Ni sehemu gani ya nchi, mji au Kijiji ulifika mpaka ukajiuliza watu waishio huko walifuata nini?

Ni sehemu gani ya nchi, mji au Kijiji ulifika mpaka ukajiuliza watu waishio huko walifuata nini?

Barabara ya kwenda Kilimanjaro nahisi ni wilaya ya Same Kuna nyumba moja nzuri tu imejengwa kwenye mlima kabisa ipo juu kileleni ipo peke yake ukipita barabarani kwa gari unaiona vzr tu...yule jamaa sijui alifikiria nini kujenga kule juu
[emoji23][emoji23][emoji23] napajua
 
MTWARA ipi?? Mtwara inaizidi mikoa mingi sana Tanzania kwa Maendeleo, Hata vijiji vyake huwezi linganisha karibu na Robo 3 ya mikoa ya Tanzania hii. Unalinganisha Mtwara na mikoa ipi??
Vijiji vya Mtwara kusema kweli sio choka mbaya.. Mambo ya Ushirika yanawasaidia sana na zao la korosho liko vizuri linawapatia kipato na exposure.

Vijiji karibia vyote vya Mtwara vina huduma muhimu za shule, zahanati, maduka, umeme ni maji tu ndio changamoto kwa baadhi ya wilaya kama Tandahimba, Newala na Nanyumbu. Ingawa wenyewe wanachimba visima virefu kuvuna maji ya mvua. Kukuta nyumba nzuri za tofali zimeezekwa msouth kigae au mgongo mpana ni kawaida kabisa.
 
Kasulu Kigoma. Nimeshuka kwenye basi naingia barabarani nakanyaga chini kiatu chote kimezama kwenye vumbi flani laini sana jekundu nikasema dah namna hii mvua zikinyesha panakuwaje si inabidi miguu iwe na 4WD.. Palinichosha mapema sana
 
Kuna Kijiji kinaitwa KWAMASIMBA Kiko wilaya ya Korogwe mjini. Aiseee pale gari zinafika cruiser mkonga tu Tena kwa gear namba moja ikisaidiwa na four wheel LOW.
Umenikumbusha, Korogwe kuna sehemu inaitwa Bungu kama sijakosea. Miaka ya nyuma kidogo 2004 au 2005. Kufika huko kuna kibasi kimoja tu. Na safari nzima kuna vipande vya kutosha mnavyotembea kwa mguu. Halafu kulikua na ushirikina wa kutosha. Kama unaishi kule na wewe si mwenyeji wa kule, siku ukitaka kusafiri kwenda nyumbani kwenu kusalimia au kama unahama hautakiwi kuaga unasepa kimya kimya tu. Yaani raia wastukie upo kwenye gari na mizigo yako. Sasa wewe jifanye ina aga hutoboi Korogwe mjini. Pia mvua ikinyesha nayo ni uchawi tu, kunateleza hata kuku hatembei barabarani na usafiri unakosekana pia
 
Umenikumbusha, Korogwe kuna sehemu inaitwa Bungu kama sijakosea. Miaka ya nyuma kidogo 2004 au 2005. Kufika huko kuna kibasi kimoja tu. Na safari nzima kuna vipande vya kutosha mnavyotembea kwa mguu. Halafu kulikua na ushirikina wa kutosha. Kama unaishi kule na wewe si mwenyeji wa kule, siku ukitaka kusafiri kwenda nyumbani kwenu kusalimia au kama unahama hautakiwi kuaga unasepa kimya kimya tu. Yaani raia wastukie upo kwenye gari na mizigo yako. Sasa wewe jifanye ina aga hutoboi Korogwe mjini. Pia mvua ikinyesha nayo ni uchawi tu, kunateleza hata kuku hatembei barabarani na usafiri unakosekana pia
Wewe utakua unaongelea Bungu ya Rufiji.
 
Mwanza miambani wananoishi watia huruma sana japo wao wanaona wamepata viwanja city centre.

Huwa najiuliza walishindwaje kuweka makazi Usagara, Misungwi na Magu badala ya kubanana kwenye mawe kama mijusi ambako kupanda ni shida na inaweza kuchukulia lisaa kwenda sehemu unayoiona kwa mbele tu hapo.

View attachment 2378247
Duh!
 
Katikati ya mpanda na kigoma kuna pori wanauza chakula
- Na wanadai kwenda makwao wanatumia zaidi ya masaa 3 kwa mguu; na mtu akitumia gari anachelewa kufika kuliko aliyepita ya mguu. 😂😂😂😂
  • Njia ya Iringa - Dodoma naonaga watu wakitembea barabarani, japo ni tambarare ila lakini vijiji havionekani.
  • Makongorosi - Chunya kule bondeni ziwani kuna kijiji unapita katikati ya kimlima cha miamba kwa miguu. Tuliwafi fika hata wenyeji wakasema, je mmefikaje?, Mmekuja kufanya nini?
 
Habari za muda huu wana JF,

Nchi yetu ni kubwa na Ina miji na vijiji vingi lakini Kuna baadhi ya maeneo unaweza ukahisi sio sehemu ya nchi yetu mpaka ukajiuliza maswali kuwa Hawa watu waishio hapa walivutiwa na Nini mpaka wakaweka makazi ya kudumu maeneo haya

Mfano, Mimi niliwahi kutembelea Kijiji cha Baranga kata ya Sirorisimba kupitia Kyagata. Nilistajabu na kujiuliza Hawa watu huku wanaishije?

Ukame ndio kwao, maji shida, Hali ya hewa mbovu, jua kali ndio kwao, vurugu Sasa ndio chimbuko lake. Siku moja tulikuwa na mechi ya kirafiki na timu ya Kijiji jirani ile tupo kwenye gari tukashangaa tunaanza kurushiwa mawe barabarani.

Kwa kuwa sisi tulikuwa wageni tuliogopa sana lakini wenyeji wakatuambia msiogope hao wote tutakutana kwenye mnada. Siku nyingine tulikuwa Mnadani Sirorisimba siku hiyo kulikuwa na mgogoro wa mpaka wa shamba kati ya ukoo na ukoo huku polisi wakiwa na mitutu ya bunduki lakini ilivyo ajabu watu wa kule nilishudia wakibebana na kuhamasishana wabebe mishale waende wakaanzishe vurugu.

Wewe ulipita wapi na ulistaajabu nini?
Kijiji cha kilosa Mpepo wilaya ya malinyi...Kila siku kule ni kupambana na Tembo na Nyati...Masika hakuendeki nilikuwa kule 2020 sijajua saivi pakoje
 
kijiji cha tanganyika,kata ya masagati tarafa mlimba wilaya ya kilombero .nikipangiwa kule kituo cha kazi mwaka 1999 nikarudi kumshukuru DED kwa kazi.nikarudi zang Dar .aise Kule watu alikuwa wanaishi kama mazombie hakuna huduma ylza jamii hata moja hadi uende mlimba 150km Dahhh ila nasikia mambo siku hizi yamebadilika Luna kula kitu japo afadhari.
Saivi kuna barabara kabisa inaenda Njombe....Kilimo cha mpunga pako poa tu
 
Weee sasa hivi kuna maji kuna hospital,kuna halmashauri
Kuna mtu alitudanganya ni kama km 6 kutoka ile kona la Kolandoto .Kuna mbuzi wanachoma barabarani kama una roho ya kinyaa huli.Mi nilibonda ,ntarudi tena huko Mhunzee.
 
Back
Top Bottom