Elections 2015 Ni Tundu Lissu pekee(Sababu moja sifa kumi)

Elections 2015 Ni Tundu Lissu pekee(Sababu moja sifa kumi)

Mwaka huu ni wa Singida.

Lakini kati ya Mwigulu, Nyalandu na Lissu, bingwa anajulikana kuwa ni Lissu. UKAWA wakimsimamisha huyu mtu hata mimi nitapiga kura. Kuna jambo watu hawathubutu kulisema - Dr. Slaa amekwishajaribu vya kutosha. Inafaa apumzike kwa sasa japo tunampenda sana.

Nichukieni wa kunichukia lakini ukweli nshasema.


Sasa wewe ndo utanifanya niseme!
CHADEMA HAINA RAIS ZAIDI YA SLAA, MAANA HATA SISI MAGAMBA TUNA IMANI NAE!
WATU KAMA LISSU NI SAWA NA VILE VIASKARI VYA 'UNDER 18'! NI VIZURI MNO VIKIPEWA AK 47 MAANA VINAUA BILA KUULIZA NA KUJUA KWANINI VINAUA, SHIDA INAKUJA VIKIPEWA KUONGOZA MAPAMBANO!
 
Kwa nini mkuu?
Umeorodhesha sifa za Lissu vizuri sana, lakini hiyo namba 7 imechafua. Hiyo ndiyo ilitumiwa kama turufu ya MM na kina Tuntemeke kwenye vikao vya mikakati yao ya mapinduzi ndani ya chama. Sioni kama ujana ni sifa muhimu kwa rais mtarajiwa.
 
Sasa wewe ndo utanifanya niseme!
CHADEMA HAINA RAIS ZAIDI YA SLAA, MAANA HATA SISI MAGAMBA TUNA IMANI NAE! WATU KAMA LISSU NI SAWA NA VILE VIASKARI VYA 'UNDER 18', NI VIZURI MNO VIKIPEWA AK 47 MAANA VINAUA BILA KUULIZA NA KUJUA KWANINI VINAUA, SHIDA INAKUJA VIKIPEWA KUONGOZA MAPAMBANO!

Kwa kuwa Slaa alikubali ombi la baba askofu?

Nisome mwanzo kabisa utaelewa msingi wa hoja yangu.Nimependa huo mfano wako kwani kwa mustakabali wa nchi hii kwa sasa tunahitaji hiki kiaskari kidogo kinachoua bila kujiuliza kwa sababu Kamanda aliyetegemewa kutuongoza ameshakufa,kinachotakiwa ni kujinasua na kujipanga upya.

Tunahitaji kurudi kwenye mstari halafu tutarejea kwa hawa watu wa kiprotokali.

Hatutoki hapa salama bila ya mtu kama Lissu.

Dr Slaa yupo vizuri ndio maana tunaelezwa alishinda 2010 lakini akachakachuliwa.Mimi ningependa kumuona akimsimamia Lissu kuingia Magogoni na busara na influance yake itaendelea kutukuka kama alivyokuwa JKN.
 
View attachment 216678
angepewa nafasi ya kuwa mwanasheria mkuu wa serikali hawa wezi wangerudisha pesa zetu za escrow zote.
Akiwa rais anakuwa na uwezo zaidi wa kuzirudisha kama ana utashi kwani hatoingiliwa na mtu yeyote. Mwanasheria mkuu anaweza kuwa na nia rais akasema hapana.
 
Akiwa rais anakuwa na uwezo zaidi wa kuzirudisha kama ana utashi kwani hatoingiliwa na mtu yeyote. Mwanasheria mkuu anaweza kuwa na nia rais akasema hapana.
kwenye uraisi bado ana jazba sana .
 
Umeorodhesha sifa za Lissu vizuri sana, lakini hiyo namba 7 imechafua. Hiyo ndiyo ilitumiwa kama turufu ya MM na kina Tuntemeke kwenye vikao vya mikakati yao ya mapinduzi ndani ya chama. Sioni kama ujana ni sifa muhimu kwa rais mtarajiwa.

Pole kwa kukwazika!
Ni ukweli usiopingika kwamba dunia ya sasa inapita kwenye kipindi cha Umri fulani kuupisha umri mwingine.Ujana unataka kupishwa hivyo ni vyema uzee ukatambua hili....sio Tanzania tu bali duniani kote


Ukiangalia wagombea na wapiga kura kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa utaelewa ninachokisema.

Strategically Ujana wa Lissu ni added advantage.

Chukulia hivyo mkuu !!
 
Tundu lisu mzuri sana.. Anafaa kuwa Waziri mkuu. uraisi unamfaa LIPUMBA au MBATIA. Hata MBOWE anafaa kuwa rais tatizo hawa wote hawana popularity kama ya TUNDU LISU. tunawaomba Ukawa wasituletee tena Dr Slaa kuwa kuwania Urais maana ki ukweli ameshachoka. Japo Mwai kibaki nae alikuwa mzee lakini aliiletea kenya maendeleo makubwa. Watanzania hawapendi wazee dizain ya Dr Slaa.

Sema unamuogopa Dr.Slaa kiaina!!
 
Naunga mkono hoja, Tundu lissu ni chaguo sahihi kwa sasa, anakubalik na makundi yote nchini, annakubalika vyama vyote. Ni kijana hivyo ni nguvu ya mabadiliko.

#GOODMORNING
 
Tundu Lissu ana advantage nyingi sana,ni handsome pia,akina mama wanapenda ma_handsome boy.Hicho ndicho kilichomsaidia JK,Ila Lissu ana akili
 
Wanajamvi habarini!

Niliweka post hivi majuzi na kuahidi kurudi tena na kuelezea kwa nini nimeamua kushawishi umma wa Tanzania ya kwamba TANZANIA ya leo inamuhitaji Tundu Lissu kama mwajiriwa mkuu wa wananchi.

wakati umefika na wakati ndio huu!

Utangulizi:

Nikijikita katika mada moja kwa moja napenda kusema kuwa Tanzania ya leo sio Tanzania ya Nyerere,hapa namaanisha sio Tanzania yenye maadui watatu yaani Ujinga,Umasikini na Maradhi...maadui hawa walishadhibitiwa usiniulize lini au na nani bali tulie tuelezane.

Watanzania wa leo wana elimu bwana...watu wanatumia simu,TV na teknolojia za kigeni bila shida.elimu ya msingi kwa sasa ni kidato cha nne,maelfu kwa maelfu ya vijana wako vyuo vikuu.hivyo sitarajii kumsikia mtu akilalamika juu ya watanzania kupata elimu iwe bora au hiyo hiyo ya kuungaunga...Adui alikuwa ni upatikanaji wa elimu na sio ubora wake!!!

Swali la kujiuliza jee elimu hii wanayopata vijana wetu hasa ile asilimia 75 ya wakulima na labda kwa kuongezea asilimia 10 ya wafugaji inafanana na ile wanayopata asilimia chini ya kumi ya tabaka la viongozi/masingasinga na washirika wao?

Hivi hii elimu waliyopewa watoto wa mbwa imelenga kuajiriwa au kujiajiri?

Watanzania wa leo sio maskini bwana.mabarabara ya lami kila kona,umeme vijijini wa kuwasha taa tu(wanakijiji wataanza kuchelewa kulala).Watu wanamiliki simu,toyo na mafundi cherehani wa sikuhizi hawajui kuweka viraka.Ukiongelea msosi hii sio issue tena kwani siku hizi hakuna kupanga foleni ya mkate huku kuna skonzi za Azam.

Umasikini hakuna tena...naam

Watanzania wa leo hawaumwi kipindupindu,Ukoma,vikope n.k watanzania wa leo wanaumwa dengue,B.P na rare cases kansa ya Tezi....
Isitoshe kuna zahanati au kituo cha kutoa huduma za afya kila kijiji.Adui alikuwa ni upatikanaji wa huduma za afya sasa zipo.

Jiulize sasa huduma hizi za hospitali hata ile zahanati kuu ya Muhimbili zinakujia kwa hisani ya nani?Jibu lako kaa nalo.

Wakuu msichoke naendelea na utangulizi.

ADUI WA TAIFA HILI NI YUPI HASWA KWA SASA??

Kabla sijamtaja ningependa kusema kuwa inawezekana miaka yote tuliyofanya uchaguzi hatukuwahi kuwa na ajenda kama taifa bali tuliendelea kuimbishwa kama kasuku kuhusu maadui hawa watatu.Sasa
ni wakati muafaka tukaingia kwenye uchaguzi huu tukiwa na ajenda ya pamoja.

Adui pekee aliyebaki Tanzania ni UFISADI...yaani huyu ndiye kubwa la maadui .Hata hayati JKN hakustuka au aliunderestimate uwezo wa Adui hili na ndio maana leo hii limekuwa kubwa la maadui.

Tanzania ya leo inakwamishwa na Ufisadi ama mfumo na mtandao wa kifisadi unaokuwa kwa kasi.....

Vijana wanakosa mikopo ya kusoma vyuo vikuu mpaka wanasingizia wazazi wao ni vilema au wafu ili tu wapate mkopo ilihali kuna mafisadi wamehifadhi vijisenti uswisi.

Madawa yanakosekana katika zile zahanati za kila kijiji ikiwemo ile zahanati kuu kisa ni madeni au labda watu wanataka kujipigia 10%

Kwa ufupi ufisadi ni janga janga janga la kitaifa kwani hata umeanza kukidhihirisha makanisani.

Tunahitaji kuwawajibisha,kuwachukia na ikiwezekana kuwapoteza.

Kazi hii hahitaji mtu legelege bali mwenye dhamira na tabia isiyokoma ya kuwa na misimamo isiyoyumba....Hii ndio SABABU MOJA YA KUMPA LISSU KIJITI KWA TIKETI YA UKAWA.

Tunapomkabidhi Mama Tanzania tumwambie kazi yako ni moja tu ya kutuondolea ufisadi na mafisadi.

Kama ni viongozi tunao tunachohitaji ni kuwaondoa viongozi wenye nasaba za kifisadi.

Kama ni madaktari au waalimu au majaji wapo na tutaendelea kuwapata lakini tunahitaji kusafisha watumishi wote wenye genes za kifisadi.

Hatuna uhaba wa maafisa ugavi au wahasibu wanaoshiriki ufisadi tunahitaji kuzalisha wagavi au wahasibu waadilifu n.k n.k

SIFA KUMI ZA TUNDU LISSU KWA MUKTADHA WA HOJA HII

1-Tundu Lissu ni mkweli kwa kimombo yuko Honest.mara nyingi hujiweka wazi katika misimamo yake na hivyo kuwafanya wake kumuelewa na wao kuamua au kuchukua upande.Kijiko hukiita kijiko na sio beleshi dogo!

2-Maono/Malengo yaliyonyooka ama kwa kimombo niseme anaweza kufocus.
Kama uliwahi kumsikiliza bungeni basi utajua hajaikosa hii tabia kwani hata panapotokea distractions kama vile kutukanwa basi yeye hubaki katika mstari na kuendelea kukifafanua au kukifikia kile anachotaka.

3-Heshima kwa utu.Toka mwanzo wa siasa/harakati Tundu lissu amejikuta akipambania utu wa mwanadamu,rejea harakati za migodini.

4-Uwezo wa kujenga hoja na kushawishi.
Hili ni jambo muhimu kwani ukienda Zanzibar Tundu Lissu ameweza kuwavutia wazanzibar mpaka kupachikwa jina la Messi wa Ukawa.Naweza kusema hakuna kiongozi kutoka bara tena mkiristo anayeweza kuwa na ushawishi kwa upande wa zanzibar isipokuwa TL.iwe ndani au nje ya UKAWA.

Na hii ndio turufu muhimu kwa UKAWA kwa wakati huu.

5-Ujasiri
Tundu lissu hajawahi kuogopa especially kuwaogopa mafisadi.

6-Ujuvi au labda kwa lugha ya malkia niite Arrogance.Arrogance ni tabia isiyopendwa na wengi lakini Tabia hii ndio inayohitajika pindi unapopewa kazi ya kipambana na mafisadi papa na watumishi wajuaji.

pia ni sifa hii inayohitajika pale utakapokutana na mataifa makubwa yanayotaka kunyakua rasilimali za nchi hii.

7-Ni kijana na bado ni mkakamavu.

8-Ni mwanasheria nguli anayejua kucheza na sheria na hiki ndio kiama cha mafisadi kwani watafilisika kwa kukodi mawakili wa kupambana na Rais mwenye dhamira ya kuwanyoosha.

9-Ameishi na kukulia katika umasikini.Amekumbana na kuchukia dhahma za kuchangishwa michango ya kipuuzi huku kodi zikiliwa na mafisadi.

10-Anajifunza na kucope na mazingira kwa haraka.Uwepo wake ndani ya bunge baada ya Dr Slaa kuondoka umekuwa ni chachu ya mabadiliko nchini.


Nimalize kwa kusema kuwa Tundu Antiphas Mughwai Lissu ni aina ya kiongozi anayehitajika kwa sasa.Tuungane kutokomeza ufisadi.

Kimsingi Tundu Lisu niMZALENDO ambaye ningependa awe moja ya viongozi wakuu wan chi hii. Hata hivyo,yafaa awe WAZIRI MKUU. Na Baraza kuwa hivi:
Rais, Dr SlaaWaziri Mkuu: Tundu Lisu,Mwanasheria Mkuu: Mnyika Waziri wa Mambo yaNdani: LemaWaziri wa Fedha na Uchumi:Prof. LipumbaJaji Mkuu: ……Waziri wa Katiba naSheria………….Nishati na Madini……………………Waziri wa Afya………………………….Waziri wa Ulinzi………………………….Waziri wa mambo ya njena Ushirikiano wa Kimataifa………………….Waziri wa TAMISEMI…………………………………………………….
 
Tundu lisu mzuri sana.. Anafaa kuwa Waziri mkuu. uraisi unamfaa LIPUMBA au MBATIA. Hata MBOWE anafaa kuwa rais tatizo hawa wote hawana popularity kama ya TUNDU LISU. tunawaomba Ukawa wasituletee tena Dr Slaa kuwa kuwania Urais maana ki ukweli ameshachoka. Japo Mwai kibaki nae alikuwa mzee lakini aliiletea kenya maendeleo makubwa. Watanzania hawapendi wazee dizain ya Dr Slaa.

Hamna mtu mwenye sifa nzuri kama Rais mteule Dr. Slaa. Mugabe ana miaka 90s na Dr ana nusu yake.
 
Pengine si wakati muafaka kumtaja raisi kupitia UKAWA, lakini nashindwa kupambana na na hoja yako kuhusu LISSU, Anaweza na huonekana ana dhamira ya dhati, na kwa kuwa taifa hili lina tatizo la makusudi la kisheria kama mikataba ya hovyo, kwa kiongozi kama Lissu amabaye ni mjuzi wa sheria itakuwa poa sana, umejitahidi kutuaminisha na ukweli ni kwamba kila kitu kipo ila vinaatumiwaje kumalizia tatizo la ujinga, maradhi na umaskini? jibu ni ufisadi ndio kikwazoo kikubwa.
Ukimpima Lissu na Jk, Lissu anaonekana ana dhamira na malengo, jazba huja mara tu anapotukanwa hasahasa anapoguswa binafsi na si hoja zake, pamoja na hilo hujichukulia mtu wa kawaida sana, tofauti na vingozi wanaopenda kujikwaza (wale wanaopenda kuitwa waheshimiwa), anajua wajibu wake na kufuata maelezo kwa kadri taaluma aliyonayo inavyomtaka awe, naamini akiwa raisi wa taifa hili atatimiza wajibu na yote ambayo watz tunategemea kutoka kwa kiongozi huyo mkubwa. Anafaa na anastahili.
 
Atawafunga ccm wote,ila ndo kwa sasa mtu anyefaa airudishe nchi katika mstari yupo opposite ya mzee wa msoga kabisa katika maamuzi.
 
Pengine si wakati muafaka kumtaja raisi kupitia UKAWA, lakini nashindwa kupambana na na hoja yako kuhusu LISSU, Anaweza na huonekana ana dhamira ya dhati, na kwa kuwa taifa hili lina tatizo la makusudi la kisheria kama mikataba ya hovyo, kwa kiongozi kama Lissu amabaye ni mjuzi wa sheria itakuwa poa sana, umejitahidi kutuaminisha na ukweli ni kwamba kila kitu kipo ila vinaatumiwaje kumalizia tatizo la ujinga, maradhi na umaskini? jibu ni ufisadi ndio kikwazoo kikubwa.
Ukimpima Lissu na Jk, Lissu anaonekana ana dhamira na malengo, jazba huja mara tu anapotukanwa hasahasa anapoguswa binafsi na si hoja zake, pamoja na hilo hujichukulia mtu wa kawaida sana, tofauti na vingozi wanaopenda kujikwaza (wale wanaopenda kuitwa waheshimiwa), anajua wajibu wake na kufuata maelezo kwa kadri taaluma aliyonayo inavyomtaka awe, naamini akiwa raisi wa taifa hili atatimiza wajibu na yote ambayo watz tunategemea kutoka kwa kiongozi huyo mkubwa. Anafaa na anastahili.
 
Tatizo lingine la lissu ni kwamba, anaweza kuharibu kabisa confidence ya mahakama kutimiza wajibu wake bila kuingiliwa. Lissu ni mtu ambaye haziamini kabisa mahakama zetu.

Akiwa rais anaweza kulazimisha Mahakama ziwe chini ya ofisi ya Rais, kitu kitakachotuingiza matatani na nchi wahisani.
 
Acha mambo ya ajabu mbona hao wanaotaka kugombea urais hujaitaji matokeo yao ya shule hizi ni chuki binafs
 
Back
Top Bottom