Ni vitu gani muhimu Mwalimu unavyotakiwa kuwa navyo wakati wa kuripoti kazini?

komekaone

Member
Joined
Sep 2, 2012
Posts
47
Reaction score
9
Wakuu naombwa kujuzwa, natakiwa kuwa na vitu gani muhimu ambavyo vitahitajiwa na Mkurugenzi wa Halmashauri husika au ofisi ya shule. Hii itanisaidia kuviandaa vitu hivyo mapema na kuepusha usumbufu wa kurudi tena nyumbani ili kufuatilia na hatimaye kujikuta napoteza nafasi ya ajira. Nawaomba wazoefu na wajuzi wa hili mnifahamishe.
 
Vyeti vya shule cha form 4,6 na cha chuo pamoja na cheti cha kuzaliwa ni cha muhimu sana+Passport size
 

  • Academic Certificates - Form 4, Form 6 kwanza - Vitahitajika ,
  • Vyeti vya vyuo vitafuata baada ya kuwa vimetoka vitatumika kama viambatanisho ujazapo fomu za TSD ili kupata TSD Number.
  • Passport size, andaa za kutosha maana maeneo mengine huduma za picha huwa ni shida.
  • Kimsingi huwa hakuna usumbufu wowote sababu taarifa zako huwa tayari Mkurugenzi anazo.
 
Vyeti vya shule cha form 4,6 na cha chuo pamoja na cheti cha kuzaliwa ni cha muhimu sana+Passport size

ahsante sana mkuu, hlo la passport kwa kweli sikulifikiria kabisa. Natakiwa angalao niwe nazo ngapi?
 

Mwl.RCT. Nakushukuru mwl. kwa mafafanuzi yako ya kina.
 
Wakuu inakuwaje kuhusu account za benki, na ni ip ambayo ni pendekezo la serikali kwa salary. maana wengine tangu tuingiziwe boom la mwisho, na akaunti zenyewe zimeshafungiwa. kama vipi tufanye mishe mishemishe mapema, tujuzeni wakuu.
 
Hapo ni NMB ndio pesa hutangulia na ndio nashauri ufungue huko.
 
saafi kabisa,,,,,,

asisahau pesa kdogo ya kujikimu angalau cku 5, tafiti mifuko ya pensheni ilyobora,peleleza kwanza mahal unakoenda kabla,epuka rushwa ya ngono kwa wadada, uwe na kopi angalau 5 kwa kila cheti.
 

Umeibu vema mkuu, thanx sana.
 
Naombeni kuuliza suala la account ya benki, wanahitaji punde tu ukiripoti?au baada ya muda fulani?
 
asisahau pesa kdogo ya kujikimu angalau cku 5, tafiti mifuko ya pensheni ilyobora,peleleza kwanza mahal unakoenda kabla,epuka rushwa ya ngono kwa wadada, uwe na kopi angalau 5 kwa kila cheti.

Elly, nakushukuru ndugu kwa kunijuza na ikiwa kunamengine tujuze mkuu.
 
Wakuu inakuwaje kuhusu account za benki, na ni ip ambayo ni pendekezo la serikali kwa salary. maana wengine tangu tuingiziwe boom la mwisho, na akaunti zenyewe zimeshafungiwa. kama vipi tufanye mishe mishemishe mapema, tujuzeni wakuu.
Nakushauri ukafungue CRDB maana huduma zao ni rahisi kupata na WANAPAMBANA NA FOLENI KWA SANA. Na wana huduma FAHARI HUDUMA ambayo inaunganishwa karibu na Posta zote Tz..
 
Nakushauri ukafungue CRDB maana huduma zao ni rahisi kupata na WANAPAMBANA NA FOLENI KWA SANA. Na wana huduma FAHARI HUDUMA ambayo inaunganishwa karibu na Posta zote Tz..

dah. hili nalo neno akili mkichwa. ahsante mkuu.
 
watumishi wa serikali wanatumia nmb kuwekewa salary hizo crdb labda kuamishia tu n kutunzia mishahara!nakushaur ufungue nmb.
 
Ukifika tawi lolote la crdb, jitambulishe tu mie Mwalimu...nataka kufungua akaunti. Mwenyewe utashangaa..fulu ukarimu. utakuja kunambia badae..
 
Umepata ajira wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…