Pre GE2025 Ni wakati sahihi Dkt. Slaa kutuambia nani alimpiga risasi Lissu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

kipara kipya

JF-Expert Member
Joined
May 2, 2016
Posts
18,833
Reaction score
23,276
Kipindi Mzee Slaa alipoulizwa ni nani alimpiga risasi Lissu, akasema ni Chadema wenyewe na Lissu anajua. Imepita takriban miaka nane Slaa anatuambia yupo tayari kurejea CHADEMA. Je, ni nani alimpiga risasi Lissu? Ni wakati mzuri wa Dkt. Slaa kutupa yale majibu yake.

Pia soma

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
 
Nilimdharau sana huyu mzee. Wakati wenzao wanapitia kikombe cha mateso, mauaji vifungo na kufilisiwa yeye alikuwa ubalozini akishiba na kutoa kejeli. Hata kama ni kusamehe, sio.
 
Akisema aliyempiga risasi Lisu ni Mbowe na Lisu akipotezea mtafanyaje ?!
Kumbuka kaanza kwa kusema "KILICHONITOA CHADEMA KWA SASA HAKIPO " Yawezekana huyo aliyemtoa chadema ndiye huyohuyo aliyempiga risasi Lisu!.
 
Akisema aliyempiga risasi Lisu ni Mbowe na Lisu akipotezea mtafanyaje ?!
Kumbuka kaanza kwa kusema "KILICHONITOA CHADEMA KWA SASA HAKIPO " Yawezekana huyo aliyemtoa chadema ndiye huyohuyo aliyempiga risasi Lisu!.
Aweke wazi atuondolee utata maana lissu ana tuhumu mwingine na yeye ana mjua mwingine!
 
Alisema hataki tena siasa wala vyama jana anasema yeye ni mwanasiasa ni mtu muongo asiye na kumbu kumbu!
Kumbukumbu anazo!.
Na kugeukageuka na kubadilikabadilika ndio uanasiasa wenyewe!.
Mwanasiasa ni yule asiyejulikana msimamo wake!
Mwanasiasa wa kweli ni yule ambaye leo akisema ziwa Tanganyika lipo magharibi mwa Tanzania , baada ya siku mbili tatu aseme Ziwa Tanganyika lipo mashariki mwa Tanzania na watu wakakubali.
 
Akisema aliyempiga risasi Lisu ni Mbowe na Lisu akipotezea mtafanyaje ?!
Kumbuka kaanza kwa kusema "KILICHONITOA CHADEMA KWA SASA HAKIPO " Yawezekana huyo aliyemtoa chadema ndiye huyohuyo aliyempiga risasi Lisu!.
Hakipo na Hayupo ni vitu viwili tofauti.
 
Alipogwa na wasio julikana.
 
Kipindi Mzee Slaa alipoulizwa ni nani alimpiga risasi Lissu, akasema ni Chadema wenyewe na Lissu anajua..
Ile ilikuwa uchawa tu.
Alisema vile kulinda ugali wake, pengine kwa maelekezo kutoka juu.
Uchawa na uongo ni kama mwili na damu.

Matukio yaliyoambatana na tukio la Lissu kupigwa risasi kwa vyovyote yalifanywa na mwenye mamlaka kubwa ya kiutawala, siyo Chadema..

Mfano:
Kuondoa walinzi wote (wanaolinda 24hrs) kwenye zile nyumba za serikali kupisha hilo tukio, kuondoa na kuficha kamera za CCTV, nk..
Kutumbuliwa kwa RC wa Dodoma kwa kutozuia Lissu kukimbizwa haraka Nairobi kwa matibabu,
Kukamatwa na kuwekwa ndani waliokuwa wanakusanyika kufanya maombi kwa ajili ya Lissu (alipokuwa iCU Nairobi), nk..
 
Kwa mwanasheria kama slaa akubali kutumika hapana aje aeleze ukweli umma uelewe ni nani ndani ya chadema au lissu aliwezaje kujipiga risasi!
 
Na kuondolewa kwa katibu mkuu wizara ya afya Dr Mpoki aliyemhudumia Lissu siku ya tukio general hospital Dodoma.
 
Duuh...!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…