Ni rasmi sasa kwa watu wa mkoa wa Kigoma ni rukra kuvaa chapa (logo) ya JWTZ

Kigoma Region Tanzania

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2021
Posts
230
Reaction score
611
Ni marufuku kuvaa nguo ya jeshi kama wewe sio mwanajeshi, lakini kwa heshima yako wewe mwana Kigoma, kwa heshima ya mashabiki wa Mashujaa Football Club, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania (JWTZ) Jenerali Jacob John Mkunda kakupa uhuru sasa utavaa Logo ya JWTZ kifuani kwako.

Hii ni heshima kubwa kwako mwanakigoma, sasa ni wakati wakuvaa kilicho bora.
Logo ya 'umoja' ya ''Tanzania People's Defence Force'' itakua kifuani kwako kuanzia Tarehe 10/8/2023, siku ya Alhamis.

Hizi ndio jezi rasmi za Watanganyika kwa msimu wa mwaka 2023-2024
Utaratibu wa kupatikana kwake na Maduka yatakayouza jezi zetu yatatangazwa kabla ya siku husika.

Jezi zitapatikana Nchi nzima kwa bei rafiki, hii ndio Mashujaa Football Club

Je utapenda kuvalia nyeupe?



...............


Au utavalia mawese?


,,,,,,,,,,,,,,


Au utavalia rangi ya Ziwa Tanganyika?


................


Karibuni Kigoma, karibuni Magharibi mwa Tanzania, Karibuni Tanganyika
 
Hiyo ya blue sana ingawaje mimi siyo shaabiki wa kabumbu,nasiri soccer lianze kwetu ki soccer.
 
Jezi ya blue ipo vizuri ila......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…