Ni sehemu ipi NAIROBI wanaishi watanzania wengi?

Ni sehemu ipi NAIROBI wanaishi watanzania wengi?

Habari wakuu?
Naomba kujuzwa kuwa ni sehemu ipi Nairobi Kenya wanakoishi/wanakofanya biashara Watanzania wengi?

Kama ukitaja na majina ya labda maduka/hoteli/baa/Club zinazomilikiwa na watanzania itasaidia pia.
Natanguliza shukuraniView attachment 2257211
Nenda soko la mitumba GIKOMBA hapo wakina Mangi wamejaa utazani Rombo
 
Wanapoishi kwa wingi si rahisi kupajua ila najua sehemu ambayo wengi wapo na wanafanya shughuli zao, hasa za kuuza mitumba kwenye soko maarufu la mitumba la Gikomba mjini Nairobi ila shida karibu asilimia kubwa huwezi kuwajua kama Watanzania kwani ni Wachaga wanaoongea lugha ya Kikuyu utadhani wamezaliwa Nanyuki.
Mkuu upo Sahihi unajua wabongo wengi walitawanyika,maeneo kama majengo ambapo ni karibu na Gikomba walikuwepo pale sababu ni karibu na shughuli zao..

Wengine walikuwa wanaishi pale California ni karibu na Majengo pameungana na Eastleigh kuna pilika nyingi za kibiashara pale Eastleigh.

Pale Eastleigh kuna wasomali wengi sana na wengine walitokea kwetu huku Tanzania sasa mpaka ufahamiane nao ndiyo utawajua.

Katikati ya mji wabongo wapo maeneo ya Accra Road kwenye Coast Bus zinapo park Bus za Malindi na Mombasa hapo utawakuta wabongo toka sehem za Tanga.
 

Ipo hiyo sehemu pia kuna Makaburi ya Kariakoo maeneo hayo ndipo alipozikwa Bondia Robert Wangira .
Baada ya Waislam kushinda ile kesi ya kuuzika Mwili wake, kesi iliyochukua zaidi ya miezi 8 Maiti ikiwa Mortuary kusubiri maamuzi ya Mahakama.

Siku ya Mazishi yake Kariakoo hapakutosha.
 
Mombasa road, Accra road,jogoo road na west land kidogo pia Karen wapo
 
Wanapoishi kwa wingi si rahisi kupajua ila najua sehemu ambayo wengi wapo na wanafanya shughuli zao, hasa za kuuza mitumba kwenye soko maarufu la mitumba la Gikomba mjini Nairobi ila shida karibu asilimia kubwa huwezi kuwajua kama Watanzania kwani ni Wachaga wanaoongea lugha ya Kikuyu utadhani wamezaliwa Nanyuki.
Ni kweli Gikomba kuna wachaga wengi sana ila wengi wameshalowea huko, ila ukifanikiwa kumpata mtanzania mmoja anaweza kukutambulisha katika vikundi vyao huko utaweza kufahamihana zaidi.
 
Mkuu upo Sahihi unajua wabongo wengi walitawanyika,maeneo kama majengo ambapo ni karibu na Gikomba walikuwepo pale sababu ni karibu na shughuli zao..

Wengine walikuwa wanaishi pale California ni karibu na Majengo pameungana na Eastleigh kuna pilika nyingi za kibiashara pale Eastleigh.

Pale Eastleigh kuna wasomali wengi sana na wengine walitokea kwetu huku Tanzania sasa mpaka ufahamiane nao ndiyo utawajua.

Katikati ya mji wabongo wapo maeneo ya Accra Road kwenye Coast Bus zinapo park Bus za Malindi na Mombasa hapo utawakuta wabongo toka sehem za Tanga.
Asante mkuu kwa maelezo mazuri
 
Back
Top Bottom