Pre GE2025 Ni wakati sahihi Dkt. Slaa kutuambia nani alimpiga risasi Lissu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kwa mwanasheria kama slaa akubali kutumika hapana aje aeleze ukweli umma uelewe ni nani ndani ya chadema au lissu aliwezaje kujipiga risasi!
Mihimili ya kitaifa yenye mamlaka Kikatiba kama Bunge, Mahakama.. washakubali kutumika, itakuwa mwanasheria mmoja?

Hata Tume ya Uchaguzi (NEC), kiongozi wake ni Jaji, je haitumiki?!!!
 
Mihimili ya kitaifa yenye mamlaka Kikatiba kama Bunge, Mahakama.. washakubali kutumika, itakuwa mwanasheria mmoja?

Hata Tume ya Uchaguzi (NEC), kiongozi wake ni Jaji, je haitumiki?!!!
Nafikiri slaa ni mkweli sana na muadilifu muda wowote ataweka ufafanuzi hadharani!
 
Huu sio wakati wa kukumbusha yaliyopita. Mwanachama yeyote wa CHADEMA aliyepotea na anatamani kurudi chadema huu mwaka ni WA kuokota watu wote. Pamoja na yote jua Kuna watu wanamuamini Dr slaa hivyo alivyo kwaiyo usidhani Dr slaa atarudi pekeyake Kuna watu atarudi nao. Ccm huwa hawaangalii sana mwanachama wao anapotaka kurudi kundini pamoja na wingi wa watu iliyonayo.
 
Slaa alihapoteza credibility yake kitambo sana. Ni kama kuku aliyekatwa kichwa anahangaika tu. Si CCM au Chadema au Mtanzania yeyote anayemwamini.
 
Mkuu ungetuwekea na hiyo clip aliyosema CHADEMA walimpiga risasi Lissu.
...Mi niliiona aliyosema akiwa Katibu mkuu kuna tukio la kutekwa lilifanywa na CHADEMA bila ya yeye kujua. Na alikurupuka kuwazodoa Usalama wa Taifa kumbe ilikuwa kazi ya ndani.
CHADEMA ya Mbowe kuna mambo Katibu mkuu huwa hashirikishwi, ni kama tu kuwaandikia barua wabunge wa COVID19 -Mnyika alikuwa anapiga kelele - Mbowe anachekea chumbani.
 
Hayo aliyasema alipokuwa balozi huko ughaibuni wacha niitafute!
 
Yeye aliondoka chadema kwa kuwa mbowe aliokota kila silaha kupambana kukamata dola aliletwa lowassa slaa akasusa na kubwaga manyanga je hatoweza kimbia tena na kuondoka na watu wake!
 
Nilimdharau sana huyu mzee. Wakati wenzao wanapitia kikombe cha mateso, mauaji vifungo na kufilisiwa yeye alikuwa ubalozini akishiba na kutoa kejeli. Hata kama ni kusamehe, sio.
Wewe umeshia kwa Slaa mimi hadi Lissu kwa aina ya kampeni alizofanya nimemdharau sana!!
 
hayo ni mambo ya siasa tu na zilikuwa bifu kati ya slaa na DJ mbowe. kuteleza ulimi kwenye siasa ni kitu cha kawaida. lakini mbona lisu mwenyewe huwa anaamini zile nissan zilizopita morogoro chini ya bashite ndizo zitakuwa zilihusika? au hujawahi kumsikia akimlaumu bashite wazi wazi? siku lisu akishika nchi bashite atahamia msumbiji.
 
sawa atakwambia
 
Itapendeza Kama ataamua kujitenga na siasa maana misingi yake ya kuharakati na ukombozi wa fikra alishindwa kuisimamia
 
Wacha tusubiri ashike nchi ila slaa ana mengi ya kutueleza!
 
Wenzake walipokuwa wanateswa yeye anachekelea huo ndio ukweli na uadilifu gani. Ameishiwa hana pa kwenda anatapatapa, siasa ndiyo mkombozi pekee aliyonayo.
Wacha tumuone mwisho wake!
 
Alimkimbiaa Lowasa hasa zile tuhuma ilikuwa ngumu kwake kulamba matapishi yake. Anafaa apokelewe maana ile list of shame ilikuwa ngumu kwake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…