Ni uongo upi usio na mantiki umewahi kutana nao kwenye Bongo Movie?

Ni uongo upi usio na mantiki umewahi kutana nao kwenye Bongo Movie?

Watanzania ni watu wazarendo sana kwa vitu vilivyo vya kwao! Lakini inafikia mahali wawasilishaji wanaviwasiliaha kimakosa!

Uwanja pekee ambao kwa sasa umefifia na uko karibu kufa ni katika tathnia ya filamu za kitanzania (maigizo), walibaki wakina mama kuwa watazamaji na mashabiki wao! Lakini kwa sasa na wao wamehamia kwenye series za kikorea!

Huwezi amini kuwa makosa kwenye tathnia hii yalikuwepo hata kipindi cha uigizaji wa Steven Kanumba! Japo kwa asilimia ndogo sana!

Twende kwenye kiini
Tufahamishe uongo wowote uliokutana nao kwenye bongo movie ambao ulikukata stimu za kuendelea kuzifuatilia!

Kwa kuanzia, mtu kuflash back na kukumbuka matukio yaliyofanyika ambapo yeye hakuwepo! Mtu anakumbuka, halafu kwenye tukio hayupo!
Tunajenga kwa pesa zetu by Mwendazake
 
Si mpenzi sana wa Bongo movies ila sometimes kuna mazingira huwa inatokea naangalia bila kupenda (mf; kwenye mabasi ya mikoani)

Huwa napenda sana kusoma subtitles za kingereza, kiukweli zina makosa mengi ya grammar na typing errors. Hapo ndo wanajinasibu wanataka waende kimataifa.! Bado tunasafari ndefu sana
 
Mimi ukiachana na maswala ya uongo ..nitazunguzumzia maswala ya makosa ya kiufundi kama editing n.k.

Kwa mfano cinematographic technique bado sana ...kumbuka hata mjongeo wa kamera katika kurekodi tukio huvuta hisia kwa mtazamaji.

Unakuta tukio labda la kukimbia ni kamera moja peke yake inatumika..hivyo kukosa baadhi ya angle kwenye scene.

Kwenye editing pia unakuta boom mic inaonekana. na mambo mengi kibao tu
Kamera ya kijinga Kama mark 3 ambayo hutumika na bongo movie nyingi unakodi kwa 50 kwa siku,lakini hata hivyo ulisema ukimbie nayo kumfuata muigizaju picha itacheza,hapa utahitaji gumbo,ambayo ni ghali,au dolly,ni ghali pia..bongo movie wanaungaunga hawana mitaji,so ngoma inabidi ipigwe chapu ili kupunguza gharama
 
Ndoto yangu siku moja kuwa na studio kubwa ya kutayarisha filamu (nina mpango wa kusomea ) ambayo italeta mapinduzi makubwa bongo movie.

Si zungumzii studio kama marvel huko mbali na pagumu Sana kufikia ,lkn kastudio flani ambacho kitazalisha movie zenye quality za kimataifa
 
Ndoto yangu siku moja kuwa na studio kubwa ya kutayarisha filamu (nina mpango wa kusomea ) ambayo italeta mapinduzi makubwa bongo movie.

Si zungumzii studio kama marvel huko mbali na pagumu Sana kufikia ,lkn kastudio flani ambacho kitazalisha movie zenye quality za kimataifa
Watakuja kina ray kwa kujiona masuper star watataka uwatengenezee bure ili wakutangaze.
 
Watakuja kina ray kwa kujiona masuper star watataka uwatengenezee bure ili wakutangaze.
Kama nipo hatua za mwanzo nitakubali (sio free kabisa) hili kutengeneza brand ,lkn nikashapata jina nitaaza kuwa expensive na Mimi and there will be nothing Free
 
Kama nipo hatua za mwanzo nitakubali (sio free kabisa) hili kutengeneza brand ,lkn nikashapata jina nitaaza kuwa expensive na Mimi and there will be nothing Free
Hata kama watatayarisha movie zao zenye uongo ndani yake!!? [emoji1][emoji1]
Kweli, aliye juu atabaki juu!!
Matokeo yake hako ka Studio kako hakatokuwa na maana tena ya mapinduzi!!
 
Mbona huzungumzii ile ,muandaji ,ray, muandishi,ray, directer ,rey, steling ,rey, yaani mtu mmoja anakuwa ameshiriki sehemu kibaaao hii pia inachangia sana kuaribu
 
Mbona huzungumzii ile ,muandaji ,ray, muandishi,ray, directer ,rey, steling ,rey, yaani mtu mmoja anakuwa ameshiriki sehemu kibaaao hii pia inachangia sana kuaribu
Hapo bado hujamzungumzia Tin White, anashiriki kila sekta, lakini kiuharisia unakuta ni photographer wa mabibo, tena mpiga picha za studio ndo anafanya mambo!!
Nchi hii ni ngumu sana! filamu za wenzetu zinaandaliwa na zaidi ya kampuni tatu! utakuta Syfy, Netflix humo humo, ma mabilioni ya pesa! na charachters wa kutosha!!
 
Kuonja sumu Kama imekolea .
Jini kuvaa jezi ya Barcelona.
Ndani usiku nje Mchana .
kuongea na simu na mtu wa mkoa afu unamskia chumba Cha 2.
 
Mchawi kaingia ndani ili amnyonye damu msukule wake halafu akawasha taa vili amuone [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kafungwa miaka 30 jela kwa kosa la kumpa ujauzito mwanafunzi! alivyomaliza kifungo wanaonesha mwanae analingana naye! Pia baba wa kijana aliyefungwa anakuja kumpokea akiwa amevaa nguo zilezile alizovaa miaka 30 iliyopita, kuanzia shati hadi viatu [emoji23][emoji23]
 
Huba imekosa reality. Matukio yamekosa ubunifu. In real life hayawezi kutokea.
 
Back
Top Bottom