Ni siku gani ilikuwa bora kabisa kwako, ilikuwaje?

Ni siku gani ilikuwa bora kabisa kwako, ilikuwaje?

Nyafwili

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2023
Posts
4,240
Reaction score
10,561
Zile siku ambazo tuliishi kuziota kuwa badae yetu, kiasi zimekua mbali na sisi, naam! zile siku tulizoambiana utotoni kuwa tungekuwa hivi na vile.

Siku zilizojengwa kwa dhana na picha ya umaridadi kwamba kabla ya miaka ya muongo wa tatu tutakua tumefika hapa na pale au kumiliki hiki na kile.

Maisha yamejengwa kwenye kila siku moja tunayoishi, ambamo ndani yake kuna mda usioeleweka wa kufurahi, sekunde za uchungu, dakika za kuchoka na saa za kusubiri siku moja ipite ili ije iliyo bora.

Ebu tiririka hapa, ni siku gani hiyo ambayo ilikua bora kabisa katika maisha yako, tag na location.

Da!! kwa upande wangu bado sijapata siku iliyo bora. 🤒🤒
 
Siku 365 za mwaka mzima, kutafuta siku 1 bora ni kama 364 umejinyima furaha. Siku ni siku tu, hakuna siku mbaya wala siku nzuri. Matukio yapo tu na hayaishi. Hata leo na kesho pia unaweza kuzifanya bora
Ni kweli mkuu, ila kuna sisi ambao kila kukicha ni heka heka zisizo na kipimo,
 
Mara ya kwanza kugonga nilipiga bao tatu ndani ya dakika 4 Ile non stop,(kitu ilikuwa mnato)haijawahi jirudia tena,nakumbuka godoro lilianikwa wiki nzima,na lilikuwa ghto la msela 😁

Kwa nini mkuu haijawahi jirudia tena?? au ndo nyota ipo kwa mishangazi kwa sasa 🤒🤒
 
Siku nilipwa usdt 5.76 mara 111 ndan ya dk 5 nilpokea more than 600usdt asee sikujua zmetoka wapi

[emoji838][emoji838][emoji838][emoji838]

Na kwakuw ni cryptocurrency haikusumbua lolote
 
Swali gumu na lenye majibu mapana sana, Kuna siku nyingi bora kulingana na nyakati, umri, nafasi nk hivyo siku bora haziishi, kuwa na siku moja tu Bora peke yake inakuwa ngumu bali Kuna makumi ya masiku ambayo Kwa kiasi fulani yalikuwa Bora...binafsi siku yoyote ile ambayo nimetimiza malengo yangu Huwa ni bora sana hata lengo dogo tu, siku zangu Bora mara nyingi nazigawa kulingana na nyakati na umri, mfano nyakati za masomo siku zangu Bora zilikuwa ni siku za mitihani, kikifika kipindi hiki Huwa akili na mwili vinakuwa vyepesi nilikuwa napenda tu ile situation ya utulivu, kukaa darasani masaa kadhaa then unatoka zako, karatasi za maswali always zilikuwa zikinipa nyakati nzuri, imagine unakomaa na swali linakusumbua kichwa unatafuta namna Bora ya kulijibu, what a moment ilikuwa Dunia ya kipekee kwangu...hivyo nikitafuta siku zangu Bora nazigawa Kwa nyakati
 
Back
Top Bottom