Elections 2015 Ni vigumu sana kupata Rais mwenye sifa bora 2015

Elections 2015 Ni vigumu sana kupata Rais mwenye sifa bora 2015

Watanzania tumejisahau kwamba kwenye uraisi tunahitaji nini hasa. Kwa mawazo yangu tunahitaji maendeleo nchi yetu ni masikini bado kiuchumi na tunahitaji kiongozi anayeelewa mambo na kutuletea maendeleo. Sasa watu wakianza kuongelea viongozi ambao wanaweza kuwa uraisi wanasema vitu ambavyo ni vya kishabiki zaidi mfano mtu mwenye kula rushwa na kila mtu anajua kuna wanaosema hao wanapedwa kama vile uraisi ni mapenzi pekee au viongozi wengine hawapendwi kibinafsi lakini si kiamaendeleo au kiuwezo. Mimi ninaona tutafute kiongozi atakayetufaa tuachane na mafisadi na mambo ya mapenzi je tukipenda watu ambao wanatuibia au wanakashfa za rushwa watatusaidia nini kwenye nchi yetu? msijamka lalamika kwanini hatuna maendeleo wakati mnachagua wala rushwa mnaowapenda
 
Umasikini wetu ni ujinga tulionao wa kushangilia wala rushwa na kuwaona mashujaa na kuwapa madaraka.
 
Rais bora ni yule mwenye upendo kwa Taifa lake aliyetayari kujikana mwenyewe kwa manufaa ya watu wake waliomasikini.Mwenye kufuata haki na katiba.Mwenye kulinda.raslimali za Taifa kwa manufaa ya Taifa. Hapa utaona kiwango cha elimu yake na chama anakotoka si mhimu kabisa; ndo maana tunahitaji ushiriki wa Mungu pia.
 
kila nikiwaza sijaona mwanasiasa yeyote ambaye anafaa kuwa rais wa nchi kutoka chama chochote cha siasa hapa nchini.
ukimtoa salim .a.salim ambaye hatagombea.ila tuombe mungu kitakachotokea
 
Hili jambo hata mm linaniumiza kichwa sana;kuna wakati nahisi hivi vyama vyote,ccm,cdm,cuf,nccr,n.k waungane pamoja ili wakiamua jambo la kitaifa liwe moja;lkn leo serikali ya ccm ikisema au ikifanya jambo ambalo hata km lina maslahi na taifa vilevile upinzani hakuna atakaemuunga mkono mwenzake hata kama yupo sahihi;mfumo wa demokrasia usipobadilishwa nchi za kiafrika zitachukua muda sana kuendelea
 
Hili jambo hata mm linaniumiza kichwa sana;kuna wakati nahisi hivi vyama vyote,ccm,cdm,cuf,nccr,n.k waungane pamoja ili wakiamua jambo la kitaifa liwe moja;lkn leo serikali ya ccm ikisema au ikifanya jambo ambalo hata km lina maslahi na taifa vilevile upinzani hakuna atakaemuunga mkono mwenzake hata kama yupo sahihi;mfumo wa demokrasia usipobadilishwa nchi za kiafrika zitachukua muda sana kuendelea

kila nikiwaza sijaona mwanasiasa yeyote ambaye anafaa kuwa rais wa nchi kutoka chama chochote cha siasa hapa nchini.
ukimtoa salim .a.salim ambaye hatagombea.ila tuombe mungu kitakachotokea

Mapungua.n.i yamekutana huku,mnataka nchi iendelee kuongozwa na kikwete au arudi mkapa? Au tukae miaka 5 ijayo bila raisi? Mwigulu,makamba jr nao hawafai?
 
Mapungua.n.i yamekutana huku,mnataka nchi iendelee kuongozwa na kikwete au arudi mkapa? Au tukae miaka 5 ijayo bila raisi? Mwigulu,makamba jr nao hawafai?

tehe..umesema mwi...nani!!?? u are not serious right?
 
Kwa upinzani mwenye mvuto kwa sasa ni tundu lissu...chama tawala Edo boy hana mpinzani
 
Mapungua.n.i yamekutana huku,mnataka nchi iendelee kuongozwa na kikwete au arudi mkapa? Au tukae miaka 5 ijayo bila raisi? Mwigulu,makamba jr nao hawafai?

mkuu matusi yote ya nini uwe na uelewa mpana ukiwa na ufinyu wa fikra utakuja sema hata panya road wanaweza kutawala
 
Mapungua.n.i yamekutana huku,mnataka nchi iendelee kuongozwa na kikwete au arudi mkapa? Au tukae miaka 5 ijayo bila raisi? Mwigulu,makamba jr nao hawafai?

Unatakiwa uwe na adabu katika maelezo yako co kuongea kama gasho
 
Majina ya watu hawa;lowasa,mwigulu,membe,j makamba,sitta na wasira yamekuwa yakipigiwa debe kwa namna tofauti tofauti kuwa wanafaa kupewa dhama ya kutangulia mbele yetu watuongoze.tumesikia wapiga debe wao na hata wenyewe wakisema😱h! huyu ni tumaini jipya kwa watanzania,wengine oh!huyu ni chaguo la mungu,mara wengine wanasema watajenga tanzania mpya na maneno mengi mengi ya kujinadi mbele ya watanzania.lakini jambo ambalo nataka watanzania mnisaidie ni kwamba;watu wote hawa tulishawapa dhamana ya kututumikia.wengine muda mrefu na wengine muda mfupi.sasa nisaidieni;mh lowasa kwa muda tuliompa atutumikie alifanya nini kwa watanzania la kumkumbuka hadi leo.hii ni halikadharika kwa akina mwigulu,makamba,sitta,membe na wasira wamefanya jambo gani la kugusika kwa watanzania kwa muda wote waliotumikia taifa; wengine tangu wakiwa wa tumishi wa umma na wangine wakiwa viongozi wa nchi hii kwa muda mrefu.nisaidieni watanzania ni kwa sababu gani niwaamini hawa kuwa wataitoa tanzania hapa ilipo?
 
Watanzania wengi walijua swala la kuchagua raisi wa nchi ni jambo dogo na pengine halina umuhimu sana kwa maisha yao.

Wengi waliamini sifa za raisi ni kama vile haiba ya mtu,sura na rangi ya mtu,kabila la mtu na hata dini ya mtu.Wengine wengi walikariri majina ya vyama pasipo kuangalia uwezo wa mtu.

Ni imani yangu;wengi wao leo hii wanajuta;wengine kimoyoyo na wengine hata hadharani.

Cha msingi kwa sasa ni tujifunze kutokana na makosa kwa kuchagua raisi bora na si vinginevyo.
 
Mara nyingi nimewasikia rafiki zangu na watu waliokaribu nami wakisema "sisi hatuwezi" au "haya wanayaweza ngozi nyeupe" au "Wakenya wapo mbali" au "Kagame hatari yule". Nimekuwa nikijiuliza ni kwanini Watanzania wengi wanaamini kuwa hawawezi ila wenzao wa nchi zingine wanaweza? Nimejaribu kuchekecha majibu mbalimbali na kufikia majibu mawili: moja, Watanzania wengi hatujiamini kifikra na pili, Watanzania wengi hatuna matumaini ya maisha mazuri siku zijazo.

Naomba kuelezea ni kwanini Watanzania wengi hatujiamini kifkra. Sababu mbili zimetufanya tusijiamini kifikra; ya kwanza ni elimu duni tunayoipata nchini mwetu inayotufanya tusiwe na uwezo mkubwa wa ushindani na ya pili ni soko huria lililoruhusu ushindani kutoka nje. Elimu ya Tanzania inamwandaa mwanafunzi ili aje aajiriwe baada ya masomo. Tatizo ni kwamba baada ya soko huria na utandawazi kuenea duniani makampuni makubwa duniani yamewekeza nchini mwetu na kujipangia yamwaajiri nani na alipwe mshahara wa kiasi gani japo sheria za Tanzania zipo na watendaji wapo japo sijui maofisini watendaji hufanya nini? Watanzania wengi wamejikuta wakibaki kwenye nafasi za chini kwenye makampuni haya na wakilipwa mishahara midogo bila marupurupu na WAGENI wengi kuwa ndio wanashikilia nafasi za juu kwenye makampuni haya na kulipwa mishahara minono na marupurupu makubwa. Jambo hili limewafanya Watanzania wengi wajidharau na kuwafanya wajihisi watumwa ndani ya nchi yao. Haya ndiyo yanawafanya Watanzania wengi kujihisi hawawezi kwa sababu wenzao WAGENI wanaweza na kuishi maisha bora na yenye heshima. Hisia hizi zimedumaza fikra za Watanzania wengi na tunahitaji rais ambaye anaweza kunena na kutenda ili kujenga hali ya kujiamini kwa Watanzania.

Watanzania wengi hawana matumaini kwa sababu wanaishi maisha ya dhiki yanayotokana na kipato kidogo na kutokuwa na vyanzo vingi vya kipato. Hivyo basi wanajikuta hawapati mlo kamili au milo mitatu kwa siku au vyote. Kwa sababu ya kipato kidogo Watanzania wengi wanakosa mahitaji mengine muhimu kama makazi bora, maji safi na salama, nguo zenye heshima na elimu bora itolewayo na shule chache za kimataifa zilizopo nchini Tanzania. Hali hii ya umaskini imewafanya Watanzania wengi kupoteza matumaini na tunahitaji rais ambaye ana uwezo wa kuwapa Watanzania Matumaini. Rais akilalamika na kutoweza kuelezea kinagaubaga hatua ambazo serikali yake inazichukua ili kutatua matatizo ya kimfumo nchini, huwakatisha tamaa Watanzania wengi kuhusu ndoto ya maisha bora.
 
Na kiboko wa haya matatizo yote ni Lowassa,nchi imeshapinda tumpe lowassa ainyoshe
 
wakuu habari!
Unahisi Tanzania tunahitaji kiongozi wa aina gani kati ya hizi sifa.
MWENYE MAAMUZI MAGUMU?
AU

MWENYE MAAMUZI SAHIHI?
 
Watanzania wanahitaji MTU mwenye maamuzi magumu ya Kifisadi atayeweza kuiweka bond hata Ikulu ili aendelee kujinufaisha; na wanashangilia mwenye pesa, waache wachague ila " majuto ni mjukuu"
Mpaka waote sugu miili kwa ugumu wa maisha huku wenzao wanawatumia na kuwanyonya kama kupe, na wanatamani kunyonywa hadi damu- hayo ndo maamuzi magumu
 
wakuu habari!
Unahisi Tanzania tunahitaji kiongozi wa aina gani kati ya hizi sifa.
MWENYE MAAMUZI MAGUMU?
AU

MWENYE MAAMUZI SAHIHI?

Mkuu Mbavu Mbili,Tanzania ya sasa tunamhitaji kiongozi mwenye hizo sifa zote,kwanza kabisa awe na maamuzi sahihi na pili magumu hasa pale panapohitajika hayo maamuzi magumu kwa sababu si kila idara itahitaji maamuzi magumu bali kila idara itahitaji maamuzi sahihi ili taifa lipate kustawi vema na kusonga mbele.
Mungu ibariki Tanzania,Mungu ibariki Afrika.
 
Habari zenu wana jamvi:,

mh. Mizengo kayanza peter pinda kazidisha utitiri wa watanzania wanaohitaji aiongoze tanzania.
Suala hili limekuja baada ya mikoa ya kaskazini kusini na mashariki kukunwa zaidi na utendandaji wake uliotukuka na mzuri zaidi ya maelezo hasa pale alipotokomeza ugaidi nchini hususani kuripuliwa misikiti na makania, kuleta kilimo bora cha kisasa kwa kutumia matrekta, kuongeza pesa kwa kuwadhamini wanavyuo wa elimu ya juu vyuo vikuu, kuboresha elimu tanzania, afya, kuinua uchumi n.k.
Kubwa zaidi ni kwa ukimya wake kama rais wa marekani mstaafu mh. Bill clincton ambapo hana makundi wala kundi la kuingia nalo ikulu.
Anawajali watanzania wote bila kujali itikadi zao za dini, rangi, ukabila n.k
anatosha kuliongoza taifa la tanzania 2015 - 2020
 
Mhhh rabda hayo wakat anayafanya nilkuwa sipo, wacha waliokuwepo waje watoe mawazo yao
 
Back
Top Bottom