Ni wakati wa Netanyahu kujiuzulu, sio kupanga vita. Anasubiri nini?

Ni wakati wa Netanyahu kujiuzulu, sio kupanga vita. Anasubiri nini?

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Kitu kilchotokea Israel ni kibaya zaidi katika historia ya nchi hiyo.Na yote ni kutokana na siasa za ubabe wa Benjamin Netanyahu.

Siasa zake hizo imekuwa sababu ya kuwakasirisha zaidi wapalestina ambao sasa wameamua kujitoa muhanga kupambana badala ya kulia lia na kuomba kuhurumiwa.

Wananchi wa Israel kwa upande wao wana sababu ya kuendeleza maandamano yao kumuondoe kiongozi huyo na sio kumuunga mkono katika matangazo yake ya kulipiza kisasi kwa makosa ya kiongozi wao.
Kuendelea kwa mikakati ya vita ijapokuwa Israel ina nguvu kubwa ya kijeshi lakini huenda ikaleta msuguano wa kivita wa muda mrefu kuyavuta mataifa mengine ya Kiarabu na ulimwengu wa kiislamu kuamua kuingilia kati kuwatetea wapalestina.

Hilo la kubadilika kwa mawazo yaliyolala ya mataifa hayo mengi yao yakiwa ni jirani na Israel ni jambo linalochochewa na kauli za kuunga mkono kwa nguvu zinazotolewa na mataifa ambayo yana urafiki na Israel kama vile Marekani,Ufaransa,Canada,Uiengereza na Ukarine ambao bila kificho wamesema wanaiunga mkono Isreael na wataipa msaada ili kujilinda.

Umuhimu huo wa kujiuzulu unaongezeka kutokana na afya yake ya moyo ambapo mambo yakienda kombo zaidi yanaweza yakamzidishia matatizo hayo ya kuifya na kulazimika kuachia katikati ya vita jambo litakalowapa ushindi Hamas mara mbili zaidi.

Ni ushauri tu.
 
Miafrika inaumia zaidi miarabu na miyahudi ikiuana kuliko wamatumbi wenzenu wakiuana. Hiyo miarabu na miyahudi haiwapi hata pole kwenye madhira yenu ila nyie kila siku mnashoboka mtakuja kuolewa.

Kinachoendelea huko kinasikitisha at all levels ila acha wafu wazikane.
 
Miafrika inaumia zaidi miarabu na miyahudi ikiuana kuliko wamatumbi wenzenu wakiuana. Hiyo miarabu na miyahudi haiwapi hata pole kwenye madhira yenu ila nyie kila siku mnashoboka mtakuja kuolewa.

Kinachoendelea huko kinasikitisha at all levels ila acha wafu wazikane.
Huko ndiko tunakochukua mafuta yetu na ngano zinakopitia. Lazima tuwe macho na yale yanayotokea mpaka hapo mitambo yetu ya kusafishia mafuta kutoka Uganda itakapokuwa tayari imeanza kazi.
 
Miafrika inaumia zaidi miarabu na miyahudi ikiuana kuliko wamatumbi wenzenu wakiuana. Hiyo miarabu na miyahudi haiwapi hata pole kwenye madhira yenu ila nyie kila siku mnashoboka mtakuja kuolewa.

Kinachoendelea huko kinasikitisha at all levels ila acha wafu wazikane.
Cha ajabu waafrika hawaumii kwa mauaji yanayofanyika DRC na kwingineko Africa, wala hawaguswi na dhiki zinazowakumba waafrika wengi.

Tukubali tu kuwa hapa duniani sisi darasa letu ni lile la kutungiwa maswali ya TRUE or FALSE au MOJA JUMLISHA MOJA NI MBI-
 
Umitashumita urudishwe mashindano ya mwandiko yarejeshwe sikwa uchafu wa hati
 
Ataachia ngazi Gaza ikishakuwa jangwa.
 
Ajiuzulu ili iweje, mwacheni yuko vitani. Acha alipize machungu ya kichapo alichopata.
 
Mwenyezi Mungu atawanusuru wapalestina.
Muda si mrefu balozi wa Palestine UN ameomba wasaidiwe amani ipatikane, Hamas wamewaingiza chaka wenzao F 16 Falcon zina spit fire tuu.
 
viongozi wa nchi za magharibi ndio wanazidi kulikoroga kwa kusema hamas ni magaidi na kuiunga mkono Israel.Jambo hilo hawalifanyi pale wapalestina wanapotolewa majumbani mwao ili maeneo yavunjwe kujengewa wayahudi.Leo hamas wamejitetea wao ndio wanawalaani na kutaka dunia nzima iwe upande wao.
 
Waarabu hawana akili kabisa wametegwa na wenyewe wamejaa. Sasa wamewapa Israel sababu ya kuingia Gaza na kuichukua na kuua watu bila lawama.
 
Waarabu hawana akili kabisa wametegwa na wenyewe wamejaa. Sasa wamewapa Israel sababu ya kuingia Gaza na kuichukua na kuua watu bila lawama.

Unaijua vizuri Gaza?.kule kuingia ni kaI nyepesi ila kutoka salama hakuna uwakika uwo.ukipeleka wanajeshi kule basi utakuwa ume sign hati yao ya kifo.

Kule kila mtu ana silaha sasa jichanganye uwone balaa lake
 
Sio tu netanyau bali idara nyingi za usalama inabidi zichunguzwe maana kweli kambi zinafanyiwa ambush nyie msijue.hata dalili wameshindwa kuona.
 
It's obvious Netanyau hatomaliza miezi sita lazima atoke. Historia huwa inatabia ya kujirudia rudia.
 
Unaijua vizuri Gaza?.kule kuingia ni kaI nyepesi ila kutoka salama hakuna uwakika uwo.ukipeleka wanajeshi kule basi utakuwa ume sign hati yao ya kifo.

Kule kila mtu ana silaha sasa jichanganye uwone balaa lake
Mjomba ukiwa jeshi huogopi kufa.
 
It's obvious Netanyau hatomaliza miezi sita lazima atoke. Historia huwa inatabia ya kujirudia rudia.
Wanaomshabikia kule Marekani na Ulaya akina Sunak hawamtakii mema.Tusubiri tutaona
 
Back
Top Bottom