Ni wakati wa Serikali na TFF kusimama na Simba kipindi hiki.

Ni wakati wa Serikali na TFF kusimama na Simba kipindi hiki.

mazaga one

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2015
Posts
2,514
Reaction score
4,042
Wadau wa Michezo na Watanzania wote kwa ujumla,kama mlivyosikia ya kuwa uwanja wa Mkapa umefungiwa na CAF na timu yetu ya Simba hivi karibuni ina mechi ya Robo fainali ya mashindano ya CAF,kama Taifa,tunahitaji kuona serikali ikisimama na Simba kupigania maslahi ya Simba.Tarehe 20/03/2025.Nimeona ya kuwa CAF watakuja kukagua uwanja.Ombi letu ni Serikalai na TFF kuhakikisha wanapigania hili jambo na Simba icheze mechi yake ya marudiano nyumbani.Ukiangalia kwa jicho la mbele ni kwamba Simba inaenda kuchukua hili Kombe na ni kama figisu zishaanza mapema kulidhoofisha Taifa letu.Tupiganie uwanja wetu ufunguliwe mapema na 09/04/2025 mechi ya Robo fainali ichezwe kwa Mkapa na sio ugenini.

Serikali na TFF tuna imani nanyi.
 
HHII NI HUJUMA YA CAF/MISRI DHIDI YA TANZANIA
WANAJUA FIKA TANZANIA ITASHINDA MECHI YAKE YA NYUMBANI WANATAFUTA NAMNA ILI TIMU YA MISRI IPITE.
 
Serikali kupitia Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo imesaini mkataba wa makubaliano ya ukarabati wa Uwanja wa Benjamin Mkapa na Kampuni ya Beijing Construction Engineering Group (BCEG) ya China ambao utagharimu zaidi ya Sh. bilioni 31 hadi kukamilika Julai 2024.

Hayo yamesemwa Dar es Salaam Julai 27, 2023 na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Pindi Chana baada ya kusaini mkataba na kampuni BCEG ya China ambao pia ndio waliojenga uwanja.

Maeneo yaliyopangwa yakarabatiwe ni pamoja na.
1. vyumba vya wachezaji,
2. chumba cha waandishi wa
Habari,
3.Eneo la watu mashuhuri (VVIP), 4. kubadilisha viti vyote vya kukalia mashabiki uwanjani hapo,
5. ubao wa kuonesha matokeo,
kuweka mfumo mpya wa TEHAMA, kubadilisha eneo la kuchezea na seti mbili za magoli ambazo zitatumika uwanjani hapo.

Maeneo mengine ambayo yatafanyiwa ukarabati ni viti vya benchi la ufundi na wachezaji wa akiba,
7. mfumo wa umeme,
8. mfumo wa sauti,
9. Eneo la kukimbilia wanariadha, 10. chumba cha VAR,
11. lifti mbili mpya,
12. mfumo wa taa,
13. mfumo wa maji taka,
14. mgahawa pamoja na vitu vingine ambavyo vimepita muda wa matumizi kwani vilitakiwa kutumika kwa muda wa miaka saba tu
 
HHII NI HUJUMA YA CAF/MISRI DHIDI YA TANZANIA
WANAJUA FIKA TANZANIA ITASHINDA MECHI YAKE YA NYUMBANI WANATAFUTA NAMNA ILI TIMU YA MISRI IPITE.
Yani bora kwa mkapa njia ni nyingi kuingia Tanzania
Ila wakikubali Zanzibar kule njia ni mbili either upite bandarini au airport
Watakufa mapema tu tena kulivyo kudogo kule hehehehehe saa tatu asubuhi mechi imeisha
 
Back
Top Bottom