Ni udanganyifu gani ulishawahi kuufanya katika chumba cha mtihani ulipokuwa mwanafunzi?

Hehehe ila mwamba alikua vyema yaani anaibia kwa kuangalia pen tu Kuna watu wapo vyema
 
Design hii utakuta wameshika nafasi nyeti za maamuzi katika nchi. Kwa ujanja huu Kwa nini wasitupige Hawa. 😁 Aisee.
 
Sijawahi fanya udanganyifu wowote ndo maana Nilifeli
Mimi kitu kama sijui naacha wazi ila kusema niombe majibu au niibie hio hapana! Huwa nawashangaa sana wazazi wa skuizi wanawajibia watoto home work wallah mimi nakuacha ukakose afu ndo uje nikufundishe! Shugulisha ubongo Hii tabia ya kuiba majibu ndio mbegu ya kuwa tegemezi! Ukikua inamea mpaka kwenye maisha ya kawaida unakua bila msaada huwezi kabisa!
Mimi wallah kuliko niige majibu ilikuaga heri nikose nifeli tu na nmewahi feli mara moja tu 😅
 
Mlitisha sana hii hawachomoki wasimamizi
 
Siyo mzuri kuiga. Kama sijui ndiyo imepita hiyo.

Wakati nipo la 6 tukiwa kwenye mtihani mwalimu akakuta daftari lipo kwenye dawati, yule mwalimu akaniambia nitoke nje. Nikamwambia daftari siyo langu, lile daftari hata jina halikua langu lakini akakomaa kunitoa nje.

Nikatoka nikanyoosha nyumbani huku nina hasira, nikamwambia mzee kilichotokea akajibu tu sawa.

La tatu ilikua shule yetu inagawanywa shule ileile moja zinatengwa zinakua mbili. Ila mtihani ndiyo unaamua mwanafunzi gani aende wapi.

Nikampa mtu chabo. Kwenye mtihani wa jumla akawa wa tano na zawadi akagewa, mimi kwa kuona ndiye mtoa chabo nikasubiri zawadi yangu nikajikuta ni wa 11.

Huyu mwana tukaenda wote shule mpya, na kwa ile nafasi yeye ndiye akaonekana genius wa shule mpya. Akagewa ukaka mkuu 😅😅😅

Kilichofuata sisemi
 
3 Idiots
 
Mimi bahati mbaya nilikuwa si haba vi B na A ni kawaida. Baada ya kujitambua kuanzia darasa la tano, Principle yangu ilikuwa sifichi paper la mtihani, kama unaweza angalia ila siwezi kufanya jitihada za kukuonesha pia, kwahiyo wafaidika wa mfumo walikuwa watu wa karibu ya dawati tu.

Kama unataka njoo nikufundishe nachokijua Mimi. Pia nilikuwa na uwezo sijui nikawaida au wa ajabu. Nilikuwa najua uwezo wa wanafunzi wote darasani, yaani nilikuwa na uwezo wa kujua katika mtihani hili swali fulani na fulani tu ndio watapata. Kwa hiyo nilikuwa naweza jua hapa naongoza au kuna mtu atanizidi marks hasa kwenye hesabu.
 
Okay kuna siku tumeingia kwenye pepa la Mathe, Ticha kaanza kugawa pepa kwa mwanetu mmoja yeye alikaa mwanzoni kabisa. Yule mwana alivyopewa pepa akapitisha macho chapu afu akatugeukia masela kule nyuma akibusu ngumi kuashiria pepa ni jepesi kinoma.

Kuja kupewa pepa swali jepesi ni la Quadratic Equation. Nikasikia mwana mmoja analaani kwa sauti ya chini "huyu mtoto anakatwa kweli."
 
Nilivujishiwa pepa la physics form two!, usiku nipo nimetulia simu hiyo nikakurupuka kitu kinakuja swali na jibu! mengine hayana majibu uta solve mwenyewe, mpk kufika saa kumi mtihani wote huu hapa hapo ni kukariri majibu tu halafu maswali baadhi nikaandika kwenye karatasi nikatimba nayo shuleni. lengo halikuwa kuingia na ile pepa ilikuwa ni kuhakiki mpk dk ya mwisho nimeweka kila kitu kichwani na nikakumbuka nina rafiki zangu pia!.

so nilichofanya ili kupunguza attention zimebaki kama dk 20 hivi kuingia kwenye chumba cha mtihani nikawafata marafiki zangu nikawaambia chukueni hii mtakutana na haya maswali, waka solve chapchap nami nikiwepo walipomaliza nikaichukua ile karatasi nikaitafuna! kupoteza ushahidi maana ulikuwa muandiko wangu lingetokea lolote ingekuwa tafrija yakujitakia.. baada ya mtihani kila mtu ananifata (wale niliyowapa pepa) wananiuliza nilijuaje yale maswali yatatoka!! mi nikawa natabasam tu pepa zilizobaki wakawa wananifata wananiuliza vipi tupe nondo..🤣
 
Aisee hizi shule kubwa kama Ilboru paper zinavuja,sisi Advance tunatafuta masela walioko Ilboru,Tabora Boys na kwingineko wanatupa maswali usiku na kesho unakutana nazo kweli, hizi shule zinazocheza kumi bora kuna ujanja mwingi sana kama una marafiki huko somo moja litavuja tu.
 
Kuna wana wameingia kwenye pepa hawajui kitu ikabidi waandike kikaratasi wampasie mwamba mmoja ambaye kichwani zinachaji. Tatizo la yule jamaa mizaha ni mingi sana.

Sasa imagine msimamizi mkaksi kinoma halafu wana wamefosi kupitisha kikaratasi kutoka kule nyuma hadi kimefika mitaa ya kati.

Jamaa akakipokea akaangalia maswali waliyoomba kusaidiwa, akaanza kuandika. Alivyomaliza akikunja kama kawaida akitafuta mazingira mazuri kirudi kwa walengwa.

Kikaratasi kimerudi wana kufunua wakakukutana na hiki kitu, "KWANINI HAMKUSOMA?".
 
Kuna pepa la Necta tulivujishiwa. Sasa tukajikusanya wote tukawa tunasolve. Wengine wakaenda mbali zaidi wakaona kukariri majibu changamoto wakawa wanaandika nondo waingie nazo. Furaha ilikua kubwa maana ni uhakika lile pepa.

Sasa kuna mwana mmoja sijui kuzidiwa na furaha hadi akaropoka shetani niongoze huku akiibisu nondo yake.

Guess what, alikamatwa na msimamizi zikiwa zmebaki dakika 10 tumalize. Alivyodakwa yule msimamizi akawa anasogeza mapepa ya jamaa wa pembeni maana naye alitakiwa aweke saini kama shahidi. Tukasikia shahidi anang'aka, "hapana ticha nitasaini hapa hapa.", huku akidhiti vizuri karatasi zake. Kumbe shahidi naye alikuwa na nondo chini ya zile karatasi za mtihani. Ilibaki kidogo.
 
Enzi hizo sekondari kipindi cha mtihani wa taifa tulibahatika kupata msimamizi aliekuwa peace kweli. Ndipo tukamshwawishi atuvujishie pepa kwa gharama ya 5M tulio changa kijiji kizima.

Mitihani yote tuliofanya kweli maswali yalikuwa yaleyale kama tuliovujishiwa na kudiscuss. Shida ikaja kwenue pepa la mwisho ile kufunua tu maswali yote ni tofauti kabisa. Nyuso za kila mmoja zilikunjamana maana hatukusoma tulitegemea kitonga kingeendelea. Ndipo uvumilivu ukamshinda Peter Bhatazaar na kuamua kuropoka kwenye chumba cha mtihani "mbona tumekupa Pesa ya maana alafu unatupa kitu kisicho chenyewe"
Patashika ilioendelea hapo haielezeki. Kwa ufupi tu. Hivi sasa mimi ni bodaboda na uyo Peter ni mvuvi
 
Hii ni ngori.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…