Ni sehemu gani ya nchi, mji au Kijiji ulifika mpaka ukajiuliza watu waishio huko walifuata nini?

Kule wasukuma wa mashuka wamejaa na kuna kilimo cha mpunga
 
Masagati hii ya Mlimba...Huku enjoy samaki na Mchele bei chee...Ila kule nasikia uchaw unauzwa
 
Bungu wilaya ya Mvuha mkoa wa Morogoro ni milimani ,hakuna usafiri, barabara ni shida daaaaah! Wale watu wanaishi maisha ya taabu kweli kweli
 
Utafkr
Bungu wilaya ya Mvuha mkoa wa Morogoro ni milimani ,hakuna usafiri, barabara ni shida daaaaah! Wale watu wanaishi maisha ya taabu kweli kweli
Dunia imejaa na hakuna sehemu nyingine za kuishi na huko huwatoi wenyew
Ng'apa, Lindi!
Basi vinafanana kingine kinaitwa hivohivo Ng'apa ukitoka Mikumi kabla hujafika Iyovi watu wako wanaishi milimani porini.
 
Hata sisi tunakushangaa kututajia majina ya vijiji kana kwamba woote humu ni wenyeji wa huko. Ungetaja angalau wilaya na mkoa (au nchi) tungekuelewa na kuchangia. Pia hujaweka picha
 
Masange ..huko kondoa irangi..ma.mae
 
Vijijii vyote vya mkoa wa kigoma
 
Kuna kijiji ukiwa unaenda Loliondo ukitoka Oldonyo Rengai kuna kijiji hapo karibu na Lake Natron huwa sielewi hao jamaa walifuata nini hapo?
 
Hata sisi tunakushangaa kututajia majina ya vijiji kana kwamba woote humu ni wenyeji wa huko. Ungetaja angalau wilaya na mkoa (au nchi) tungekuelewa na kuchangia. Pia hujaweka picha
Pole mkuu Ni makosa ya kiuandishi, unajua unapoandika anahisi kila mtu amefika hiyo sehemu. Ni sawa na aliyeshiba hamuoni mwenye njaa, Ila Ni Wilaya ya Butiama, mkoa wa Mara.
 
Kuna kijiji ukiwa unaenda Loliondo ukitoka Oldonyo Rengai kuna kijiji hapo karibu na Lake Natron huwa sielewi hao jamaa walifuata nini hapo?
Inashangaza Sana kwamba walikosa maeneo au na sehemu nyingine Ni Kawetere njia ya kwenda Chunya Mbeya, Kuna Baridi Kali na ni mlimani Hadi nyumba tu wamejengea mbao na mabanzi kupunguza Baridi. Lakini wanakomaa palepale miaka.
 
Hatari mno ndo unaumwa mkuu si unafia njiani.
Kutoka Mahenge mjini kwenda Mzelezi au Ruaha distance ya kilometers 30 nauli elf 50 kwa pikipiki masaa mawili ,wakati Toka mahenge Hadi Dar kwa bus masaa kumi na mbili nauli elf 35.
 
Hatari sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…