Ni utapeli au napoteza bahati?

Ni utapeli au napoteza bahati?

Huu ujinga mbona unafanyika mda mrefu sana
Na matapeli wako Kenya
Akutumie iphone sawa mkuu
 
yaani unajaa kizembe hasa..mzigo ufike baada ya masaa 9 alafuwakutafute mapema hivyo...namba uliyipigiwa nahisi si ya kenya ...na ungepiga video call wasingekuwa airport
 
Kisa Changu Kiko hivi, Kuna mzungu aliniomba urafiki Facebook baada ya kumkubalia akaniomba namba ya Whatsapp. Tukaanza kuwasiliana ndani ya siku mbili tatu akaahidi kunitumia mzigo ambao ni simu ya iPhone 16.

Yeye anaishi London uingereza na siku aliyotuma mzigo alisema kuwa amekosa ndege inayokuja moja kwa moja Tanzania hivyo akatuma kwenye ndege inayoishia Kenya maana walimwambia kuwa mzigo ukifika wanaweza kufanya delivery uwanja wa ndege ulio karibu (hapahapa East Africa).

Basi bwana yule mzungu akatuma mzigo na akanitumia picha ya mzigo pamoja na risiti na zote Zina majina yangu maana aliniambia nimtumie majina yote matatu na namba ya simu, na akaniambia mzigo utafika Nairobi baada ya masaa 9 na akanisisitiza kuwa niwe Makini na muda kwani mzigo ukishafika watanijulisha na kweli baada ya masaa Tisa (mzigo aliutuma saa 2 usiku saa 11 ukawa umefika Jomo Kenyatta Airport Kenya).

Wale jamaa wa airport wakanipigia wakaniambia kuwa Kuna mzigo wangu wameupokea kutokea uingereza na umeshalipiwa Kila kitu ni Mimi kwenda na kitambulisho Changu tu nikauchukue.

Nikawaambia Mimi sipo Kenya nipo Tanzania Kama wanaweza kuutuma wautume. Kwa sehemu niliyowaambia wakasema inagharimu shilingi 125,000 ili mzigo ufike uwanja wa ndege niliopo.

Wamenionesha na picha ya mzigo kabisa ndio ule uliotumwa Kule uingereza. Sasa najiuliza hii kitu imekaaje? Maana wao wanasema mzungu kalipia mzigo mpaka pale ulipofikia Ila hizo gharama za kuja huku Tanzania ni gharama nyingine kwakuwa mzigo unatakiwa kukatiwa ticket na hiyo ni gharama ya ticket.

Na njia ya malipo wamesema naweza kutumia mpesa au Tigo pesa. Ndo najiuliza hapa nitumie au nakaribia kutapeliwa? Maana Sina uzoefu na upokeaji wa mizigo iliyotumwa kutokea nje ya nchi.

Nawasilisha wakuu. Naombeni ushauri wenu.
Anakupa iphone 16 kwa kazi gani uliyofanya? Jiulize kwanza hilo swali
 
Kisa chako ni kama changu tena mimi lilikuwa lishangazi ukweli alikuwa anaishi USA. Tulikuwa tunasalimiana kwa video call usiku nikiwa job tunaongea hata lisaa na watoto wake wa2 wakike wote mmoja mkubwa nadhani ndo alikuwa ananitosha mimi kwa habari ya mbususu.......

Muda ukaenda sana tunaongea nae nami sikuwa na tamaa na niliamini ni mtu sahihi .Basi akanimbia nitume accoun no anipe $26,000 daaah nikasema bahati hii hapa sasa.Kabla sijatuma nilikuwa na m47 ya mkopo kwenye account yangu ya crdb nikamuuliza bro akaniambia mpe yangu ....huyu bro nilikuwa namshirikisha sana hili swala hadi narekodi maongezi yetu namtumia anasema umepata asee.. baada ya kutuma ile no akauliza mbona majina tofauti?

nikamjibu acc yangu inashida kubwa akasema usijari hizo pesa nitatuma pamoja na mizgo mingine..... siku ya kutuma ulivyotoa maelezo ni hivyohivyo sema vitu ni simu3 zote iphone computer 4 (laptop) JBL (radio) nguo vifaa vya michezo na viatu nk yalikuwa mabox2 na hela hizo wakuu kipindi anafunga huo mzigo huku ana record video then akatuma.Alinimbia computer na simu nitawapa wazazi pia na wife.


Nilipata hamasa then akatuma ticket halafu muda sio mrefu akatuma mzigo upo airpot ya huko USA!
Baada y muda akasema nimewasiliana na watu wa huko watakuchaji kama 1.421,000/= kama ushuru hivyo utawapa hiyo hela nikamwambia sawa .....baada ya masaa2 nikatumiwa msg ""Habar bwana ..... tuna pend kukupa taarifa kuwa mzigo wako utafika hapa uwanja wa ndege wa julius k nyerere saa5 usiku hivyo tunakuomba uwe karibu kuja kupokea mzigo huo... "baada ya msg hiyo mzungu wangu naye akanitumia txt umewasiliana nao nikamwambia ndio
.

Basi mzigo ukafika airpot wakanipigia simu nami nikawaambia nipo mkoani hapo anakuja mtu kuuchukua na hiyo hela. Wakakomaa hela haitolewi cash tunaomba ulipe kwa no hii nikawaambia sawa pigeni picha mkiwa na huo mzigo hapo airpot kwa nyerere then nifanye malipo .....wakawa kimya kama lisaa then wakanipigia tena sauti ya mwanamke hapo nimelala na wife anasikia na nilikuwa nimemwambia juu ya neema hii njema wife akasema wee lipa tu uondoe usumbufu. nikamwambia hapana kesho dogo ataenda kuuchukua hapo halafu akifika na kupokea ndo nitalipa.


Baada ya kushindwa kulipia cha ajabu nilipolomoshewa matusi na jianaume linasema usipende vya bure maku wewe mkuyundu wako..Khaaaaaah halafu nika blockiwa chap yani hata mzungu wangu nae akaniblock vilevile


Nikawaaza sana hadi leo sijawahi pata jibu hii connection huyu mzungu alitoa wapi? Ikumbukwe nina uhakika alikuwa anaisha USA kwa 100% maana alisema ana viwanda na kweli alikuwa anapiga video call naona hata siku ananunua simu na hizo vifaa hadi nachagua rangi za nguo yupo USA hata kiwanja cha ndege ni USA!!

Ilikuwa nikiwa night huku job nae yupo kwake viwandani na niliongea na wafanyakazi wake 2 cha ajabu ni huyu mbogo kunitukania hadi ama yangu.Niliumia sana na kupigwa butwaa hapohapo kaka mkubwa nilikaa kimya hadi aliponiuliza vipi kuhusu mzungu wako? nikamwambia tapeli lile. Hadi picha za wazazi wake na clip fupi alinitumia hata mimi nikifanya hivyo na mambo mengine mengi .....Hii connectioni huwa wana toa wapi hawa watu ?

Manyanza Yoda
Ishanitokea mara nyingi hasa messenger hii ishu. Ukitaka kuwakomoa hawa waombe tracking number hapa ndio huwa wanapotelea hewani
 
Kuna watu wameshatepeliwa kwa staili hiyo hiyo. Waambie unataka kulipia wakupe account ya benki, ukiona wanang'ang'ania ulipe kwa simu watukane matusi yote
 
Ishanitokea mara nyingi hasa messenger hii ishu. Ukitaka kuwakomoa hawa waombe tracking number hapa ndio huwa wanapotelea hewani
Hta mimi sio huyo tu ila huyu ndo nilidumu nae kama miezi2 na wiki kadhaa. Swali langi connection na wabongo hutoa wapi maana kwa upande wa mzungu nilikuwa na uhakika100% kuwa ni kweli na kama ile no angetuma yeye direct nilikuwa nimeibwa asee. ila waliponicheki wabongo nikawa na mashaka mengi sana
 
Kisa Changu Kiko hivi, Kuna mzungu aliniomba urafiki Facebook baada ya kumkubalia akaniomba namba ya Whatsapp. Tukaanza kuwasiliana ndani ya siku mbili tatu akaahidi kunitumia mzigo ambao ni simu ya iPhone 16.

Yeye anaishi London uingereza na siku aliyotuma mzigo alisema kuwa amekosa ndege inayokuja moja kwa moja Tanzania hivyo akatuma kwenye ndege inayoishia Kenya maana walimwambia kuwa mzigo ukifika wanaweza kufanya delivery uwanja wa ndege ulio karibu (hapahapa East Africa).

Basi bwana yule mzungu akatuma mzigo na akanitumia picha ya mzigo pamoja na risiti na zote Zina majina yangu maana aliniambia nimtumie majina yote matatu na namba ya simu, na akaniambia mzigo utafika Nairobi baada ya masaa 9 na akanisisitiza kuwa niwe Makini na muda kwani mzigo ukishafika watanijulisha na kweli baada ya masaa Tisa (mzigo aliutuma saa 2 usiku saa 11 ukawa umefika Jomo Kenyatta Airport Kenya).

Wale jamaa wa airport wakanipigia wakaniambia kuwa Kuna mzigo wangu wameupokea kutokea uingereza na umeshalipiwa Kila kitu ni Mimi kwenda na kitambulisho Changu tu nikauchukue.

Nikawaambia Mimi sipo Kenya nipo Tanzania Kama wanaweza kuutuma wautume. Kwa sehemu niliyowaambia wakasema inagharimu shilingi 125,000 ili mzigo ufike uwanja wa ndege niliopo.

Wamenionesha na picha ya mzigo kabisa ndio ule uliotumwa Kule uingereza. Sasa najiuliza hii kitu imekaaje? Maana wao wanasema mzungu kalipia mzigo mpaka pale ulipofikia Ila hizo gharama za kuja huku Tanzania ni gharama nyingine kwakuwa mzigo unatakiwa kukatiwa ticket na hiyo ni gharama ya ticket.

Na njia ya malipo wamesema naweza kutumia mpesa au Tigo pesa. Ndo najiuliza hapa nitumie au nakaribia kutapeliwa? Maana Sina uzoefu na upokeaji wa mizigo iliyotumwa kutokea nje ya nchi.

Nawasilisha wakuu. Naombeni ushauri wenu.
Matapeli hao, achana nae. Nilishakuwa na rafiki nikaenda nae mpaka hatua ya kuniambia nitume kiasi ili nichangie mzigo kufika kupitia Nairobi.
 
waambie una kuja hapo Kenya, kuupokea mwenyewe [emoji23][emoji23].

Uki itwa kwenye fursa, jua wewe ndo fursa.
Ahahaha kuna mwanangu pia alishawahi kutana na hii akanishirikisha nikamuambia hawa matapeli utalia sio muda.

Anyway, ukikutana na suala kama hili ni simple, kwa kua mara nyingi hawa jamaa huwa ni wanaume ambao wanajifanya wanawake, we muombe umpigie video call muongee, hapa katu abadani hawezi kukubali kupigiwa video call.

Pili, omba atume location yake alipo kwa kupitia whatsapp live location, hapa pia hawezi fanya.

La mwisho, ukiambiwa uko wapi mwambie nipo Namanga, ambapo ni karibia na Kenya ,ukiaambiwa mzigo umefika we waambie ntaufata mwenywe ndani ya huo muda ntakua nishafika.


Kwa kesi ya yule jamaa angu alietaka tapeliwa, niliogelea matusi ya kutosha sana baada ya kumwambia mie nishakujua we tapeli[emoji1][emoji1]
 
Pia ndugu zangu wa Tanzania, kuna hawa matapeli wanaliza sana watu hasa FB na insta wengi wanatumia majina ya watu maarufu na mashuhuri kama Dr. TULIA, PM wa Tz Majaliwa, Nayce Moshi wa Tilisho, Nandy, Chief Godlove, Waganga wa kienyeji.

Hao wote hapo juu ni matapeli na wala hizo sio official accs za wahusika.

Wengi wao wanatangaza ajira za kazi na mikopo ya online.

1. TUKIANZA NA MIKOPO
Hapa utakutana na Tulia Trust mikopo online na majina mengine yenye tulia, utakutana Mo DEWJI foundation, TALA mikopo online and alikes.

Hawa wote wana operate the same, ukiclick link yao ambayo itakua imepostiwa aidha fb au insta itakuleta moja kwa moja whatsapp.

Huko sasa ukituma sms unapata auto reply ya kutuma majina matatu, picha 2 full, mkoa na kazi unayofanya.

Kama utakua mjinga ukatuma hivyo basi utaendelea na hatua nyingine ambayo utapewa kiasi cha riba au installment ambacho unaweka kama kianzio ili kupata mkopo. Mfano ,unataka milioni 1 weka kianzio cha laki 1 etc.

Ukikubali hiyo hatua, wanakupa namba then utafanya muamala. Baada ya hapo utasubiri hadi uchoke hutopata kitu na wata kublock.

Endapo utatuma picha na taarifa zako zingine,LAKINK ukashindwa kulipia aidha kwa kujua kuwa ni matapeli basi watatumia pichazako kukuchafua mitandaoni.

2. WATOA AJIRA
Hapa utakutana na Nandy supermarket, Nayce Moshi etc wao pia watatka taarifa zako kama hapo juu lakini watakutaka ulipie kama laki 1 ili ushonewe nguo za kazi then ukianza kazi utakuwa unakatwa mdogo mdogo. Kama ukawa tahira ukaingia kingi basi utaliwa kichwa na kula block.

3. MAOMBEZI NA KAFARA.
Hapa kuna Masanja mkandamizaji, Mwamposa, Chief Godlove etc. Hao pia huja na lugha za kichurch hurch kama vile karibu mwanangu nikuombee etc, watakutakuta utoe sadaka ili uombewe ukiwa bwege ukatoa itakua umechangia msosi boya mmoja wa pale Manzese ale.

Kwa kesi ya Chief Godlove, yeye anataka utoe admission fee ya 200k ili upate fomu na pete ya bahati. Ukiingia mkenge imekula kwako.

4. VITUO VYA WATOTO YATIMA
Kuna mmoja anajifanya anahusika na watoto yatima kuwaombea msaada mtandaoni. Ila ukitaka mgombane muulize kituo kikowapi uende kupeleka misaada physically au address ya sehemu kilipo HUTOJIBIWA.



NAMNA WANAVYO OPERATE
1. Wanakua na fake accs nyingi za kupost na kukoment wao kwa wao. Wengi wao wanakoment kwa kushukuru kuwa wamepataka kazi, wameponywa.

Chukua muda pitia hio timelines zao, hawana engagements za kutosha kama vile like, comments, posts pia wanakua na marafiki wachache sana.

2. Wanazuia kukomenti na pia ukikomenti kinyume na wao komenti yako inafutwa.

3. Hizo komenti nyingi ambazo ni za kwao lengo huwa ni kuwaaminisha umma kuwa wao ni legit hivyo mtu akiona anafanya hima kufata matakwa yao.


JINSI YA KUWABANA.
1. Ukifanikisha kuwacheki whatsapp ukafata maelezo yao, kabla ya kulipia omba upewe location ya ofisi yao. Hapa wengi watasema wana operate online hivyo hawawezi toa location ya ofisi na kama watatoa wengi watasema wako Nsalaga (Tulia mikopo) , Mo dewji (Dodoma uhindini), Posta ya zamani(Jokate mikopo) sasa wewe waambie wakutumie live location uweze kuwa track UTAKULA TUSI unawekwa block.



Kwa leo niishie hapa
Screenshot_20250126_133125_WhatsApp.jpg
 
Hta mimi sio huyo tu ila huyu ndo nilidumu nae kama miezi2 na wiki kadhaa. Swali langi connection na wabongo hutoa wapi maana kwa upande wa mzungu nilikuwa na uhakika100% kuwa ni kweli na kama ile no angetuma yeye direct nilikuwa nimeibwa asee. ila waliponicheki wabongo nikawa na mashaka mengi sana
Hao ni Matapeli wanakuwaga wapo Mikocheni tu hapo
 
Kisa Changu Kiko hivi, Kuna mzungu aliniomba urafiki Facebook baada ya kumkubalia akaniomba namba ya Whatsapp. Tukaanza kuwasiliana ndani ya siku mbili tatu akaahidi kunitumia mzigo ambao ni simu ya iPhone 16.

Yeye anaishi London uingereza na siku aliyotuma mzigo alisema kuwa amekosa ndege inayokuja moja kwa moja Tanzania hivyo akatuma kwenye ndege inayoishia Kenya maana walimwambia kuwa mzigo ukifika wanaweza kufanya delivery uwanja wa ndege ulio karibu (hapahapa East Africa).

Basi bwana yule mzungu akatuma mzigo na akanitumia picha ya mzigo pamoja na risiti na zote Zina majina yangu maana aliniambia nimtumie majina yote matatu na namba ya simu, na akaniambia mzigo utafika Nairobi baada ya masaa 9 na akanisisitiza kuwa niwe Makini na muda kwani mzigo ukishafika watanijulisha na kweli baada ya masaa Tisa (mzigo aliutuma saa 2 usiku saa 11 ukawa umefika Jomo Kenyatta Airport Kenya).

Wale jamaa wa airport wakanipigia wakaniambia kuwa Kuna mzigo wangu wameupokea kutokea uingereza na umeshalipiwa Kila kitu ni Mimi kwenda na kitambulisho Changu tu nikauchukue.

Nikawaambia Mimi sipo Kenya nipo Tanzania Kama wanaweza kuutuma wautume. Kwa sehemu niliyowaambia wakasema inagharimu shilingi 125,000 ili mzigo ufike uwanja wa ndege niliopo.

Wamenionesha na picha ya mzigo kabisa ndio ule uliotumwa Kule uingereza. Sasa najiuliza hii kitu imekaaje? Maana wao wanasema mzungu kalipia mzigo mpaka pale ulipofikia Ila hizo gharama za kuja huku Tanzania ni gharama nyingine kwakuwa mzigo unatakiwa kukatiwa ticket na hiyo ni gharama ya ticket.

Na njia ya malipo wamesema naweza kutumia mpesa au Tigo pesa. Ndo najiuliza hapa nitumie au nakaribia kutapeliwa? Maana Sina uzoefu na upokeaji wa mizigo iliyotumwa kutokea nje ya nchi.

Nawasilisha wakuu. Naombeni ushauri wenu.
Unapigwa mchana kweupeee, yaani huoni harufu ya utapeli hapo? Hizo mambo washaambiwa watu kibao. Halafu uliona wapi mtu anakuwa tajiri baada ya kumiliki iphone16?
 
Back
Top Bottom