Ni sahihi mwenye nyumba kumwekea mpangaji sharti la aina ya wageni wanaomtembelea?

Ni sahihi mwenye nyumba kumwekea mpangaji sharti la aina ya wageni wanaomtembelea?

Jamani, sasa nisipate huduma za msingi za kimwili? Lakini pia, kila mwanamke anayekutembelea lazima awe mshirika wako wa kingono? Na hata akiwa mpenzi wangu, kuna shida gani yeye kuja ninapoishi tukapika, tukackeki muvi na kufurahiana?

Itabidi tukutane gesti kila siku?
Sasa wasiwe wengi inakuwa kero bana!!
Unakuta na midada mingine ina misifa inapiga mikelele ya sauti za kimahaba mnaanza kutesa wengine kihisia 🤣
 
Unda Teeth yako binafsi, imfuatilie huyo Mzee ni Dini/Dhehebu gani?. Kuna madhehebu wachumba kuonana hadi awepo mtu wa tatu[emoji1787]
Wewe utakua dishi limeyumba sio bure,unaonekana ni mtu mwenye umri mkubwa ila kichwani patupu,

Hii mada haihusiani na udini,tutolee upuuzi wako hapa.
 
Kuna mwenye nyumba wengine hasa wa kike wao huomba omba vyakula kwa wapangaji wao kuanzia asubuhi mpaka usiku. Wanaishi kwa kugongea misosi kwa wapangaji wao. Ukiwa msela tu huna mke na hupiki geto ataomba hela ya kitunguu, nyanya, chumvi, kiberiti na vikorombwezo vingine. Ni kero tupu
 
wanajiamini sana kiasi cha kupangia wapangaji masharti ya kuishi. Unapangiwa namna ya kutumia choo na kujisafisha utumie material gani, muda wa kurudi usiku, aina ya vyakula vya kupikwa, muziki wa kuwekwa na aina ya wageni wa kuja
Imagine mtu ukikubali kuishi namna hiyo kwa miaka mitatu tu utakuwa umepoteza kiasi gani cha maisha yako. Si jambo jema kwa afya ya akili na ustawi wa mwanadamu.
 
Njoo uku kwetu mwenye apartment ana namba za malaya wa levo zote ukiwa mpangaj mnyonge mnyonge anakwambia hapa n olmpk utapaweza kwel
 
Mimi nilipata changamoto mwanzoni baada ya siku kupita nikala kuku na mayau yake
 
Mimi niliambiwa siruhusiwi kulala na watu zaidi ya 3 Yani kama ndugu zangu wamenitembelea wengi hawaruhusiwi😭
 
Ni vizuri kuwe na utaratibu wa wageni,kwani si ustaarabu kugeuza chumba kuwa DANGURO,lakini vilevile wakati mwingine haohao wageni huwa ni WEZI,
 
Sasa wasiwe wengi inakuwa kero bana!!
Unakuta na midada mingine ina misifa inapiga mikelele ya sauti za kimahaba mnaanza kutesa wengine kihisia 🤣
Hapo kwenye kelele nakubali kuwa ni kukosa ustaarabu kwenye eneo ambalo watu wanaishi kama jumuiya. Lakini kama hakuna hayo au matusi na mambo mengine ya ajabu yanayotokea, basi mwenye nyumba hapaswi kuleta tu hisia za kwamba kuna ngono inaendelea humo ndani. 😂
 
Jijini Dar es Salaam na maeneo mengine nchini Tanzania, suala la makubaliano kati ya mwenye nyumba na mpangaji ni jambo la kawaida. Makubaliano haya hujumuisha mambo mengi kama vile kodi, malipo ya huduma za nyumba, na masuala mengine yanayohusiana na kukaa kwenye nyumba ya kupanga. Hata hivyo, kuna baadhi ya wenye nyumba ambao huenda zaidi kwa kumuwekea mpangaji sharti la aina ya wageni wa kumtembelea.

Njoja niwape stori kwanza. Mwaka 2017, niliamua kuishi kwenye nyumba moja maeneo fulani huko Goba, Dar es Salaam. Mwenye nyumba naye alikuwa anaishi hapo, na tukiwa tayari kwenye mkataba wa kupanga, hakunipa taarifa yoyote kuhusu sharti la kutoleta wageni wa jinsia tofauti.

Mwenye nyumba alianza kuonesha wasiwasi juu ya wageni wa kike waliokuwa wakija kunitembelea. Alifanya mambo kama kuniangalia kwa jicho la tatu kila wageni wa kike walipokuja. Yaani alikuwa hadi akisimamisha shughuli zake ili kujiridhisha kama walikuwa wageni aliowahi kuwaona awali au ni wageni wapya.

Siku moja, alinitolea uvivu na kuniambia kuwa wageni wa kike wamekuwa wengi sana kwenye nyumba. Nilimuuliza ikiwa kuna siku nilivunja amani au niliwahi kusababisha fujo na kelele zisizo za kistaarabu, na jibu lake lilikuwa "hapana." Tatizo lake na wageni wa kike eti ni kwamba nitawaharibu wanae kwa kushuhudia vitendo vya “kimalaya”. Cha! Nilichoka.

Hata hivyo sikukaa kimya. Nilimkumbusha mwenye nyumba kuwa watoto wake wanahitaji kufundishwa kuhusu ustaarabu na kuheshimu watu na wasiige mambo ya kipuuzi hata wakiwa huko shule. Nilimkumbusha kuwa ana jukumu hilo la kutekeleza kwa wanae na si kwa kumzuia mpangaji kuleta wageni.

Nilisisitiza pia kuwa si kila mwanaume au mwanamke anayekuja kumtembelea mpangaji anakuja kwa lengo la kufanya mambo ya kimapenzi. Baadhi ya wageni ni marafiki wa kawaida, ndugu, au jamaa ambao wanataka kutembelea na kufurahi pamoja. Nilimwambia kuwa si sahihi kuvunja ustaarabu na uhuru wa mpangaji kwa kisingizio cha kuwalinda watoto wake.

Lakini pia nilimwambia kuwa bado mimi ni kijana na nipo katika mchakato wa kutafuta mwenza wa maisha. Kwa hiyo, baadhi ya wageni wa kike, mbali na marafiki na familia, wanaweza kuwa wanawake ambao ninafikiria kuwa huenda nikaoa siku za usoni, kwahiyo hakupaswa kuninyima fursa ya kupenda na kupendwa. Sijui alitaka niishi vipi mzee yule. Sema alijitahidi kunielewa.

Wenye nyumba, kuweka mazingira ya kukodisha ambayo yanawapa wapangaji uhuru wa kufanya maamuzi kuhusu wageni wao ni muhimu sana. Hii inahitaji uelewa wa utofauti wa tamaduni, imani, na mienendo ya kijinsia.

Kuwapa wapangaji nafasi ya kuwa na wageni au marafiki bila kuwahukumu au kuwabagua ni ni jambo la msingi sana. Pia, ni muhimu kuondoa ubaguzi wa kijinsia na kuacha watu wa jinsia tofauti kuwa na mahusiano ya urafiki au kufanya shughuli pamoja bila kutafsiriwa kwa dhana za ngono. Cha!
sema ulikua unabadilisha mademu wa kila sampuli si wageni wa kike.

sema nini ?

kuna vojana mna mambo ya hovyo hovyo kweli mkipanga sehemu panageuka kua dangulo yaani wanawake wanapishana kama clinic vile tabia ambayo sio ya kistaraabu kabisa.

sina nyumba mjini hapa ila nikijenga halafu nikapangisha kijana akawa na mambo ya hovyo hovyo kama wewe nakuondoa chap.

ndio maana sehemu zingine ukienda kupanga swali la kwanza ni UMEOA ?

ili kuepusha mambo ya aibu kwenye mji.
 
Jamani, sasa nisipate huduma za msingi za kimwili? Lakini pia, kila mwanamke anayekutembelea lazima awe mshirika wako wa kingono? Na hata akiwa mpenzi wangu, kuna shida gani yeye kuja ninapoishi tukapika, tukackeki muvi na kufurahiana?

Itabidi tukutane gesti kila siku?
tunaijua hio 😁
 
Hapo kwenye kelele nakubali kuwa ni kukosa ustaarabu kwenye eneo ambalo watu wanaishi kama jumuiya. Lakini kama hakuna hayo au matusi na mambo mengine ya ajabu yanayotokea, basi mwenye nyumba hapaswi kuleta tu hisia za kwamba kuna ngono inaendelea humo ndani. [emoji23]
Hata mm nikijenga nyumba yangu siwezi ruhusa kuwa sehemu ya kufanyia uzinzi, kama ninge taka kujenga sehemu ya kufanyia uzinzi ninge jenga guest bubu.
 
Hata mm nikijenga nyumba yangu siwezi ruhusa kuwa sehemu ya kufanyia uzinzi, kama ninge taka kujenga sehemu ya kufanyia uzinzi ninge jenga guest bubu.
Natumai umesoma na kuelewa hoja yangu.
 
Kuna mwenye Nyumba mmoja mkataba wake ameandika wageni wakija kumtembelea mpangaji wasikae zaidi ya siku moja maana watajaza Choo.
Hiyo ni sahihi kabisa kwasababu nyumba inapojengwa kwa mfano apartments hujengwa kuzingatia jumla ya watu watakaoishi humo ; ndio maana kabla ya kupangishwa unaulizwa ukubwa wa familia yako ili iendane na capacity ya nyumba husika.
Wenyenyumba wasipokuwa strict kwa mfano apartment ya vyumba viwili mpangaji anaweza kuleta ndugu zaidi ya sita kuishi humo! Hii si busara kwani sio tu nyumba its jamaa upesi bali pia sio vizuri kwa afya za wahusika.
 
Back
Top Bottom