Elections 2015 Ni Tundu Lissu pekee(Sababu moja sifa kumi)


Vyumba vya madarasa sio issue mkuu!Kwa historia baba yake na Lissu aliwahi kuitoa nyimba yake iwe shule ya msingi.

Unachangisha wananchi maskini kujenga maabara wakati kodi yao halali inaliwa na singasinga hui ndio upuuzi asioutaka Lissu.

akichukua nchi hii michango ya kipuuzi ndio mwisho wake.
 
lisu ni kiongozi mzuri sana but anafaa awe MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI uraisi hatouweza yupo strict sana na raisi anatakiwa awe flexible sometime.

katika maamuzi namfananisha na magufuli kabisa but even magufuli awezi kuwa raisi kutokana na kuwa na kaliba zinazofanana.

doctor slaaa
lipumba.
mbowe.
lowasa
kidogo wanaweza kuvaa hivyo viatu ya uraisi wa TZ
 
Tundu lisu mzuri sana.. Anafaa kuwa Waziri mkuu. uraisi unamfaa LIPUMBA au MBATIA. Hata MBOWE anafaa kuwa rais tatizo hawa wote hawana popularity kama ya TUNDU LISU. tunawaomba Ukawa wasituletee tena Dr Slaa kuwa kuwania Urais maana ki ukweli ameshachoka. Japo Mwai kibaki nae alikuwa mzee lakini aliiletea kenya maendeleo makubwa. Watanzania hawapendi wazee dizain ya Dr Slaa.
 
Naunga mkono hoja,hakuna atakayeweza pambambana na Lowasa kama chama chake kitamuweka na bila shaka CCM hawana mtu zaidi ya Lowasa. kwa sababu zifuatazo sio lengo langu kuongeza topic bali jamaa anasifa tosha!
1. Lisu hatoki kaskazini ,ambayoni dhana ya UKASKAZINI hivyo kutoa upinzani.
2.Hana kashfa
3.Anaelewa out of Box. Zaidi maana hajawahi ajiriwa na serikali hivyo anawakisha the true story. Of Tanzania life.
4.Hajawahi kuwa MCCM hivyo ni askari Royal,si rahisi kutumika na CCM kama Msaliti wa Mageuzi Mrema
5.Ni kiongozi mwenye maamuzi magumu kama ya Lowasa ambayo ndio sifa ya Lowasa kama alivyosimamia kumtosa rafiki yake Zitto hadi mahakamani
6.Anatoka katika kabila dogo ambalo haita athiri utaifa.
7.Ana elimu ya Philosoph ambayo
hutafuta ukweli bayana maana aliweza kuhoji makosa ya Nyerere 8.Ni mtu pekee atakaye weza kurudisha uhuru alio uleta Nyerere maana kama mali zote zimeibiwa kwa mikataba mibovu,Lowasa hawezi chunguza Richmond!
9.Lisu anakubalika na dini zote maana hata majina yake hayaakisi saana dini kwa wapigakura
10.Aliweza kurekebisha sheria ambayo hata rais alidanganywa na Bunge,amebobea sheria
11.Lowasa ni tajiri,hata akijaiba hakuna atakaye hoji,lakini Lisu maskini ni maskini rahisi Kuhoji.
 

kwa jinsi unavyo muona lissu anaweza kuwa na gentleman?
unadhani akiwa rais anaweza kubaki uprof wa kupewa?

naona anafaa kuwa president.ila jazba ndo shida
 
kwa jinsi unavyo muona lissu anaweza kuwa na gentleman?
unadhani akiwa rais anaweza kubaki uprof wa kupewa?

naona anafaa kuwa president.ila jazba ndo shida

Kwa Tanzania yetu ilipo sasa Mimi naona jazba ni sifa nzuri itakayosaidia kudhibiti mafisadi, lakini itatuma meseji kwa would be mafisadi kuwa ukiiba inakula kwako fasta bila kuremba kama CCM inavyowaremba mafisadi.
 
Tundu lisu tumpe miaka mitano mbele akomae vizuri kwa sasa Dr slaa anafaa kabisa mtu yeyote aliye wai kukaa na doctor karibu akaona utendaji wake wa kazi Kama Mimi awezi kusita kusema doctor apewe nchi mwaka huu.
 
Lisu anafaa kuwa rais wa nchi hii, nafasi yake bungeni kama mwanasheria itazibwa na nguli wengine akina Peter Kibatala
 
Lisu anafaa kuwa rais wa nchi hii, nafasi yake bungeni kama mwanasheria itazibwa na nguli wengine akina Peter Kibatala
 
You're spot on,bra!Hilo la kuungwa mkono na dini zote ni muhimu sana,La kutotoka Kaskazini nalo lina umuhimu wake,Jambo la kusikitisha baadhi ya WanaCHADEMA watapinga wakiamini Slaa naweza kuongoza.Hata miye ningependa sana Slaa awe rais kwasababu ana sifa.Tatizo linakuja ktk uhalisia wa siasa za Tanzania, Candidacy ya Slaa itawagawa wapiga kura zaidi kuliko kuwaunganisha hasa linapokuja kwenye suala la udini.Tundu Lissu remain a safe choice to me,He is a lesser of the two evils to the Muslims.
 
Ni sahihi kam mleta mada livyosema,lakini nadhani mua wake utafuata baadaye. Kwa sasa kama UKAWA watapata nafasi a kwenda Ikulu basi,yeye anapaswa kupewan nafasi ya Waziri wa Shera ama Attoney General
 

Mkuu kwa miaka hamsini ya uhuru tumekuwa tukiongozwa na hiyo the so called 'flexibility' huu ni muhula wa kuturejesha kwenye mstari tukishanyooka tutamleta Rais aliye flexible.

Hawa wote uliowataja hapo chini ni wastaafu au pensioners kwa mujibu wa sheria.Nchi inahitaji kijana mwenye nguvu kutuvusha.Urais isiwe pango la kutunza wazee wastaafu.
 
Ni sahihi kam mleta mada livyosema,lakini nadhani mua wake utafuata baadaye. Kwa sasa kama UKAWA watapata nafasi a kwenda Ikulu basi,yeye anapaswa kupewan nafasi ya Waziri wa Shera ama Attoney General
Lissu ni chaguo sahihi strategically kama CHADEMA inataka kushinda mwaka huu,Slaa is a wrong choice strategically. CHADEMA need to win this election and Lissu is a shoe_in Presidential candidate.
 
Busara ndo zimetufikisha hapa mkuu!vielelzo vya dawa za kulevya vinabadilika na kuwa unga wa nafaka aina ya ngano! Pombe ya gongo hugeuka na kuwa maji au mafuta ya taa kwenye vituo vyetu vya polisi ! Mtoto wa shule x hufundishwa kuwa kuna sayari tisa na aliekuwa shule y anaaminishwa kwa kufundishwa kuwa zipo kumi kwenye nchi moja! Busara hizo ndo ziliruhusu 75 bil za escrow zitoke taslmu kinyume na sheria za nchi na za kimataifa busara hizoooo ! Ushindwe na utakomee zako
 
Mzee Slaa hafai Tena?

Kuna kijana gani ndani ya ccm atakayeweza kusimama na Lissu?

Wapiga kura wengi wa mwaka huu ni vijana nafasi ya mzee iwe kwa UKAWA AU CCM haipo.
 
Tundu lisu hana masters ana degree tu, pia hawezi wala hana sifa ya kuongoza nchi, amejaa matusi tu kichwani hafai kwa matumizi ya umma
Ni wapi na lini Tundu Lissu alitukana?
Kwa nini hakuchukuliwa hatua?

Tusiwe waoga na tusilete propaganda za kitoto.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…