Mateo Kovasic
JF-Expert Member
- Aug 9, 2022
- 420
- 334
Vijiji vya njiani ukiwa unapita kwenda mikoani unakuta mtu anatembea kuelekea uelekeo ambao ww huoni nyumba
Vijiji vya lindi
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Vijiji vya njiani ukiwa unapita kwenda mikoani unakuta mtu anatembea kuelekea uelekeo ambao ww huoni nyumba
Viko hivyo eeVijiji vya lindi
Kiyegeya siyo mchezoNimekaa mtwara Lind sijakaa ,nimekaa pale ligula mnarani kwa kweli ni fresh Tena karibu na hospital Pako poa sana ningependa huduma zipo halafu watu wachache
Lutindi pako poa umeme tangu 1975Unapajua lutindi mashindei
Mtwara hakuna vijiji vibaya sana, ni moja ya mikoa ambayo vijiji vyake unakutana na NYUMBA nyingi kabisa, wanakuwa na Soko, maduka yanakuwepo. Kule 90% ya vijiji magari yanafika, nyumba nyingi ni zile za udongo lkn zenye bati na kubwa sio kama vijiji vya kule DODOMA Jmn hadi unajiuliza wanalalaje mule?? Sijui ilikuwaje lkn Mtwara kwenye vijiji wako far better than 80% ya mikoa ya TZ.Nimekaa mtwara Lind sijakaa ,nimekaa pale ligula mnarani kwa kweli ni fresh Tena karibu na hospital Pako poa sana ningependa huduma zipo halafu watu wachache
Baridi linaunguza mimea😳?Niliwahi kufika kule mwaka 2002 mpaka mimea inaungua kutokana na baridi nilifika kandete, kyejo mpaka isange kupitia kiwanda Cha majani ya chai Katumba au Tandale Tukuyu Mjini.
vijiji vingi hilo limkoa havifai kuishi binadamu.Dodoma ni hatari ,kuna vijiji vinapatikana shortcut (mpwapwa to Iringa road)
Imagine hadi wakiona gari wanakimbia,ilibidi tushuke kwanza tuwauulize maswali ya hapa na pale kuhusu maji,chakula maana Hamna mazao kabisa na vumbi linatimka muda wote ,Vitoto vimebuka hatari unahisi hata wakipiga maji hawatakati,kiswahili pia shida
ulisoma mwaka gani pale au wakati wa mwandi baby kule mule paleMwakaleli- Tukuyu Mbeya..aisee baridi lilinushinda pale Mwax sec
Et vimebuka[emoji23][emoji23]we itakua mmakonde wwDodoma ni hatari ,kuna vijiji vinapatikana shortcut (mpwapwa to Iringa road)
Imagine hadi wakiona gari wanakimbia,ilibidi tushuke kwanza tuwauulize maswali ya hapa na pale kuhusu maji,chakula maana Hamna mazao kabisa na vumbi linatimka muda wote ,Vitoto vimebuka hatari unahisi hata wakipiga maji hawatakati,kiswahili pia shida
Nilipanda mlima uluguru nikakuta waluguru huko juu Tena wanavijiji vyao Hali ya hewa ilikuwa nzuri ila huduma za kijamii Hadi uteremke mlima, binafsi nilishuka miguu inatetemeka na maumivu makali mno. Mpaka Leo nawashangaa watu Kule wanavyoishi
🤣🤣🤣🤣 hapanaEt vimebuka[emoji23][emoji23]we itakua mmakonde ww
Hahahavijiji vingi hilo limkoa havifai kuishi binadamu.
Kumbe mpaka lisaa linaweza kukata uko juu vilimani unatembea?Mwanza miambani wananoishi watia huruma sana japo wao wanaona wamepata viwanja city centre.
Huwa najiuliza walishindwaje kuweka makazi Usagara, Misungwi na Magu badala ya kubanana kwenye mawe kama mijusi ambako kupanda ni shida na inaweza kuchukulia lisaa kwenda sehemu unayoiona kwa mbele tu hapo.View attachment 2378247
Kwa mara ya kwanza kufika kijiji cha Bugamba kilichopo mwambao wa Ziwa Tanganyika Kigoma vijijini nilipigwa na mshangao baada ya kushuka kwenye boti kutokea Kibirizi Kigoma ! Pale boti zinapoegesha sikuona nyumba yoyote ! Mwenyeji wangu kaniambia tunaenda nyumbani yaani ananionyesha juu utafikiri tunaenda mwezini ! Kutoka hapo tunapanda huko juu nilitaka kulia maana chini Ziwa Tanganyika juu ndio kijijini, halooo kupanda ilibidi mpaka nishikwe mkono. Kufika huko juu ndoo nakuta kijiji na shule ya msingi ukitizama chini ziwa Tanganyika liko bondeni ! Kwa kweli inatisha kijiji hicho hakuna shamba la maana sehemu kubwa ni milima tu mihogo wanalima kwenye mitelemko ya milima na ukiteleza unaporomokea ziwani na ziwa lina kina kirefu ni hatari. Pale kijijini hakuna baiskeli maana mazingira hayaruhusu ! Shughuli za uchumi pale ni uvuvi. Ukitaka kwenda kijiji cha jirani cha Zashe au Mwamgongo lazima utumie boti kwa mguu haiwezekani.Kijiji cha Bugamba Kigoma vijijini mwambao wa ziwa Tanganyika
Kuna kijiji nilifika kutafuta ndizi biashara miaka hiyo.
Aisee ni mbali katikati ya turiani na korogwe njia ya pori kwa pori.hamna magari ni kwenda kwa baskeli tu alafu unachepuka kwenda mlimani huko nikakuta kakijiji aisee vijumba kichekesho,alafu wana mfalme wao yaani chakula wanakula woote familia zoote pale kwa mfalme.
Kila kaya inaleta ilichopika pale.
Nilikula mboga mboga mpk nilikoma.
Siku nikalogwa nikanunua kuku 2 wameniuzia wao wenyewe kaya 1 niliokuwa nakaa nikawapa wapike nikajua ntakula japo nusu aaah wakapeleka kwa mfalme kule tunakokula nikaambulia kibawa,yaani mkulu ana nyofoa kinyama anampa mtu kushoto au kulia kwake kinatumwa mpk kikufikie kila mtu kakishika
Nilikasirika sana.