Ni utoto, ujinga, ushamba na ulimbukeni kwa vijana kushindana kukimbiza magari ovyo ovyo mitaani

Ni utoto, ujinga, ushamba na ulimbukeni kwa vijana kushindana kukimbiza magari ovyo ovyo mitaani

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Kuna mtindo wa kitoto, kijinga, kishamba na ulimbukeni unaokuwa kwa kasi miongoni mwa vijana wa sasa kujivunia kukimbiza magari ovyo ovyo mitaani, yaani kuanzisha ligi na mtu yoyote wanayemkuta barabarani hususani safarini maeneo ya high way, akiwa anaendesha gari yake, basi ghafla hupambana kumpita ili kujivunia ukimbizaji wake na aina ya gari anayoendesha. Nasema hii ni tabia ya kitoto na hatari.

Yaani yuko tayari kununua gari fulani fulani ili aje kufanya hizo ligi zisizo rasmi barabarani halafu aje mitaani na mitandaoni kujigamba na kujitamba.

Yaani kijana kumiliki gari (wengine magari ya wazazi wao, marafiki nk) anataka kila mtu ajue ana gari, anajua kulikimbiza nk.

Sote tunajua barabara zetu zina watumiaji wengi tena ovyo ovyo, ubora na upana kwa sehemu nyingi ni mdogo, magari mengi ni mikweche iliyotumika na kuchoka huko Ulaya, Marekani na Japan kisha ikatupwa hapa nchini, sasa hizo mbio za nini?

Kama wewe unapenda kukimbiza magari nenda rasmi kwenye mashindano ya magari, huko kuna taratibu na kanuni zake, kashindane huko.
 
Hahaha nimekumbuka kitu tu..

Kamsafara fulani kama maV8 walijifunza kitu , Mjapan vs Mnyamwezi.
 
Kukimbiza kwenye makazi au misongamano ya watu hatari sana. Wanao wajibika na usalama barabarani wafanye jambo.. Mtu kama anataka kukiwasha yapo maeneo maalumu
 
Hasa vijana wasio na majukumu ya kifamilia ni vichomi sna
wengi wao hizo gari siyo zao km nizao huenda ni za mkopo!
Itoshe kusema kwamba hayo magari wameyajuli/wameyajuta ukubwani😄😄
 
Tafuta pesa boss, hutajua kabisa kama kuna vijana wanakimbizana na magari utakuwa busy na shughuli zako kataaa umaskini bro
Hii misemo na hizi mentality ni za maskini. Umejuaje kama jamaa hana pesa? Tafuta wewe wengine tunazo wala hatuzitafuti ila tumeshaweka mifereji mizuri sasa pesa zinatufuata tu.
 
Hii misemo na hizi mentality ni za maskini. Umejuaje kama jamaa hana pesa? Tafuta wewe wengine tunazo wala hatuzitafuti ila tumeshaweka mifereji mizuri sasa pesa zinatufuata tu.
Ujawahi kushika pesa ukajua state mtu anayokuwa nayo hawezi waza ujinga huu
 
Ugeni,ushamba,mizuka tu ya watumia vyombo vya moto wa sasa
Na sahvi asilimia kubwa ya waendeshaji vyombo vya moto wana ukichaa

Ova
 
Hii hali inakera sana,, niko mkoa flan hv ambao matajiri wa huu mkoa wengi wao n waarabu,, sasa hao watoto wa waarabu wanaendesha magari kwa speed kubwa, mbio afu wamekata exhaust kwa hyo znapiga kelele balaa!!! Kamji kenyewe kana barabara nyembamba!!!!!

Afu mm nafanyia kazi kat kat ya mji kabisa kwa hyo mda wote ni kusikiliza tu kelele za exhaust zao!!!
 
Hii hali inakera sana,, niko mkoa flan hv ambao matajiri wa huu mkoa wengi wao n waarabu,, sasa hao watoto wa waarabu wanaendesha magari kwa speed kubwa, mbio afu wamekata exhaust kwa hyo znapiga kelele balaa!!! Kamji kenyewe kana barabara nyembamba!!!!!

Afu mm nafanyia kazi kat kat ya mji kabisa kwa hyo mda wote ni kusikiliza tu kelele za exhaust zao!!!
😆😆😆😆
 
Namshukuru Mungu huku mjini naenda mwendo wa Serikali ila huko nje ya Mji nikiitafuta Mbeya au Dalsm kupunguza kuchoka nasoma dashboard inataka nini pamoja na bara bara maana kwa sisi madereva bara bara huwa inaongea yenyewe pamoja na kuangalia vibao kweli kukimbia kimbia hovyo mjini walikojaa watoto wa shule ni ushamba sana mtu mwingie anakupita kulia kwenye Zebra umepisha watu yeye anakupigia na honi kabisaa kana kwamba kuwapisha watu wapite kwenye kivuko ni kosa...
 
Back
Top Bottom