Tate Mkuu
JF-Expert Member
- Jan 24, 2019
- 33,092
- 96,127
Kwa heshima na taadhima naomba huyu Mheshimiwa ajitokeze hadharani kuwaomba mashabiki msamaha kwa kuwaita mbumbumbu wakati alipokuwa kiongozi mkubwa tu wa Simba Sports Club.
Ni vizuri akalifanya jambo hili wakati bado akiwa hai. Hata kama alighadhabika kiasi gani, bado hakutakiwa kuwaita mashabiki wa timu mbumbumbu! Yaani hawana chochote wanacho kijua!
Binafsi nilikuwa najua hili jambo wanamsingizia tu! Ila siku nilipoona kipande cha gazeti humu jukwaani, ndipo nilipoamini kuanzia siku ile.
Kiukweli naomba mashabiki wote wa Simba mniunge mkono katika hili. Hii kauli siyo nzuri hata kidogo. Na kwa kweli wengi mnachukizwa na hili jina! Maana imesababisha mpaka Watani wenu Yanga wawaite MBUMBUMBU FC!!
Uungwana ni kitendo. Mheshimiwa Ismail Aden Rage, jitokeze kokote ulipo. Omba msamaha kwa kuwakosea mashabiki wenzako wa simba. Usisubiri mpaka siku uko hoi kitandani, ndipo uombe huo msamaha.
Naomba kuwasilisha.
Ni vizuri akalifanya jambo hili wakati bado akiwa hai. Hata kama alighadhabika kiasi gani, bado hakutakiwa kuwaita mashabiki wa timu mbumbumbu! Yaani hawana chochote wanacho kijua!
Binafsi nilikuwa najua hili jambo wanamsingizia tu! Ila siku nilipoona kipande cha gazeti humu jukwaani, ndipo nilipoamini kuanzia siku ile.
Kiukweli naomba mashabiki wote wa Simba mniunge mkono katika hili. Hii kauli siyo nzuri hata kidogo. Na kwa kweli wengi mnachukizwa na hili jina! Maana imesababisha mpaka Watani wenu Yanga wawaite MBUMBUMBU FC!!
Uungwana ni kitendo. Mheshimiwa Ismail Aden Rage, jitokeze kokote ulipo. Omba msamaha kwa kuwakosea mashabiki wenzako wa simba. Usisubiri mpaka siku uko hoi kitandani, ndipo uombe huo msamaha.
Naomba kuwasilisha.