Ni vigezo vipi vilimpa Hussein Bashe Uwaziri wa Kilimo?

Ni vigezo vipi vilimpa Hussein Bashe Uwaziri wa Kilimo?

Mkulima auze popote anapotaka, hilo la kuuza mpaka akiba sio kosa la Bashe ni kosa la huyo mkulima mzembe, misimu inayokuja atajifunza
Mkulima yupi? Hakuna mkulima anaye jua hata Mpaka wa Namanga au Silali au Tarakea au Holili, wakulima ndio kwa sasa wanapelekewa mahindi ya misaada
 
Wivu,
Mtu alime auze anako taka, Ajiwekee Akiba kadiri ya Familia yake,

Mahindi yalipo zuiliwa mlilia, now mnalia tena,
ACHENI USHAMBA VIJANA
Auze wapi? Sema Dalali auze anako taka, hakuna Mkulima anaye weza kuuza Mahidi nje ya nchi, hayatokea bado, sema Dalali auze anako taka
 
Waukize wanajua bei.ya pembejeo au walitaka mkulima aendelee kuwa masikn..?
Still Bado wakulima ni masikini, unazani gunia 150, 000 kuna mkulima ana mahindi? Sikiliza Wakulima ndio wana njaaa kwa sasa wanapelekewa mahindi ya misaaada au uananiza hayo mahindi ya misaaada wanapelekea wafanya kazi?
 
Mimi pia nimemfuatilia Bashe kwa muda namuona kama ana tofauti kidogo, anaweza kutufaa. Kuna wakati alivyokuwa backbencher bungeni alikuwa anaongea sense sana.

Ana mpango mkubwa wa kilimo cha umwagiliaji ukifanikiwa tunaweza kupiga hatua kubwa.

Ila tatizo mfumo wetu na CCM mara nyingine ni vigumu sana kubadili mambo.
Maigizo, hio mipango ipo sana tangu enzi za Mwinyi
 
Mkulima yupi? Hakuna mkulima anaye jua hata Mpaka wa Namanga au Silali au Tarakea au Holili, wakulima ndio kwa sasa wanapelekewa mahindi ya misaada
Wakulima walikuwa wakiuza mahindi debe shilingi 3000 hadi 5000
Mipaka kufunguliwa imewafanya kuuza debe shilingi 14000 hadi 25000

Mfanyabiashara akiwa anauza kwa bei nzuri basi demand Kwa wakulima inakuwa kubwa na bei inapanda,

Kufunga mipaka ni kumuumiza mkulima kwa faida ya wasiolima
 
Maigizo, hio mipango ipo sana tangu enzi za Mwinyi
Mkuu nakubaliana nawe mipango ipo miaka mingi.

Nimesoma kitabu cha Mwinyi "Mzee Rukhsa : Safari ya Maisha Yangu".

Ukurasa wa 136 anaelezea alivyotembelea Korea ya Kaskazini tarehe 7 mpaka 23 April 1985, akiwa Makamu wa Rais. Akasaini mikataba ya kilimo cha umwagiliaji na shamba la pamoja la hekta 100,000 katuka bonde la mto Rufiji. Wakipanga kila hekta hata ikizalisha tani 10 za mahindi na mpunga, kuwe na tani 2,000,000 za chakula kwa mwaka.

Lakini Mwinyi anasema shamba halikuwahi kulimwa lote wala kufikia tija hiyo.

Pia kulikuwa na mpango mwingine wa kulima pamba hekta 100,000 kanda ya ziwa. Habari ni ile ile, mpango haukufanikiwa.

Kwa hiyo una kila sababu ya kusema mipango hii ilikuwapo tangu enzi za Mwinyi, Mwinyi mwenyewe kaandika.

Ila huoni kwamba watu kama kina Bashe wanaleta matumaini mapya?

Mimi naona tatizo la kimfumo ni kubwa sana na inawezekana watu wachache tu hata wakiwa na ideas nzuri vipi wakashindwa.

Sasa wewe umefanya nini kujiongeza tuondoke hapa tupige hatua zinazotakiwa?

Sasa hapa kwenye matatizo ya kimfumo tunafanya vipi?

Maana ni rahisi kulaumu wengine, wewe umefanya nini?
20221122_190502.jpg
 
Wakulima walisha uza kwa bei ya chini kitambo sana, we unashikiwa akili inaonekana
Sasa suala la wakulima kuuza mazao mpaka wakasahau kuweka akiba huo ni upumbavu wao na wala Bashe hatakiwi kulaumiwa kwa hilo.

Yaani mpaka kuweka akiba ya chakula kwa ajili ya familia yako na yenyewe unasubiri serikali ikukumbushe?

Wa Tz tuna tabia za kuendekeza upumbavu ndani ya vichwa vyetu.

Ngoja njaa iwanyooshe kwanza ili mwaka ujao watakumbuka kuweka akiba ya chakula.
 
Aliyefungua nchi ndiye aliyeruhusu mazao kusafirishwa na Bashe alikuwa anatekeleza maagizo huku akijitafutia sifa kwa wakulima. Wakulaumiwa ni SSH.
 
Uwezo wenu ni mdogo sana , sikiliza kwanza hakuna Mkulima anaye jua hada mpakana pakoje, na pili wakulima walisha uza mahindi mara tu baada ya kuvuna tena kwa bei ya chini sana, na hao wakulima ndio kwa sasa wana lia njaaa
Kwani huyo mkulima kuna aliye mshikia bunduki kuuza mahindi yake mpaka akashindwa kuweka akiba?
Ngoja njaa iwanyooshe kwanza ili mwaka ujao watakumbuka kuweka akiba.

WaTz tuache kuendekeza upumbavu ndani ya vichwa vyetu.
 
Bashe ana mapungufu ya kibanadu kila mtu anaweza kuanayo,ila ni bora kuliko wengine
 
Bashe akili kubwa sana, i wish aje kuwa waziri mkuu au rais kabisa.!

Mbolea ya ruzuku ni nyingi san kipind hiki.

Kuhusu bei ya mahind ttaumia huu msimu lkn next time wengi wataingia shamba na watalima kibiashara hadi graduates tutaacha kujazana mjini na bahash za kaki tukimbikie shamba.
 
Mpaka sasa sijajua ni kigezo kipi kilimpa Uwaziri wa kilimo kwa sababu ni moja ya Mawaziri wa hovyo sana wanao shinda kutafuta sifa.

Bashe aliruhusu mahindi yaende sana nje, na kwa sasa cha ajabu Wakulima ndio wabao lia njaaa, na wenye mahindi ni Madalali.

Sehemu kama Arusha gunia ni sh 150, 000/ na hakuna mkulima mwenye mahindi ya kuuza, kwa sasa wanalia njaa lakini Bashe hadi leo akihojiwa utasikia nchi ina ziada ya chakula.

Na mbaya zaidi Raisi anawaini sana hawa wahuni itachukua.muda sana kuja kujua anafanya kazi na wahuni

View attachment 2424396
Hao wakulima unaowapangia bei uliwapa pembejeo?
 
Hivi kuna Mkulima wa Tanzania anapajua ata mpakani Namanga panafanaje kweli?
Wakulima wa hii nchi bado hawana sauti na wanachozalisha,Madalali ndiyo wanapanga Bei kwa Mkulima alafu wao ndiyo wanatajirika kwa kuwauzia wafanyabiashara wakubwa.Nimeshiriki study nyingi za Kilimo vijijini Morogoro,Iringa,Njombe,Manyara,Mbeya,Ruvuma,Iringa na Njombe.
Wakulima bado wananyonywa,uyo Bashe Mwambieni aende vijijini akaongee na wakulima "aandae Focus Group Discussion"ataambiwa mambo ajawahi kuyasikia.
 
Nipende kujibu swali lako kama ifuatavyo.
Bash aliwauzia chama pendwa media house yake (gazeti la Mtanzania) kwa kuwapa umiliki wa gazeti na yeye kupewa unaibu waziri.
Baada ya kuonesha uwezo ndio akapanda cheo kuwa waziri.
Maamuzi ya kuto zuia mahindi kuuzwa nje ya nchi, sio maamuzi binafsi ya Bashe.
Ni maamuzi yalioyochukuliwa kutokana na matokeo ya kitafiti.
Iwapo bei za nafaka zingekuwa chini, wakulima wangepata hasara na wasingekuwa na mtaji wa kuwekeza kwenye msimu unaofuata wa kilimo.
 
Unadhani hata anaelewa anachoongea sasa. Yeye anataka hela zake ajipangie ila wakulima wapangiwe wapate bei gani ilhali ni wao wamevuja jasho.

We mtoa mada ingia shambani alafu usiuze mahindi yako nje simple tu
Mnajichanganya sana kushindwa kitofautisha mkulima na mfanyabiashara,mkulima aliuza mazao yake zamani sana msimu wa mavuno, waliopo sasa ni wafanyabiashara ambao nyinyi ndo mnawaita wakulima kisa tu wana stock ya mahindi kwenye maghala yao[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom