Ni sahihi kupigwa na Mwenzi hata kama umekosea?

Ni sahihi kupigwa na Mwenzi hata kama umekosea?

Tlaatlaah

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2023
Posts
24,665
Reaction score
25,388
Kupigwa makwenzi, makofi, ngwara, ngumi au mateke na mwenzi wako wa kike, hadharani au faragha ni sahihi hata kama umekosea?

Jamaa, jirani mwenye ndoa yake mtaani, na ana nafasi kubwa tu miongoni mwa mashirika ya kutoa huduma za kifedha mjini, ameamua kwenda kuripoti kwa mjumbe baada ya kuchoshwa na kipigo cha makwenzi, makofi, ngumi na mateke vya mara kwa mara kutoka kwa mkewe. Lakini kama haitoshi, akuamua pia kwenda kuripoti polisi kwa msisitizo na msaada zaidi.

Hii imekuja baada ya muungwana huyu kushindwa kuvumilia hali hiyo inayojirudia mara kwa mara kutoka kwa mkewe, na kuamua kuvunja ukimya na kutafuta usaidizi huko alikoenda kuripoti..

Jamaa atasaidika au atafedhehheka kwenye jamii?

Kama mwanaume kamili, unadhani jamaa amekosea ama yuko sahihi?

Na je, unadhani hali hiyo itaimarisha na kuchochea afya na uhai wa ndoa yao, au itadhoofisha na pengine kusambaratisha kabisa ndoa yenyewe?

Nani wa kulaumiwa baina yao..
NDOA SI LELEMAMA NDRUGO ZANGO, YAHITAJI HEKIMA, UVUMILIVU, USTAHIMILIVU NA SUBRA YA KIPEKEE SANA.
 
Kabla ya kuzingatia uanaume wake nadhani jamaa yuko sahihi kwenda kwenye vyombo vya sheria. Kwa sababu huwezi jua pengine jamaa angeamua kupanic na kuanza kumpiga yeye yangetokea yapi! Kuhusu mustakabali wa ndoa hiyo ni juu ya wao wenyewe na mapokeo baada ya hatua za k8sheria.

Kwangu binafsi siwezi kwenda polisi kuripoti huo upuuzi kwa sababu hatuwezi kufika hatua hiyo ya mwanamke kunipiga mimi. Nadhani ni yeye ndio ataanza kutafuta usuluishi kwa wazazi. Kuna mambo wanaume tunayatengeneza wenyewe na hatujui namna ya kusuluhisha. Ni upuuzi eti umeoa halafu unapigwa makofi, mibanzi shenzi kabisa
 
Jamaa ndie mwenye maamuzi ya kutoa talaka fasta. Kama kaenda kulalamika ni sahihi kabisa ila sasa sio kaenda kushitaki akitumaini itamrekebisha mkewe ili waendelee na ndoa yao hilo ni kosa atakalolijutia sana.
 
Kuna baadhi ya Wanawake wameumbwa ni wababe tu kama ilivyo baadhi ya Wanaume wenzetu kuwa wababe Kwa wake zao🙌

Kuna askari mmoja wa jwtz, jirani yetu alikuwa akipigwa sana na Mkewe (Mbabe) mara kwa mara

Kutokea hapo nilijiapizaga nikija Kuoa Mwanamke mnene Mimi, labda sio Grahams Mimi 🤗🙌

Maana jamaa Mkewe alikuwa mnene kaenda hewani halafu ndiyo Mbabe 🙌
 
Mnyanyasaji hana jinsia. Aweza kuwa mwanamke au mwanamme. Alipoti polisi , kikubwa zaidi afanye mchakato wa kuvunja hiyo ndoa .
Wananwake wananyanyasa sana wanaume siku hizi mbaya zaidi vijana wananyanyasika wakiwa wadogo.sijuwi wakifika uzeeni itakuwaje shida mwanaume akirevange majibu matatu ategemee kifo, jela au ulemavu wa kudumu.
 
Kuna baadhi ya Wanawake wameumbwa ni wababe tu kama ilivyo baadhi ya Wanaume wenzetu kuwa wababe Kwa wake zao🙌

Kuna askari mmoja wa jwtz, jirani yetu alikuwa akipigwa sana na Mkewe (Mbabe) mara kwa mara

Kutokea hapo nilijiapizaga nikija Kuoa Mwanamke mnene Mimi, labda sio Grahams Mimi 🤗🙌

Maana jamaa Mkewe alikuwa mnene kaenda hewani halafu ndiyo Mbabe 🙌
Wanawake wanene wengi wanajua kupiga miili inawabeba.
 
kupigwa makwenzi, makofi, ngwara, ngumi au mateke na mwenzi wako wa kike, hadharani au faragha ni sahihi hata kama umekosea?

Jamaa, jirani mwenye ndoa yake mtaani, na ana nafasi kubwa tu miongoni mwa mashirika ya kutoa huduma za kifedha mjini, ameamua kwenda kuripoti kwa mjumbe baada ya kuchoshwa na kipigo cha makwenzi, makofi, ngumi na mateke vya mara kwa mara kutoka kwa mkewe. Lakini kama haitoshi, akuamua pia kwenda kuripoti polisi kwa msisitizo na msaada zaidi.

hii imekuja baada ya muungwana huyu kushindwa kuvumilia hali hiyo inayojirudia mara kwa mara kutoka kwa mkewe, na kuamua kuvunja ukimya na kutafuta usaidizi huko alikoenda kuripoti..

Jamaa atasaidika au atafedhehheka kwenye jamii?

kama mwanaume kamili, unadhani jamaa amekosea ama yuko sahihi?

na je, unadhani hali hiyo itaimarisha na kuchochea afya na uhai wa ndoa yao, au itadhoofisha na pengine kusambaratisha kabisa ndoa yenyewe?

nani wa kulaumiwa baina yao..
NDOA SI LELEMAMA NDRUGO ZANGO, YAHITAJI HEKIMA, UVUMILIVU, USTAHIMILIVU NA SUBRA YA KIPEKEE SANA 🐒
Hapo Muhimu zaidi ni kupigwa Ngwara, Ngwara linatoa wenge mapema kuliko makwenzi

Sijui kama umenipata vizuri
 
Back
Top Bottom