Nashukuru kwa kunipatia elimu maana elimu haina mwisho.
Ubarikiwe sanaYajue makosa yaliyoainishwa kupitia Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015
SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO, Sheria ya makosa ya mtandao imetungwa 2015, Sheria hii inahusu makosa yanayohusiana na mifumo ya kompyuta na teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA); na uchunguzi, ukusanyaji na matumizi ya ushahidi wa kielektroniki na unaohusiana na hayo. Vipengele muhimu na...www.jamiiforums.com
Soma sehemu inayoonesha mamlaka ya polisi
Kichwa habari unasema umma, habari ndani inasema mahakama. Kifupi suala likishaitwa la kiuchunguzi halina mipaka tena hasa kwa sheria zetu.Nimesikia jana kuwa kampuni moja ya simu imetoa mawasiliano ya Sabaya mahakamani.
Je, hili linatoa taswira gani kwa wateja wake?
Binafsi siijui sheria hivyo nawaomba wenye uelewa tujulishane.
Nashukuru kwa elimu .Kichwa habari unasema umma, habari ndani inasema mahakama. Kifupi suala likishaitwa la kiuchunguzi halina mipaka tena hasa kwa sheria zetu.
Polisi wanauwezo wa kuomba mawasiliano ya mtu yeyote kwa sababu za kiuchunguzi
Huku kwetu watu ni waoga wanaogopa kufa,kule Marekani kuna tukio moja lilitokea miaka michache iliyopita,kampuni ya apple waliigomea katakata FBI,kuifungua simu iliyowekwa lock,iphone hiyo ilikuwa inamilikiwa na kijana mmoja mwenye asili ya Asia ambaye alishukiwa kwenye tukio la ugaidi,ambapo aliidondosha simu hiyo na makachero wa FBI,walishindwa kuifungua simu hiyo,hiyo simu ilivyotengenezwa ilikuwa ukifanikiwa kuifungua kwa kuilazimisha basi inafuta data zote,kwa hiyo FBI kimbilio lao la mwisho kuifungua simu hiyo ilikuwa ni kuwaomba kampuni ya Apple wawasaidie kuifungua simu hiyo,lakini Apple wakakataa kwa kuhofia Siri za mteja wao zikianikwa basi kampuni yao ingekosa sifa ya kitu za Siri za wateja wao,na jinsi sheria za Marekani zilivyo,FBI hwakuwa na uwezo wa kuilazimisha Apple kufanya upuuzi huo.Unayaona Leo hayo au?
Sheria zimewekwa kama utaratibu tu unavyotaka, Wanaosimamia sheria ni wale wenye Mamlaka
Katiba yetu imetoa mwanya kuna watu wapo juu ya sheria na huwezi kuwagusa
Hivi Mkurugenzi wa Voda au Tigo ana nguvu gani akitumiwa wale Jamaa, Najua unawafahamu
Maisha yako binafsi ni muhimu kuliko kukumbatia taarifa zinazohitajika na watu waliojuu ya katiba
Kwa usalama wa Taifa au nchi ukigoma kutoa taarifa kesho tunaweza tukakusindikiza kwa nyimbo za pala panda ikilia
Sheria zipo, Kuna muda lazima uangalie maisha yako
Huwezi Shindana na mtu ana Vifaru, Bunduki na Jeshi lote linamuheshimu
Mdomo na kiburi vimewagharimu watu maisha na Leo wameacha familia kisa tu kujifanya wanafuata sheria na katiba
Katiba ni karatasi tu, Wanaosimamia katiba wapo juu ya katiba
Muda wowote sheria hupindishwa au kunyooshwa kwa matakwa ya Mamlaka
Ongeza PCCBKwenye hiyo orodha tcra hawamo maana wenyewe wanamiliki mtambo wao wenyewe wa kurekodi mawasiliano