaje umekosea lakini ukitulia Kwa wakati mwingine utafanya vizuri zaidi; nakuamini kijana wangu,
Kauli za ujasiri, kama Wewe ni jembe, wewe ni dume la Simba, unatakiwa uwe na maamuzi magumu yenye tija, usiogope bali uwe na tahadhari,
Pamoja na kumnenea maneno mazuri.
Hayo ndio maneno ya upendo, hata usipomwambia nakupenda.

Mtoto wakike, kuambiwa na Baba yake Nakupenda Binti yangu ni Haki yake, Upendo ni Haki ya wanawake, heshima ni Haki ya wanaume. Ingawaje wote Kwa kiasi Fulani huweza kupewa upendo na heshima.

Anachosema Mtoa mada ni zile pigo za kuisakama Saikolojia ya mtoto Kwa kumtolea maneno ya shombo ATI Huko ndio kumfanya awe shujaa wakati ni kumharibu kisaikolojia.
 
Upo sahihi Kabisa.
Kuna upendo wa Matendo na upendo wa maneno.
Mtoto anaweza akajua unampenda Kwa kuona mambo hayo mawili. Matendo na maneno yako.

Epuka kuonyesha Huduma unazowapa Watoto au MKE kama sehemu ya Upendo, hiyo ni big mistake.
Na epuka kusema kwa mdomo Kuwa unawapenda Watoto kuliko wao wanavyoona.

Hata hivyo Haivutii wala kupendeza Kwa Baba kumwambia "NAKUPENDA"mtoto wake wakiume (kijana). Upendo wa Baba Kwa mtoto utahusu kauli za kumtia moyo Kwa mfano, Kijana wangu wewe unaakili Sana, au ingawaje umekosea lakini ukitulia Kwa wakati mwingine utafanya vizuri zaidi; nakuamini kijana wangu,
Kauli za ujasiri, kama Wewe ni jembe, wewe ni dume la Simba, unatakiwa uwe na maamuzi magumu yenye tija, usiogope bali uwe na tahadhari,
Pamoja na kumnenea maneno mazuri.
Hayo ndio maneno ya upendo, hata usipomwambia nakupenda.

Mtoto wakike, kuambiwa na Baba yake Nakupenda Binti yangu ni Haki yake, Upendo ni Haki ya wanawake, heshima ni Haki ya wanaume. Ingawaje wote Kwa kiasi Fulani huweza kupewa upendo na heshima.

Anachosema Mtoa mada ni zile pigo za kuisakama Saikolojia ya mtoto Kwa kumtolea maneno ya shombo ATI Huko ndio kumfanya awe shujaa wakati ni kumharibu kisaikolojia.

Kabisa, najua wajibu wangu, ila protection, care, kuwauliza concerns, protections, ila kusema neno Nakupenda, sijui naanza kwa mtoto, kwangu ngumu, it is a heavy work, may be in English
 
Back
Top Bottom