Ni Tanzania tu, tunakotaka mabadiliko bila vitendo

Ni Tanzania tu, tunakotaka mabadiliko bila vitendo

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Watanzania wamekereka kweli kweli na wanataka mabadiliko.

Wanataka katiba mpya. Wanataka wabadhirifu wawajibishwe. Wanataka utawala bora, hawataki uwakilishi wa walamba asali au wa wahuni nk.

Yote mema kabisa. Tatizo kubwa ni kuwa wanayataka mema hayo wakiwa unorganized. Matokeo yake wamekuwa ni kama genge la wenye kuyataka mema hayo kwa maneno si kwa vitendo.

"Wamekuwa genge la watu ambao wangependa yule au wale wafanye vitendo lakini si wao."

Ifahamike kuwa mabadiliko hayataletwa na walamba asali, wahuni au wale vijana wa hovyo. Kwa huruma zao au kuwalilia hali.

Vile vile tufike mahali tuambiane ukweli. Wenye maneno matupu au maoni, ni heri wakakaa nayo tu. Hayahitajiki!

Tumeyaona kote kwingine Kenya, Zanzibar, SA nk. Vinahitajija vitendo? Wako wapi kina Raila, Maalim Seif, Tutu, Mahlangu, Biko, Mandela au Malema?

Siyo siri tena. Kwa hapa tulipo hatunao viongozi wa kutuongoza kwenye tunayoyataka. Hapa ndipo pa kuanzia:

"Tupange safu za viongozi wetu kulingana na matokeo tunayotaka."

Tupite kwenye primaries tusikie mikakati ya kila mmoja anayetaka uongozi. Asiyefaa akae pembeni au tumweke pembeni.

Hizi nyimbo za kuwalaumu wafuasi wakati wanaofisha jitihada hizi wanajulikana ni muda sasa zikakoma.

Uongozi usiwe fursa. Uongozi ni mzigo. Uongozi una risks. Uongozi ni kuwajibika. Uongozi si lele mama.

"Joto likikuzidi unawaachia wengine."

Luka 18: 18-27 -- alipoambiwa kuuza kila kitu awape maskini ....

"Mitu ya Fursa."
 
Chawa at work

Chawa wa nani basi? Labda wa Maalim Seif, Tutu, Biko, Mahlangu, Nyerere, Raila, Malema au wa namna hiyo?

Kama miye ni chawa at work, wewe ni nani? Mlamba asali, mhuni au kijana wa hovyo?

Kazi kweli kweli.
 
Tuko kwenye maridhiano tafadhali!

Kuongea huku tukomaliana ndiyo njia bora zaidi ya kupata muafaka.

Maridhiano yana nini Cha kufanya na kuwawajibisha wezi wetu au kutokuwa na ratiba ya tunayoyataka?
 
Chawa wa nani basi? Labda wa Maalim Seif, Tutu, Biko, Mahlangu, Nyerere, Raila, Malema au wa namna hiyo?

Kama miye ni chawa at work, wewe ni nani? Mlamba asali, mhuni au kijana wa hovyo?

Kazi kweli kweli.
We jaza jedwali unavyoona I don't care
 
Chawa at work -- ninejaza ndugu
Miaka zaidi ya 60 ya uhuru nchi maskini bado huku watu wa fanya ubadhilifu kweupe na hawachukuliwi hatua

Then what? Kila Mara kudhulumu haki za watu

Ndo Maana watu tunawacheki tu
 
Miaka zaidi ya 60 ya uhuru nchi maskini bado huku watu wa fanya ubadhilifu kweupe na hawachukuliwi hatua

Then what? Kila Mara kudhulumu haki za watu

Ndo Maana watu tunawacheki tu

"Ndo Maana watu tunawacheki tu."

Kwani ninyi ni kina nani na mnaowacheki ni kina nani ndugu? 🤣🤣
 
Je, Hili andiko lako la "hamasa" linawahusu watu wa dini zote au ni Wakristo tu??

Dini zote ni zipi ndugu?

"Mormoism, Judaism, Buddhism, unitarianism, Islam, Scientology, Jewish, ... ?"
 
Democracy na Ugaidi ni itikadi tofauti zenye malengo na matendo sawa.
 
Democracy na Ugaidi ni itikadi tofauti zenye malengo na matendo sawa.

Hapana. Hiyo ni tafsiri potofu. Tafsiri sahihi iko hapa ndugu:

 
Sisi mabadiliko tunayafanya kwa maridhiano ya kisiasa na hatutaki vurugu
Kwani ninyi ni kina nani?

"Mwongozo kidogo kwenye utambulisho wenu usiotuhusisha sisi wengine tusiofurahi wanavyolelewa wabadhirifu, ingependeza zaidi."

Hii ni kwa sababu tunajua huo wenu ndiyo ulio msimamo wa walamba asali, wahuni au hata wale vijana wa hovyo.
 
Maana wengine wamezoea vurugu

Vurugu? Jina hilo huitwa kutegemea umesimama upande upi.

Wengine tunaona walamba asali, wahuni na wale vijana wa hovyo ndiyo wanaotaka vurugu.

Screenshot_20230322-230708.jpg


Kwani wewe uko upande upi hapo?
 
Dini zote ni zipi ndugu?

"Mormoism, Judaism, Buddhism, unitarianism, Islam, Scientology, Jewish, ... ?"

Zote isipokuwa christianity??!!--- read the question again.
 
Back
Top Bottom