Elections 2015 Ni vigumu sana kupata Rais mwenye sifa bora 2015

Elections 2015 Ni vigumu sana kupata Rais mwenye sifa bora 2015

Kigarama

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2007
Posts
2,492
Reaction score
1,230
Mwaka 1995 Mwl.J.K. Nyerere alitoa sifa za mtu anayetaka kuwa Rais wa Tanzania kwa mwaka ule, uchaguzi ulioshirikisha vyama vingi toka vyama vingine vilipopigwa marufuku na TANU mwaka 1965. Miaka 20 baadaye (2015) tangu mwalimu alipotoa sifa zile pale Kilimanjaro Hotel, tutafanya tena uchaguzi wa kuchagua Rais wetu. Jee sifa zilezile alizopendekeza mwalimu ndiyo tuzitumie kuchagua Rais wetu wa mwaka 2015?

Tunataka Rais ajaye asimamie nini katika mfumo upi?
Awe ana madaraka ya kiutendaji au awe ni Rais wa Heshima (ceremonial President)?
Akiwa ni mgombea Binafsi atafaa kutuongoza au ni lazima atokane na vyama vya siasa?
Kwa changamoto zilizopo duniani na hapa nchini tunahitaji Rais wa aina gani?

Tofauti kati ya Kichaa na mtu mwenye akili timamu, siyo miili yao bali ni akili zao.
 
Sifa alizozitoa Mwalimu 1995 bado ziko valid leo hii. Tunataka rais ambaye akisema anachukia rushwa anaonekana kabisa kuwa anaichukia rushwa.

Tunataka rais atakayetuambia kuwa mikataba yote ya madini nchini imepitishwa kwa njia za rushwa rushwa na kwa hiyo ni null and void.

Tunataka rais ambaye ataweka maslahi ya Watanzania kwanza na sio wawekezaji. Rais atakayetambua kuwa tunahitaji uwekezaji lakini wawekezaji si wakombozi katika uchumi wetu.

Tunataka rais atakayeiweka Tanzania kwanza, na wala si kutafuta sifa za Wamarekani.

Naweza kuendelea lakini ngoja niwaachie na wengine nao wakune vichwa.
 
Heri ya Mwaka mpya wa 2012!!

Ukiwa ni mwanzo wa mwaka 2012 napenda kushirikiana na wana jamvi juu ya jambo mojawapo nililokuwa nalifikiria sana katika mwaka uliopita; nalo ni Rais wa Tanzania (ama Tanganyika) wa awamu ya tano(5) awe na sifa gani?
Naamini kama nchi mafanikio hayaji kwa kubahatisha au kwamba wengine walaaniwe na sisi tubakie tuliobarikiwa; bali huja kwa kukusudia.
Some people succeed because they are destined to, but most people succeed because they are determined to. ˜-Author unknown.
Kutokana na pale tulipo kama nchi, mtu mwenye akili akija kututathmini atatuonea huruma sana. Na mwingine anaweza kusema Peter Botha alisema ukweli juu watu weusi japo kauli yake ilikuwa ya kibaguzi zaidi.
By now every one of us has seen it practically that the Blacks cannot rule themselves. Give them guns and they will kill each other. They are good in nothing else but making noise, dancing, marrying many wives and indulging in sex. Let us all accept that the Black man is the symbol of poverty, mental inferiority, laziness and emotional incompetence
And here is a creature that lacks foresight. There is a need for us to combat him in long term projections that he cannot suspect. The average Black does not plan his life beyond a year. Peter Botha

Lakini ukweli unabakia kuwa sisi tunaweza, tatizo wenye kutuongoza si viongozi na wenye kututawala si watawala. Hawakujijali kauli hii
As long as I am a leader, our position is not going from that of our forefathers. I do not want the responsibility for selling the rights of our children yet unborn. – unknown author.
Kufikiri kwangu kulinipeleka kuona sifa hizi zifuatazo:

Asiwe na uhusiano na mtandao wowote wa kifisadi

Ili aweze kuiongoza Tanzania huru bila ya shinikizo la watu wengine wanaomongoza kwa remote hasa mafisadi, ni LAZIMA asiwe na ushirika wowote na mtandao huo. Vinginevyo hatufai, atakuwa janga.

Asitoke CCM
Najua wako wengi watanishambulia katika point hii, lakini ndiyo ukweli. Rais ajaye hafai kutoka CCM, akiwa mwana CCM ni kujiongezea janga jingine. CCM yenye kuwajali wakulima na wafanyakazi imekwisha potea. Haiwezekani kumpata kiongozi miongoni mwa hawa waliopo katika CCM atakaye kuwa na uchungu na wakulima na wafanyakazi na kufikiri ustawi wao wakati huohuo akawasahau CCM wenzake ambao walio "wabinafsi/walafi". Ikiwa unafikiri yupo mwenye uchungu katika hili ama kwa kauli na vitendo mtaje. Wengi watasema tu, kwenye vitendo mgogoro. Ndiyo

Awe na isfa na ujasiri wa kuuvunja mtandao wa kifisadi
Ili Tanzania itoke katika hali ngumu ya maisha iliyonayo sasa na kufufuka kiuchumi ni LAZIMA Rais ajaye awe na ubavu wa kuubomoa mtandao wa mafisadi. Hawa wanaotajwatajwa CCM kwamba wanawania urais 2015 hawawezi kusema kwamba wana ubavu wa kuuvunja mtandao huo ikiwa wa nao wamenufaika na mtandao wenyewe. Ni lazima kwa Rais ,si kuubomoa tu mtandao huo bali pia, kuwashitaki wahusika wote katika mashitaka yayatayoipatia ushindi Serikali (Umma wa watanzania) dhidi ya mafisadi hao.

Mwenye maono ya kuijenga Ikulu na kutunza heshima yake
Heshima ya Ikulu imeporomoka mno mno. Sasa kinaonekana kama kijiwe cha "wahuni" Fulani wakati ni taasisi yenye heshima ya juu Tanzania. Kuna minong'ono kuwa mfumo wa utendaji kazi wa Ikulu(kwa maana ya watendaji wake) umeparaganyika. Walioingia baadaye wakafikiri wanajua kuliko waliokuwepo awali nao wamechangia kuivuruga nidhamu na uwajibika wa Taasisi hii. Kwasasa huwezi kumwambia mtu mwenye "akili" ,Ikulu ni mahalali patakatifu akakubaliana nawe, kama si kukudharau.

Anayeweza kuvitumia vichwa vya wataalamu mbalimbali kuijenga Tanzania
Rais hajui kila kitu kuhusu Tanzania; hajui kila kitu kuhusu fani zote kuanzia kwenye kilimo hadi kwenye viwaanda; michezo hadi utamaduni; elimu hadi uchumi. Anahitaji kuwa ni mtu msikivu na anayeshaurika, na anayeweza kutumia vichwa mbalimbali vya wataalamu katika kuijenga Tanzania.

Anayeweza kusoma na kuzithamini tafiti mbalimbali na kuziiingiza katika sera kama si kuboresha utendaji wa serikali
Rais anayekuja ni LAZIMA awe anasoma, kama si yeye mwenyewe moja kwa moja basi kupitia wasaidizi wake tafiti mbalimbali za wanataaluma wa ndani. Kisha kuzitumia kwa ustawi wa jamii ya watanzania kwa kuziingiza katika sera. Pia zaweza kutumika kuboresha utendaji wa serikali ama taasisi za serikali.

Ni bahati mbaya kubwa sana ya kwamba ziko tafiti nyingi zimefanywa lakini matokeo yake ni kuwekwa katika maktaba za vyuo au taasisi husika. Nchi za wenzetu wanatumia kazi za utafiti kustawisha jamii zao, lakini kwetu…ni jambo lahuzini.

Anayethamini utu wa mtu
Hatuhitaji Rais anayethamini mali ya mtu au kile alichonacho mtu bali, kwanza athamini utu wa mtu kisha mchango wa mtu katika kuijenga jamii huru yenye matumaini ya ustawi wake bila ya kudhalilishwa.
 
nimependa hiyo comment..''...awe anasoma...'' Asisubiri aletewe taarifa.. Tena aingie mtandao wetu huu tukuka.... Jamii Forums!!!!!! Humu akiwa anaingia,hatatoka mtupu!
 
mwamuongelea dr.slaa au? Nitarudi.

Sija muongelea Dr Slaa. Nimeeleza sifa zile ambazo naona kuwa kama mtu atakayegombea nafasi ya urais wa JMT kwa awamu ya tano atakuwa nazo basi wanachi tutakuwa tumelamba dume.

Kwa mfano huwezi kuwa na Rais anayejali/ama yuko tayari kuilinda Katiba kama ni mvivu wa kuisoma hiyo Katiba. Vinginevyo, ataambiwa jambo na wapambe wake kuwa hili lipo katika Katiba, na yeye kujibu sawa, halafu anaingia kutekeleza kitu ambacho hakipo.

Najua ndani ya CCM wapo watu wachache sana ikibidi niseme wachache mno, ambao wanfaa kuwa viongozi wazuri wa nchi hii lakini si kutoka ndani ya CCM bali wakitokea nje ya CCM.
 
nimependa hiyo comment..''...awe anasoma...'' Asisubiri aletewe taarifa.. Tena aingie mtandao wetu huu tukuka.... Jamii Forums!!!!!! Humu akiwa anaingia,hatatoka mtupu!
Mkuu, si humu tu (japo humu haziwekwi kazi za utafiti ki-vile, sana sana utaona ripoti ya utafiti fulani) bali kuna sehemu nyingi ambazo utakuta research works. Yeye mwenyewe awe anasoma, lakini pia wasaidizi wake kwa kuwa wako wengi nao wasome, halafu baadaye wanam-brief kile walichosoma. Siyo kushinda na taarifa za magazeti ya udaku au kumpa umbea ambao hauna proof.
 
Kama sifa zenyewe ndiyo hizo, mbona viongozi wote wa cdm wanazo isipokuwa Zitto na Shibuda (kibuda).
 
Mkuu, ni lazima awe mtu anataka kuacha legacy ya kuwa Tanzania ameijenga kama nchi katika nyanja mbalimbali ikiwemo kiuchumi, kisiasa, kijamii na kimaadili.
 
Mkuu, ni lazima awe mtu anataka kuacha legacy ya kuwa Tanzania ameijenga kama nchi katika nyanja mbalimbali ikiwemo kiuchumi, kisiasa, kijamii na kimaadili.

Mkuu, nakubaliana na wewe. Lakini kama akiwa ni mtu fisadi, au anauhsiano na mafisadi au mwoga wa kuuvunja mfumo/mtandao wa kifisadi na mengine niliyotaja hapo juu, he/she will never accomplish what Tanzanians are in needy for the moment.
 
Kama sifa zenyewe ndiyo hizo, mbona viongozi wote wa cdm wanazo isipokuwa Zitto na Shibuda (kibuda).

Wapo na wengine wasio wanachama wa CHADEMA nao wanasifa hizo. Tatizo mgombea huru kabanwa.
 
Hizo sifa ni muhimu sana..maana huyo rais atakuwa na kaz kubwa..yakuirudisha tanzania kwenye nafasi ya kuwa nchi yenye kuthamin mali zetu.....nakusihi mungu utusikie maombi yetu.
 
dr JOHN POMBE MAGUFULI ndo mwenye sifa zote hizo kasoro moja tu kuwa anatoka ccm
 
Mr. Kamakawa or sorry kawakama Dr. John Ulabu Magufuli akiwa Rais watu wote wa Dar watajua kupiga mbizi bahari mpaka Zanzibar maana mhm hana mchezo huyu.
 
1. awe mkristo safi - kwa sababu ni zamu ya mkristo
2. anayejua shida na matatizo ya watanzania
3. aje na plan ya kutatuat matatizo na shida za watanzania
4. awe muadilifu na anayejiheshim sio wa kutoa matusi kwa watanzania kama asiye na nauli apige mbizi, ukitaka kula lazima uliwe, wahitimu wa vyuo msio na kazi kafugeni kuku etc
5. awe na elimu walau ya degree moja hasa ktk science subject maan marais wote waliopita ni ualimu na fani nyinginezo.
6. muhim kuliko yote awe anaweza kuhimili pressure za expectations za ndugu jamaa na marafiki.
 
Back
Top Bottom