Elections 2015 Ni vigumu sana kupata Rais mwenye sifa bora 2015

Elections 2015 Ni vigumu sana kupata Rais mwenye sifa bora 2015

Hizo sifa ni muhimu sana..maana huyo rais atakuwa na kaz kubwa..yakuirudisha tanzania kwenye nafasi ya kuwa nchi yenye kuthamin mali zetu....nakusihi Mungu utusikie maombi yetu.

Amina!!
 
[h=1]What Makes a Great President?[/h]We have probably heard the old saying that "anybody can grow up to be President." But, not everybody is cut out to be President. It takes a special kind of person, someone tough, smart, and driven, just to run for the job. It takes still more talent and character to hold up under the pressures of life in the White House.

Great Expectations
Americans expect a lot from their Presidents. Understandably, they want the President to take quick action on problems facing the nation, such as crime and drug abuse. However, the U.S. Constitution limits the President's power to act. Only Congress can pass legislation, and Congress sometimes moves slowly. The President can only approve or veto (reject) legislation that Congress passes. Even then, Congress can override a veto and make it the law. The Supreme Court can also limit the President's power by ruling that a law or action violates the U.S. Constitution. "The President has less power than the average voter thinks he does," says presidential expert Paul Boller. "He can't simply by himself make major domestic policies."

1. The "Bully Pulpit"
2. Facing Crises
3. Who Is Best Qualified?
4. Passing the Test
 
Naomba kutoa mtazamo wangu juu ya mwenendo mzima wa mbio za uraisi 2015. Naamini kuwa kutokana na hali mbaya ya kisiasa nchini kwa sasa ni vigumu sana kumpata Raisi mwenyesifa stahiki 2015 kwasababu zifuatazo.


  1. Kila kundi la watu au wanasiasa watatumia kila aina ya mbinu chafu au nzuri kuhakikisha kuwa mtu wao anapita haijalishi ni mtu mwenye sifa au hana sifa kwa maslahi binafsi.
  2. Kunauwezekano mkubwa kila dini kutoa mwongozo juu ya mtu wanae mtaka awe Raisi 2015 haitajalisha kama mtu huyo anasifa au hana sifa kunauwezekano wa watanzania kuchagua mtu kwasababu ya dini. Hii ni kutokana na joto la udini kupanda kwa kasi sana nchini.
 
Ndugu wa JF,

Wote tunafahamu baadhi ya majina ya wanasiasa ambao wamekua wakitajwa kuwania nafasi ya Urais mwaka 2015. Bila kujali Rais atatoka chama gani, ni vyema watanzania tuelewe tunahitaji mtu mwenye sifa gani hata kabla ya uchaguzi. Kwa mtazamo wangu, Rais ajae awe angalau na sifa hizi:

1. Mwenye ujasiri wa kuilinda Katiba na Sheria za nchi bila woga.

2. Mwenye uwezo na ujasiri wa kuifuta au kuichambua kwa upya mikataba yote isiyo na maslahi kwa Taifa.

3. Ambae hatageuza Ikulu kuwa pango la wanyang'anyi: Yani awe ni mtu anayeichukia rushwa na ambae hataingia Ikulu kwa kutumia rushwa.

4. Ambae hatakuwa na hofu wala aibu ya kumchukulia hatua za kisheria yeyote atakaevunja sheria za nchi bila kujali cheo chake, urafiki, au maslahi binafsi.

5. Mwenye mipango madhubuti na inayotekelezeka ya kuweza kututoa Watanzania katika hatua tulionayo na kufikia hatua nyingine.

6. Ambae atadumisha umoja, undugu, na mshikamano wa Taifa na kukemea kwa nguvu zote chokochoko za udini, ukabila, ukanda, au ushabiki wa kisiasa unaotishia umoja wetu.

Haya ni baadhi tu ya mambo tunayoyataka kwa Rais ajaye. Kwa wale wanaotajwa tajwa sijui nani ana vigezo hivi? Mwisho wa siku ni kura yako ndio itakayoamua nani awe Rais.

Asanteni.
 
Huyu ni dr slaa toka cdm,kuwaendekeza ukoo wa panya tutaendelea kumaliza nchi.
 
Ndugu wa JF,

Wote tunafahamu baadhi ya majina ya wanasiasa ambao wamekua wakitajwa kuwania nafasi ya Urais mwaka 2015. Bila kujali Rais atatoka chama gani, ni vyema watanzania tuelewe tunahitaji mtu mwenye sifa gani hata kabla ya uchaguzi. Kwa mtazamo wangu, Rais ajae awe angalau na sifa hizi:

1. Mwenye ujasiri wa kuilinda Katiba na Sheria za nchi bila woga.

2. Mwenye uwezo na ujasiri wa kuifuta au kuichambua kwa upya mikataba yote isiyo na maslahi kwa Taifa.

3. Ambae hatageuza Ikulu kuwa pango la wanyang'anyi: Yani awe ni mtu anayeichukia rushwa na ambae hataingia Ikulu kwa kutumia rushwa.

4. Ambae hatakuwa na hofu wala aibu ya kumchukulia hatua za kisheria yeyote atakaevunja sheria za nchi bila kujali cheo chake, urafiki, au maslahi binafsi.

5. Mwenye mipango madhubuti na inayotekelezeka ya kuweza kututoa Watanzania katika hatua tulionayo na kufikia hatua nyingine.

6. Ambae atadumisha umoja, undugu, na mshikamano wa Taifa na kukemea kwa nguvu zote chokochoko za udini, ukabila, ukanda, au ushabiki wa kisiasa unaotishia umoja wetu.

Haya ni baadhi tu ya mambo tunayoyataka kwa Rais ajaye. Kwa wale wanaotajwa tajwa sijui nani ana vigezo hivi? Mwisho wa siku ni kura yako ndio itakayoamua nani awe Rais.

Asanteni.

Mwenye sifa hizi ni Stephen Masato Wassira pekee yake.
Ndie mwanafunzi wa Nyerere mtiifu aliyebaki.
Hapendi Rushwa.
Ana msimamo usiyoyumba.
Uwezo wa kukemea na akamaanisha.
Hana hulka ya kujilimbikizia Mali.
Mtetezi wa wakulima na wanyonge tangu zamani.
 
Mmepewa vigezo badala ya kujadili,kurekebisha kuongeza au kupunguza mnaanza kutaja watu!!!!

Wakianza kuchambuliwa hapa kwa vigezo hivi mtaanza kurushiana kejeli na kebehi!!!!!!!

Punguzeni utumwa wa mawazo tujue mustakabali,ukishakuwa na measuring gauge ambayo ni objective mchujo ni kitu rahisi tu!!!!!!!

Mi nadhani hata hao mnaowatumikia kuna kipindi wanawashangaaa!!!
 
Wanajamvi, Rais J. Kikwete Amekaribia Kumariza Muda Wake. Anaondoka Madarakani Kukiwa Na Changamoto Zifuatazo, Mosi, Sintofahamu Mahusiano Mabaya Ya Rwanda Na Tanzania, Pili, Mgogoro Wa Ziwa Nyasa Kati Ya Malawi Na Tanzania, Tatu, Kuongezeka Kwa Vitendo Vya Kigaidi,mf.Kulipuliwa Kwa Kanisa La Olast Arusha,mauaji Ya Padri Mushi, Uchomaji Wa Bar. N.K, Tano, Mchakato Wa Katiba Mpya Sita, Elimu Ambako Walimu Mishahara Ni Midogo, Shule Za Kata Hazina Waalimu Wa Kutosha, N.K. Sasa Kutokana Na Changamoto Hizo, Unadhani Ni Nani Ambae Au Unafikiri Ndiye Mtu Pekee Wa Kumkabidhi Usukani Wa Kuendesha Gari Letu? Anasifa Zipi Ambazo Unatushawishi Tumpe Dhamana Hii Kubwa? Pia Amefanya Yepi Mazuri Hadi Tumwamini? Hebu Leteni Hoja Na Vioja.
 
Mgombea atakayepitishwa na chama cha mapinduzi atakuwa na sifa zote za kuwa rais wa JMT.
Wanajamvi, Rais J.
Kikwete Amekaribia Kumariza Muda Wake. Anaondoka Madarakani Kukiwa Na
Changamoto Zifuatazo, Mosi, Sintofahamu Mahusiano Mabaya Ya Rwanda Na
Tanzania, Pili, Mgogoro Wa Ziwa Nyasa Kati Ya Malawi Na Tanzania, Tatu,
Kuongezeka Kwa Vitendo Vya Kigaidi,mf.Kulipuliwa Kwa Kanisa La Olast
Arusha,mauaji Ya Padri Mushi, Uchomaji Wa Bar. N.K, Tano, Mchakato Wa
Katiba Mpya Sita, Elimu Ambako Walimu Mishahara Ni Midogo, Shule Za Kata
Hazina Waalimu Wa Kutosha, N.K. Sasa Kutokana Na Changamoto Hizo,
Unadhani Ni Nani Ambae Au Unafikiri Ndiye Mtu Pekee Wa Kumkabidhi
Usukani Wa Kuendesha Gari Letu? Anasifa Zipi Ambazo Unatushawishi Tumpe
Dhamana Hii Kubwa? Pia Amefanya Yepi Mazuri Hadi Tumwamini? Hebu Leteni
Hoja Na Vioja.
 
tatizo siyo rais tatizo ni CCM aka intarahamwe....
 
Back
Top Bottom